Zanika
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 1,316
- 752
Kumezuka tabia mbaya sana na yenye kila viashiria vya kutaka kuwabagua Watanzania. Hili limekuwa gumzo kubwa la wasiopenda cake ya Taifa iende kila mahali baki kwao tu.
Kwa kisingizio kuwa Kuongozi akitoka mahali fulani basi maendeleo yasipelekwe huko bali yaendelee kwenda kwao kwa sababu itakuwa ni upendeleo na dhambi kubwa kuendeleza anakotoka kiongozi Mkuu.
Huu kwangu ni uchoyo na uchonganishi wenye nia ovu ya kuligawa Taifa.
Nazungumza hivi ni kiwa ni Mzaliwa wa Kaskazini na ambaye nimeshuhudia miongo ambayo kwetu tumependelewa sana tangu Uhuru kuanzia Umeme hadi miundo.binu nk. Tumekuwa na kawaida ya kuwahadaa wenzetu kuwa maendeleo yanaenda kwetu kwa sababu tumesoma nk.
Nakumbuka hata Mh: Nagu aliwahi kulalamikiwa kuwa kuna idara na Wizara fulani zimejaa watu wa Kaskazini na moja ya majibu aliyojibu ni kuwa sio kosa kwa watu wa Kaskazini kujazana TRA kwa sababu ndio waluosomea taaluma hizo, akaongeza kuwa kama jamii zingine zinataka kufanya huko waende wakasome na wao wataajiriwa.
Tulishangilia sana hili huku tukisahau kuwa kauli zile ndizo zilikuwa Alalaye usimwamshe kwani akiamka utalala wewe. Na hili ndilo limetumia sasa ambapo mnaona kuna wanasiasa wanatumia Mwanya huo huo kujiimarisha kwa kutoa kauli za kibaguzi huku wakisahau kuwa wao ndio waliopanda mbegu hizi.
Kutoka Mwanza hadi Bukona ni km 446
Kutoka Bukoba hadi Chato ni km 220
Geita hadi chato ni km 118
Na Moshi hadi Arusha ni km 119
Sasa miji ya Moshi na Arusha yote ina Airport ndogo halafu ikajengwa International Airport kubwa mpakani mwa miji hiyo mitatu yaArusha,Manyara na Moshi, na watu wa Manyara hawalalamiki kukosa Airport ingawa eneo lao lina activities za migodi,Utalii,Kilimo na Ufugaji.
Je sio Bisara kwa Serikali kutafuta eneo ambalo ni rahisi kifikika kutokea pande zote tajwa hapo juu na kujenga International Airport ili watu wa zone hiyo ya Kaskazini Magharibi(Nyanza) wote wafikie huduma km ilivyo Kule Kaskazini KIA?
Tujiulize faida itakayopatikana kwa uwekezaji huu si inaenda Serikalini na kupanua wigo wa upatikanaji wa fedha za Maendeleo tunazopewa kwenye Mikoa yetu kupitia idara mbalimbali?
Sambamba na hili Mbeya uwanja unaboreshwa na kuwa wa hadhi ya Kimataifa, mbona hatusikii kelele zikipigwa kuwa labda wanapendelewa?
Mtu atakuja na hoja kwamba kwanini Mwanza Airport isiboreshwe,lkn wengi wetu tuliofika pale tunajuajinsi palivyo padogo na changamoto zinazoikabili uwanja ule Mvua kubwa ikinyesha
Namaliza kwa kusema tusirubuniwe kwa kupotoshwa na wasiopenda maendele ya Taifa letu bali tupendane tuvumiliane pale unapoona mkate fulani umepelekwa kwa jirani yako.
Kikubwa ni nchi yetu sote km unaona sehemu fulani fursa zinaibukia huko jipange uwahi ukakamate hizo fursa, na hii ndio raha ya uhuru tulionaousiobagua Kabila au Ukanda.
Tuache roho mbaya na kugawa Taifa letu kwa ubaguzi huu unaofanywa na Upinzani.
Kwa kisingizio kuwa Kuongozi akitoka mahali fulani basi maendeleo yasipelekwe huko bali yaendelee kwenda kwao kwa sababu itakuwa ni upendeleo na dhambi kubwa kuendeleza anakotoka kiongozi Mkuu.
Huu kwangu ni uchoyo na uchonganishi wenye nia ovu ya kuligawa Taifa.
Nazungumza hivi ni kiwa ni Mzaliwa wa Kaskazini na ambaye nimeshuhudia miongo ambayo kwetu tumependelewa sana tangu Uhuru kuanzia Umeme hadi miundo.binu nk. Tumekuwa na kawaida ya kuwahadaa wenzetu kuwa maendeleo yanaenda kwetu kwa sababu tumesoma nk.
Nakumbuka hata Mh: Nagu aliwahi kulalamikiwa kuwa kuna idara na Wizara fulani zimejaa watu wa Kaskazini na moja ya majibu aliyojibu ni kuwa sio kosa kwa watu wa Kaskazini kujazana TRA kwa sababu ndio waluosomea taaluma hizo, akaongeza kuwa kama jamii zingine zinataka kufanya huko waende wakasome na wao wataajiriwa.
Tulishangilia sana hili huku tukisahau kuwa kauli zile ndizo zilikuwa Alalaye usimwamshe kwani akiamka utalala wewe. Na hili ndilo limetumia sasa ambapo mnaona kuna wanasiasa wanatumia Mwanya huo huo kujiimarisha kwa kutoa kauli za kibaguzi huku wakisahau kuwa wao ndio waliopanda mbegu hizi.
Kutoka Mwanza hadi Bukona ni km 446
Kutoka Bukoba hadi Chato ni km 220
Geita hadi chato ni km 118
Na Moshi hadi Arusha ni km 119
Sasa miji ya Moshi na Arusha yote ina Airport ndogo halafu ikajengwa International Airport kubwa mpakani mwa miji hiyo mitatu yaArusha,Manyara na Moshi, na watu wa Manyara hawalalamiki kukosa Airport ingawa eneo lao lina activities za migodi,Utalii,Kilimo na Ufugaji.
Je sio Bisara kwa Serikali kutafuta eneo ambalo ni rahisi kifikika kutokea pande zote tajwa hapo juu na kujenga International Airport ili watu wa zone hiyo ya Kaskazini Magharibi(Nyanza) wote wafikie huduma km ilivyo Kule Kaskazini KIA?
Tujiulize faida itakayopatikana kwa uwekezaji huu si inaenda Serikalini na kupanua wigo wa upatikanaji wa fedha za Maendeleo tunazopewa kwenye Mikoa yetu kupitia idara mbalimbali?
Sambamba na hili Mbeya uwanja unaboreshwa na kuwa wa hadhi ya Kimataifa, mbona hatusikii kelele zikipigwa kuwa labda wanapendelewa?
Mtu atakuja na hoja kwamba kwanini Mwanza Airport isiboreshwe,lkn wengi wetu tuliofika pale tunajuajinsi palivyo padogo na changamoto zinazoikabili uwanja ule Mvua kubwa ikinyesha
Namaliza kwa kusema tusirubuniwe kwa kupotoshwa na wasiopenda maendele ya Taifa letu bali tupendane tuvumiliane pale unapoona mkate fulani umepelekwa kwa jirani yako.
Kikubwa ni nchi yetu sote km unaona sehemu fulani fursa zinaibukia huko jipange uwahi ukakamate hizo fursa, na hii ndio raha ya uhuru tulionaousiobagua Kabila au Ukanda.
Tuache roho mbaya na kugawa Taifa letu kwa ubaguzi huu unaofanywa na Upinzani.