Kustaafu kwa hiari iwe ni muda wowote endapo mtumishi wa umma ataamua kufanya hivyo

Torero

Senior Member
Dec 22, 2017
122
138
Wanadau, muda umefika sasa Sheria kubadilishwa ili itoe Fursa kwa watumishi wa Umma kustaafu kwa hiari muda wowote endapo Mtumishi huyo ataamua kufanya hivyo kwa hiyari yake mweyewe.

Kwa maoni yangu muda wa miaka 55 uliowekwa na Sheria ya sasa wa kustaafu kwa hiari ni kipindi kirefu Sana na unanyima Watumishi wenye nia ya kustaafu mapema haki yao ya maamuzi sahihi.

Matarajio ya kuishi kwa nchi za kiafrika yameshuka sana miaka hii kwa ajili hiyo umri wa kustaafu kwa hiyari miaka 55 No mrefu mnoo Na kustaafu kwa lazima miaka 60 ni vyema kurekebishwa kwa mujibu wa Sheria.

Itasaidia sana kwa watanzania kwa kutoa fursa za wale wasioajiriwa kuajiriwa kwa kuwa wapo watumishi wa umma wengi tu wanahitaji kustaafu mapema zaidi kabla ya kufika umri huo ili kuwapisha Watanzania wengine waingie katika ajira lakini hawawezi kufanya hivyo kwa kuwa wanabanwa na hitaji la kisheria la miaka 55 kustaafu kwa hiari.

Muda muafaka sasa wakati wowote Mtumishi akiamua kustaafu kwa hiari hata akiwa na miaka 40 au 45 aruhusiwe kisheria. Na huo ndio Uhuru wa kujiamulia mambo wayatakayo katika maisha watanzania.

Ni wajibu wangu kutoa maoni na kwamba katiba ya Tanzania, 1977 inaniruhusu kufanya hivyo.
 
Umefikiria vyema sana mkuu hii ni ishara ya weledi katika ubongo wako umetoa kawazo flani ivi kazuri ila tatizo lipo kwa sizonje siunajua unaweza ukajiteka mwenyewe kama nondo
 
Unaruhusiwa kuacha kazi Muda wowote ukitaka Kwa ama kutoa notisi ya Miezi Mitatu Au kurudisha Mshahara wa Mwezi Mmoja in lieu of notice!

Kustaafu kuna Muda wake ambao Ni Miaka 55-60 Ni Kama ilivyo huruhusiwi kuajiriwa Kama Mtumishi wa kudumu ukishafikisha umri wa Miaka 45!

Ni sawa Na kuomba utambuliwe unapumzika kufanya kazi wakati hujachoka, kupumzika maana yake ni kutofanya jambo Fulani kutokana Na Kuchoka lakin ukiacha jambo kufanya kabla hujachoka hatusemi umepumzika tunasema umeacha kufanya jambo fulani
 
Umefikiria vyema sana mkuu hii ni ishara ya weledi katika ubongo wako umetoa kawazo flani ivi kazuri ila tatizo lipo kwa sizonje siunajua unaweza ukajiteka mwenyewe kama nondo
Huwezi kutoa hoja bila kumdhalilisha mwenzako? Una hakika kuwa uliyemtaja alijiteka au ndio wale makinda ya ndege mliozoea kulishwa kila uchafu? Tabia mbaya sana hii!
 
Ni wazo zuri, lakini ukistaafu kabla ya umri wa kustaafu, unaweza usipewe mafao yako hadi ufikishe umri uliowekwa, yaani kama umeamua kustaafu ukiwa na miaka 50, utasubiri hadi ufikishe miaka 55 ndio ulipwe:D:D:D, hii ndio TZ.
 
Ni wazo zuri, ajira zimekuwa chache huku mtaani ukilinganisha na idadi wahitimu vyuoni, vijana wanaomaliza masomo yao na wale wengi waliopo mtaani wazo hili litawasaidia sana vijana wengikupata fulsa ya kuajiriwa serekalini
 
Huwezi kutoa hoja bila kumdhalilisha mwenzako? Una hakika kuwa uliyemtaja alijiteka au ndio wale makinda ya ndege mliozoea kulishwa kila uchafu? Tabia mbaya sana hii!
Mkuu vipi kwani mbona povu linakutoka bhasi sawa wewe uko sahihi kifupi unahoja zamsingi Sana
 
Ni wazo zuri, lakini ukistaafu kabla ya umri wa kustaafu, unaweza usipewe mafao yako hadi ufikishe umri uliowekwa, yaani kama umeamua kustaafu ukiwa na miaka 50, utasubiri hadi ufikishe miaka 55 ndio ulipwe:D:D:D, hii ndio TZ.
Ah wapi!, sasa mtu huyo ataishije??.
 
Hivi mimi kwa mfano nina miaka tuseme 44 nikaamua kuacha kazi hizi za masimango kuna chochote nitalipwa kweli? Na nimewafanyia kazi miaka 8
 
Hii ni sheria ya ufhulumati kabisa na inaoyesha watunga sheria wa huko nyuma walivyo kuwa wamejawa na mioyo ya udhulumati. Kwa nini usimpe mtu haki yake ya huo muda aliotumika? Labda kama hali ya uwezo hairusu.
 
Sijazungumzia kuacha kazi nimeongelea kustaafu kwa hiari mkuu.kuacha kazi na kustaafu kwa hiari ni vitu viwili tafaut kabisa. Jifunze kusoma na kuelewa kabla ya kuandika chochote
 
Unaruhusiwa kuacha kazi Muda wowote ukitaka Kwa ama kutoa notisi ya Miezi Mitatu Au kurudisha Mshahara wa Mwezi Mmoja in lieu of notice!

Kustaafu kuna Muda wake ambao Ni Miaka 55-60 Ni Kama ilivyo huruhusiwi kuajiriwa Kama Mtumishi wa kudumu ukishafikisha umri wa Miaka 45!

Ni sawa Na kuomba utambuliwe unapumzika kufanya kazi wakati hujachoka, kupumzika maana yake ni kutofanya jambo Fulani kutokana Na Kuchoka lakin ukiacha jambo kufanya kabla hujachoka hatusemi umepumzika tunasema umeacha kufanya jambo fulani
Sijazungumzia kuacha kazi mkuu. Nimeongelea kustaafu kwa hiari. Kuwacha kazi na kustaafu ni vitu viwili tofaut. Jifunze kuelewa kabla ya kuandika chochote na kuposti
 
Unaruhusiwa kuacha kazi Muda wowote ukitaka Kwa ama kutoa notisi ya Miezi Mitatu Au kurudisha Mshahara wa Mwezi Mmoja in lieu of notice!

Kustaafu kuna Muda wake ambao Ni Miaka 55-60 Ni Kama ilivyo huruhusiwi kuajiriwa Kama Mtumishi wa kudumu ukishafikisha umri wa Miaka 45!

Ni sawa Na kuomba utambuliwe unapumzika kufanya kazi wakati hujachoka, kupumzika maana yake ni kutofanya jambo Fulani kutokana Na Kuchoka lakin ukiacha jambo kufanya kabla hujachoka hatusemi umepumzika tunasema umeacha kufanya jambo fulani
Mkuu ukitaka acha kazi ukitoa notice ya miezi mitatu bado mshahara wako utakuwa unalipwa kwenye hiyo miezi mitatu
 
Mkuu ukitaka acha kazi ukitoa notice ya miezi mitatu bado mshahara wako utakuwa unalipwa kwenye hiyo miezi mitatu

Yes utakuwa unalipwa Kama kawaida

Kama hutaki kutoa notice ndio unapaswa kulipa basic salary yako then unakuwa umemalizana nao
 
Back
Top Bottom