Lizaboni
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 33,894
- 20,372
Wadau, amani iwe kwenu.
Watu hawashiriki kwenye maandamano kwa kushawishiwa. Maandamano ni utashi wa mtu na hushiriki tu kwa kuwa ameguswa. Maandamano ya kushawishiwa kwenye mikutano na waandishi wa habari ama kwenye mitandao ya kijamii siku zote hayafanikiwi.
Wananchi wakiguswa hata utumie vifaru huwezi kuwanyamazisha. Maandamano ya CHADEMA na ACT Wazalendo hayakuwa na hisia za wananchi bali yaliitishwa na watu waliokosa ulaji kupitia sanduku la kura.
Wananchi wanajua wazi kuwa Ushindi wa CCM ni wa halali hivyo wameamua kuwapuuza waandaaji wa maandamano hayo. Maandamano ya CHADEMA na ACT Wazalendo hayakuwa na hisia za wananchi bali yalisukumwa na genge la watu lililokuwa linapigania maslahi binafsi.
Hivyo tunahitimisha kuwa Ushindi wa CCM ni halali kabisa na wananchi wameamua kuwaadhibu CHADEMA na ACT Wazalendo kupitia sanduku la kura na kupitia maandamano feki.
Hongereni sana Waheshimiwa Wananchi. Ninyi ni zaidi ya Wale Wajumbe wa CCM. Mmetuheshimisha Watanzania. Mmewatia adabu CHADEMA na ACT Wazalendo kupitia sanduku la kura na kukataa maandamano yao
Watu hawashiriki kwenye maandamano kwa kushawishiwa. Maandamano ni utashi wa mtu na hushiriki tu kwa kuwa ameguswa. Maandamano ya kushawishiwa kwenye mikutano na waandishi wa habari ama kwenye mitandao ya kijamii siku zote hayafanikiwi.
Wananchi wakiguswa hata utumie vifaru huwezi kuwanyamazisha. Maandamano ya CHADEMA na ACT Wazalendo hayakuwa na hisia za wananchi bali yaliitishwa na watu waliokosa ulaji kupitia sanduku la kura.
Wananchi wanajua wazi kuwa Ushindi wa CCM ni wa halali hivyo wameamua kuwapuuza waandaaji wa maandamano hayo. Maandamano ya CHADEMA na ACT Wazalendo hayakuwa na hisia za wananchi bali yalisukumwa na genge la watu lililokuwa linapigania maslahi binafsi.
Hivyo tunahitimisha kuwa Ushindi wa CCM ni halali kabisa na wananchi wameamua kuwaadhibu CHADEMA na ACT Wazalendo kupitia sanduku la kura na kupitia maandamano feki.
Hongereni sana Waheshimiwa Wananchi. Ninyi ni zaidi ya Wale Wajumbe wa CCM. Mmetuheshimisha Watanzania. Mmewatia adabu CHADEMA na ACT Wazalendo kupitia sanduku la kura na kukataa maandamano yao