Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,330
- 45,638
Umewahi kupeleka mahari kisha hukurudi tena na ukaachana na ndoa? Umewahi kutolewa mahari na muoaji hakurudi tena? Umewahi kushuhudia mahari imetolewa na ndoa ikafia njiani?
Kwa kuwa tunafahamu mahari ni hatua ya mwisho kabisa kuelekea ndoa kipi kinaweza kusababisha mahari kutolewa na kupokelewa na ndoa isifanyike kwa mahusiano kufa?
Pia soma:
Mambo ya kuzingatia katika kuchagua mwenza wa maisha
Ikiwa wale wanaokusudia kuoana hawataki kuwa na mashaka mengi wala kuwa na mambo kadha wa kadha ya kuwanyima furaha baada ya kufunga ndoa, imewalazimu kufikiria vyema na kwa moyo wote juu ya jambo hili na kwa wakati huu kabla ya kuoana. Ikiwa hatua hii itafanywa kipumbavu, itakuwa mojawapo ya...
www.jamiiforums.com
Ushuhuda wa mdau
Nimewahi mimi binafsi,, nilitoa mahari, na kumvalisha pete baada ya miezi mitatu alinipigia kwa jeuri na kunitusi kisa nimepeleka mbele tarehe ya harusi hapo ndipo ukawa mwisho wa uchumba wetu, mama yake alichanganyikiwa alitaka wamuombee msamaha ila mimi sikuhitaji suluhu nae tena.