Kusoma vitabu vingi sio cheo kama wengi wanavyodhani

Singida ndio home

JF-Expert Member
Feb 23, 2012
3,192
3,351
Kumekuwa na tabia ya watu hasa kwenye mitandao ya kijamii kupost rundo la vitabu walivyosoma ndani ya mwaka au hata kuonyesha vyumba vyao special kwajili ya kujisomea vilovyojaa vitabu.

Nachoweza kusema ni kwamba kusoma sio kuelewa bali.......... kusoma bila kuelewa ni kama kuangalia picha kwenye magazeti ila kuelewa ni kama kuangalia picha pamoja na kusoma habari yake.

kusoma sio kujifunza, usiperuzi tu kitabu kama gazeti la michezo uwahi kulimaliza ili uendelee na lengine, Soma vitabu kwa kuvielewa, kuvi tathmini kwa kina na chukulia point za author katika perception yako. Collection yako ya vitabu ulivyosoma sio taji la ushindi endapo hujavielewa.

Kwa mfano mrahisi tu kuna njemba ilipost imemaliza vitabu vitano vya kuishi na watu ikiwemo kitabu maarufu cha how to influence people and win friends lakini cha ajabu ile njemba ukikutana nayo yenyewe inataka kusikilizwa tu bila kusikia unayosema(arrogancy), maringo na dharau za kijinga, eye contact hakuna kabisa yeye yupo na simu.

ndege aliye mkononi ana thamani zaidi kuliko wawili ambapo wapo kichakani, kusoma vitabu vingi endapo na hata kuvikariri kama marking schemes za kujibia mtihani ni upuuzi, soma kwa malengo ili uelewe kitabu na kukitumia in real life na kwa hakika itabu vitakusaidia. Hata ukisoma kitabu kimoja au viwili kwa mwezi sio mbaya endapo utavielewa kuliko kusoma vitabu 50 kwa mwaka na bado havijakusaidia wala hujavielewa.

HAIJALISHI VITABU VINGAPI UMESOMA BALI NI VITABU VINGAPI UMEVIELEWA

MDAU
NAUNGA MKONO HOJA KWA 100%..
Kusoma vitabu vingi bila kufanyia kazi ulichokisoma ni wastage of time and money..
Kusoma ni kuelewa,kufanyia kazi,mwishowe upate tija ya kile ulichokisoma..
Ila wabongo wengi sasa hivi wanafanya usomaji vitabu kama fashion flani hivi ila ukimuangalia huyo anaejifanya msomaji hafanyii kazi hicho anachokisoma..
 
NAUNGA MKONO HOJA KWA 100%..
Kusoma vitabu vingi bila kufanyia kazi ulichokisoma ni wastage of time and money..
Kusoma ni kuelewa,kufanyia kazi,mwishowe upate tija ya kile ulichokisoma..
Ila wabongo wengi sasa hivi wanafanya usomaji vitabu kama fashion flani hivi ila ukimuangalia huyo anaejifanya msomaji hafanyii kazi hicho anachokisoma..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NAUNGA MKONO HOJA KWA 100%..
Kusoma vitabu vingi bila kufanyia kazi ulichokisoma ni wastage of time and money..
Kusoma ni kuelewa,kufanyia kazi,mwishowe upate tija ya kile ulichokisoma..
Ila wabongo wengi sasa hivi wanafanya usomaji vitabu kama fashion flani hivi ila ukimuangalia huyo anaejifanya msomaji hafanyii kazi hicho anachokisoma..

Sent using Jamii Forums mobile app
kuna wasomaji wanasoma vitabu vingi hadi 60 kwa mwaka, ila katika hawa wasomaji wa vitabu wale walioelimika kupitia hivi vitabu ni mmoja kati ya wasomaji 20:):) upo 100& real
 
Unazingua mkuu! Elimu ni kile kinachobaki/ unachokikumbuka baada ya kusahau mengine. Sio ukisoma kitabu unategemea kuelewa kila mstari.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni lazima uelewe kitabu kinakufundisha nini na ndio lengo la kusoma vitabu, ukisoma viabu kama unavyokariri marking schemes au kusoma kwa juu juu bila kukielewa ni kupoteza muda.
 
Kusoma ni kipaji. Mshana Jr kasoma elimu ngumu kuliko zote duniani inaitwa kallabah, kwa elimu hiyo unaweza kuwa mchawi au ukawa nabii
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom