Kusaidia Ndugu/familia ni wajibu au lazima?

hii kitu ngumu sana ndugu zangu...tunapaswa kuwasaidia hakika...ila ukicheza hao ndio watakuangusha.....nlishawasomesha shemeji zangu duh...mie sikufika univ....hakika nliwalipia kwa kuunga unga.....walichokuja kuniambia....ila nimewasamehe kabisa...eti " kama baba etu angekuwepo angeweza kutosomesha...tukipata kazi tutakurudishia" na wamepigika na digrii zao...wacha...mmoja fundi simu posta,,,,mwingine keshatunguliwa 2 na baba tofauti......mie nadunda tuuu....adabu imewakaa....
Ungewaambia waache ungese wao.
 
Ubinafsi si mzuri kama una nafasi au kipato saidia tu wenye uhitaji kwa kufanya hivyo unajenga koo au familia yenye nguvu kiuchumi na maamuzi ktk jamii
Swali langu ni kwamba wakati mimi napambana wao walikua wanafanya nini!?

mana hapa naona tunapeana ulemavu na ufukara.

nadhani ni vema kubadili mifumo ya maisha yetu kuiboresha mara mbili Au zaidi ya tulipotoka.

leo hii siwezi ona mtoto wangu aje kusomeshwa na mtu.

lengo ni kurithisha uwezo mbele zaidi.
Tuache hizi style za kizee.
 
Kwa andiko hili naamini wewe ni mcha Mungu na bila shaka ni mtu mwenye mafanikio. What a great thinker! Thanks.
Hapa pia kuna tatizo.

ata imani ilisema asiyefanya kazi na asile.

lengo langu ni kizazi chetu nije kurithisha mafaniko sio shida.

mtegemea cha ndugu hufa maskini.

kusaidia kusiwe sababu ya kisingizio cha kutofanikiwa.

kuamini Mungu ni imani ya mtu.
(With respect)

lakiki tukitumia vibaya imani pia inaleta chanzo cha ufukara.
 
Ubinafsi si mzuri kama una nafasi au kipato saidia tu wenye uhitaji kwa kufanya hivyo unajenga koo au familia yenye nguvu kiuchumi na maamuzi ktk jamii
Ukijaribu kutazama kwa ukaribu
Siri mojawapo ya mafanikio ni UBINAFSI.

Hata mti uweze kwenda juu zaidi unahitaji ukate baadhi ya matawi.

Kama kipato chako kinamzigo wa kuhudumia wengine na bado hakikutoshi
You are a definition of “LOOSER”
 
Jamani jamani wapendwa

Kuna watu humu tumepata mafanikio kutokana na kulelewa na watu ambao sio wazazi wa kutuzaa. Kuna baadhi wazazi wenu walilelewa na wajomba/bamkubwa and all the like.

Upendo ni kitu kidogo sana. Sikulazimishi kupenda lakini upendo unalipa. Kuna mahali unapata msaada usifkiri ni wewe hapana ni sadaka ya mzazi wako alimlea mtu au kumsaidia mtu.

Binafsi yangu wengi walionisaidia kufika hapa sio ndugu wa ukoo ni watu baki kabisa..sikuwafahamu..

Mnahisi connection zinatoka wapi???ishi na watu vizuri na Mungu atakuinulia watu wa kukushika mkono somewhere. Hakuna asiyehitaji msaada nenda hata kwenye biblia akina Yusufu pale ambapo walitajwa kwa Farao yote kwa kumtafsiria mtu ndoto...

#tupendanewapendwalifeistooshorttohate#
Forget history
Maisha ya sasa yanaruhusu vipi!?

kwanza hizi connection unataja sio za haki mara zote. Most likely ni kupeana priority in a shortcut way.

Hoja yangu sio kupunguza upendo “NO”

Sababu moja wapo ya kurudishana nyuma ni familia/ndugu kubweteka kwa kutegemea mwingine.

Umenisoma!?
 
Forget history
Maisha ya sasa yanaruhusu vipi!?

kwanza hizi connection unataja sio za haki mara zote. Most likely ni kupeana priority in a shortcut way.

Hoja yangu sio kupunguza upendo “NO”

Sababu moja wapo ya kurudishana nyuma ni familia/ndugu kubweteka kwa kutegemea mwingine.

Umenisoma!?
Nimekuelewa sana tu

Basi kwa kujazia...kama mtu umefika ulipofika kwa msaada wa watu kadhaa, yakupasa na wewe kuwasaidia wenye uhitaji wa kweli. Sisupport wanaobweteka lakini na wewe play a certain role in someones life. Kama unaweza kusaidia hata wasiokuhusu do it.....

Nweiz kila mtu anaweza simamia anachoona kinafaa. Bless you all
 
Ndugu ni baba mama mwanao, na kaka au dada uliozaliwa nao tumbo moja... Hao wengine ni wajinga kama wajinga wengine huna haja ya kuwasaidia hata wakiumwa mahutut...
 
Kwenye suala kama hiliinategemea na familia.
Kama wewe familia ilikuchangia kukusomesha mpaka unapata kazi , hivyo nawe lazma tu utajikuta upo kwenye hako kamfumo na kwa sababu ulisaidiwa nawe saidia kama uwezo unao.
Ila kuna familia nyingine kila mtu na kafamilia kake (nucleur family base) kila mtu na habar zake , tukutane kwenye matukio ya kijamii tu .
Na mara nyingi mifumo kubadilika ni ngumu sana , sasa inategemea umekualia katka mfumo gani .
Ila suala jingine kama una uwezo wa kumsaidia mtu msaidie tu kama huna basi .
 
Nimeona sehem nyingi, familia nyingi na hata mmoja wa polisi aliyefariki kwa tukio la Juzi inaonesha kua alikua tegemeo la familia nzima mpaka mtoto wa kaka yake.

Hoja yangu ni moja.
Hii ni tamaduni au ni vipi!?

Unamaliza shule, unapata kazi baada ya hapo unatakiwa kusaidia familia nzima na ndugu wa pembeni(kitanzania)

Mtazamo wangu:
hii ni moja ya kurudishana nyuma kimaendeleo

Nilidhani ni vema iwe kutazama future ya yako kwanza na kuhudumia/kusaidia wengine isiwe ni wajibu/lazima bali iwe HIYARI kulingana na uwezo wa mtu.
Inategemea umetoka familia gani, hizi familia zetu mzazi unakuta mjasiliamali mdogo hana kipato kikubwa,mzazi anakusomesha kwa tabu we na wadogo zako, bahati nzuri wewe umetoboa mzazi kazeeka hana nguvu za kutafuta hela kama zamani, wewe kama mtoto huo ni wajibu wako kumsaidia mzazi wako na wadogo zako bila kusahau kumtunza mzazi wako kwani unaweza ukakuta hana bima ya Afya. Haya ndio maisha ya watoto wengi walitoboa kutoka familia duni.

Ila kama familia bora hela yako fanyia mambo yako binafsi.
 
Acha choyo naimani na ww umepita hizo njia pia na ww kuna kipind huenda ulionekana kero kuomba omba lkn huenda ulisaidiwa usiwe na roho ya kukunja mzee saidia pale unapoweza na sio ujione umeshamaliza mwendo
 
Inategemea umetoka familia gani, hizi familia zetu mzazi unakuta mjasiliamali mdogo hana kipato kikubwa,mzazi anakusomesha kwa tabu we na wadogo zako, bahati nzuri wewe umetoboa mzazi kazeeka hana nguvu za kutafuta hela kama zamani, wewe kama mtoto huo ni wajibu wako kumsaidia mzazi wako na wadogo zako bila kusahau kumtunza mzazi wako kwani unaweza ukakuta hana bima ya Afya. Haya ndio maisha ya watoto wengi walitoboa kutoka familia duni.

Ila kama familia bora hela yako fanyia mambo yako binafsi.
Siku hizi nikisikia mtu anasema hasaidii mtu huwa namuelewa sana binafsi dingi yangu alikuwa first born na alisaidia wadogo zake wote almost 8 na ndugu wapembeni lakini baada ya kifo chake hakuna hata mmoja aliyetupa msaada hata katika nyakati ngumu tulizopitia.
 
Kama walikusomesha kwa kujinyima, itabidi nawe ujinyime ili usaidie kwa kadiri ya uwezo wako. Ila chunga wema usizidi uwezo.
 
Siku hizi nikisikia mtu anasema hasaidii mtu huwa namuelewa sana binafsi dingi yangu alikuwa first born na alisaidia wadogo zake wote almost 8 na ndugu wapembeni lakini baada ya kifo chake hakuna hata mmoja aliyetupa msaada hata katika nyakati ngumu tulizopitia.
Sawa ila angalia walio kunyanyua kwani uliyetafuta naye kuni ndiye wakuota nae moto.
 
Nimeona sehem nyingi, familia nyingi na hata mmoja wa polisi aliyefariki kwa tukio la Juzi inaonesha kua alikua tegemeo la familia nzima mpaka mtoto wa kaka yake.

Hoja yangu ni moja.
Hii ni tamaduni au ni vipi!?

Unamaliza shule, unapata kazi baada ya hapo unatakiwa kusaidia familia nzima na ndugu wa pembeni(kitanzania)

Mtazamo wangu:
hii ni moja ya kurudishana nyuma kimaendeleo

Nilidhani ni vema iwe kutazama future ya yako kwanza na kuhudumia/kusaidia wengine isiwe ni wajibu/lazima bali iwe HIYARI kulingana na uwezo wa mtu.
Familia zetu za Kitanazania nyingi ni maskini ! Kwa hiyo kama unao uwezo wa kusaidia hasa upande wa elimu usisite kufanya hivyo ili kuongeza wasomi watika ukoo wenu. Mungu akusaidie ili uweze kulitambia hilo.
 
Back
Top Bottom