Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu inauza Habari za ofisi ya Rais Kikwete

Michuzi ndio anaonekana yuko fasta zaidi. Hata hivyo Maro ni mpiga picha rasmi wa ikulu. Huenda urasimu nao huchangia katika suala hili hasa ukizingatia kila mtu anafanya kazi asijiweke katika mazingira mabaya na wengine.
 
Siwezi kubishana kwa hilo ya wezekekana one is a subordinate to the other, lakini Issa anatambulishwa rasmi kama mpiga picha wa rais na picha zote za shughuli za rais ni product yake.

Last time I checked, Issa Michuzi alitambulika kama Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi. Kwa order of seniority anaanza Salva Rweyemamu kama Mkurugenzi akifuatia Bi. Premi Kibanga - Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi. Kwenye Kurugenzi hiyo pia kuna mpiga picha wa Rais Freddy Maro. Na kwa ninavyofahamu pia kuna maafisa habari wawili kwenye idara hiyo hiyo. Sasa Anko yuko kwenye level gani sijui, ila common sense yangu inanituma kwamba yupo sawa na Freddy Maro lakini sio kwa cheo cha Mpiga Picha wa Rais maana kazi za Uandishi wa Habari wa wanasiasa/makampuni/mataasisi zina mambo mengi kulingana na human resource na nature ya kazi. Kwa mfano ofisi zingine Afisa Mawasiliano/Mwandishi wa Habari wa Mwanasiasa/kampuni pia anaweza ku-double kama Speech-writer pia. Hii ni jambo la kawaida, kwahiyo sishangai kwa Anko kukamata Nikon yake na kuanza kutwanga picha.
 
Muhidin Michuzi ni mpigapicha wa Rais tangu lini ? Ninachojua Michuzi alienda Ikulu kipindi kifupi kupiga picha kwa ajili ya blog yake. Mpiga picha wa Rais hivi sasa ni Freddy Maro.
 
Muhidin Michuzi ni mpigapicha wa Rais tangu lini ? Ninachojua Michuzi alienda Ikulu kipindi kifupi kupiga picha kwa ajili ya blog yake. Mpiga picha wa Rais hivi sasa ni Freddy Maro.
fredy maro huyo hana ubavu kama michuzi..misafara mingi michuzi yupo na jk....si unajua ushkaji tena
 
Michuzi ndio anaonekana yuko fasta zaidi. Hata hivyo Maro ni mpiga picha rasmi wa ikulu. Huenda urasimu nao huchangia katika suala hili hasa ukizingatia kila mtu anafanya kazi asijiweke katika mazingira mabaya na wengine.

inaonekana mkulu wa nchi ali force tu kumuingiza michuzi, kujuana ndiyo zake
 
Ninaendelea kuwashukuru wale wote waliotoa na wameendelea kutoa mchango wao katika msingi wa hoja za kujenga taifa endelevu katika bandiko langu.

Ni haki na wajibu wetu kuikumbusha Ikulu na hasa Rais ili atende wajibu wake katika misingi ya usawa kwa wananchi wake.

Kwa vile wanaendelea kutumia kodi zetu, na sisi hatutachoka kuwaeleza na kuwakosoa pale wanapoiacha njia ya haki na usawa kwa raia wake ambayo walikula viapo kuifuata.
 
Sichangii Mada yako ila umeniudhi kuweka msemo wa kiingereza ambao wahenga wetu pia wanao. Kwani ungesema "Msemakweli ni mpenzi wa Mungu" ungepungukiwa nini?
Mkuu,
Unasema huchangii mada yangu wakati umeishachangia!

Kile kitendo cha kuandika ujumbe wowote na kukiweka hapa kinahesabika ni mchango.

Ninashukuru kwa mchango wako!
 
Nijuavyo mimi Michuzi ni mpiga picha wa rais, hivyo ana access ya moja kwa moja na shughuli za kikazi za rais (Mf. ziara ya rais Marekani). Kuzuia upakuaji picha na taarifa ktk blog yake kwangu mimi, ni ulinzi ili zisije tumiwa vibaya na ikachukuliwa source ni yeye. "Tuelomishane"


Aiseee..!hebu tuelewesheni taratibu,mbona mnaongea harakaharaka?taarifa zianze kuwekwa wapi kati tovuti ya ikulu na ya michuzi?mi bado nawaza Escrow mjue?
 
Mambo ya Tz yanapunguza umri wangu wa kuishi duniani.watu wanahoja nzito sana halafu hakuna mtu wa kutoa majibu.tunaishije wakuu?
 
Hii habari imenisikitisha sana ... yaani ofisi kubwa namna hiyo nayo imekuwa ya kiubabaishaji kiasi hichoo... Mungu wa mbinguni tusaidie na kuwarehemu wahusika maana ni ufisadi wa hali ya juuu ... ofisi kuendeshwa kiswahili swahili ni hatari sana....
 
Mambo ya Tz yanapunguza umri wangu wa kuishi duniani.watu wanahoja nzito sana halafu hakuna mtu wa kutoa majibu.tunaishije wakuu?
Hawa wana siasa akina chadema hawalioni hili? kwanini wasilipue bungeni?
 
Hivi majuzi yalitolewa madai ya Kwamba kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inauza habari na imekasimisha habari za Rais kimaslahi kwa watu wengine na hasa kwa blog ya mwananchi mmoja anayeitwa Muhidin Issa Michuzi.

Mara ya kwanza sikuona sababu ya kuchangia hoja hiyo wala kuitolea ufafanuzi ama jibu, lakini kwa mara nyingine shutuma hiyo imejirudia katika mitandao mingine ya kijamii, hivyo nikajikuta nashawishika kuchangia hoja hiyo na kumweleza aliyeijenga na kuitoa:-

Kwanza, naamini kuwa Kurugenzi imesikia na inaifanyia kazi hoja hii. Isipokuwa niseme mawili tu ambayo nayaelewa kiundani:

· Kubwa ambalo nina uhakika nalo ni kwamba kamwe haijapata na haitatokea kwa Kurugenzi ya IKULU kuuza ama kukasimisha kimaslahi habari za Rais na Ikulu kwa mtu ama kwa kikundi cha watu. Madai haya ni sehemu tu ya politics za kawaida za media scene ya hapa kwetu Tanzania. Kila mtu anamtafuta mtu, kama vile hakuna mambo ya maana zaidi ya kuhangaika nayo.


· Jambo moja ni dhahiri sana. Ndani ya Kurugenzi ile wanaofanya kazi ni binadamu kama alivyo mjenga hoja mwenyewe. Hivyo, wanaweza wasiwe watu wenye uwezo wa kupindukia sana. Lakini Kurugenzi ile ina watu makini sana, wenye kuelewa wanafanya nini na wenye maadili ya msingi kabisa ya utumishi wa umma. Madai kwamba wanaweza kuuza habari za Rais ni completely laughable.

Tuendelee kujadili kwa hoja na weledi, uzushi na tuhuma zisizo na msingi kila wakati hazina maana.
 
Kumbe huyu menezi wa chama cha kijani ni msemaji wa Sefue ..... au unatafuta visifa vya uongo

Mbona hukanushi ya Sethi
 
umesomeka mkuu wasikubabaishe hao wazushaji wa mambo kwa faida zao
ACHANA NAO
 
issue ikiongelewa bungeni moja kwa moja inaingia kwenye records za bunge,nilitegema mapema kabisa hii ikanushwe?including ya prosper mbena,cha kushangaza wamesubiri hadi mzee wa tezi dume arudi ndo wakanushe,hii ina ashiria nini,ni kwamba wameambia mkaseme hivi................hii ndo tanzania bwana
 
Hivi majuzi yalitolewa madai ya Kwamba kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inauza habari na imekasimisha habari za Rais kimaslahi kwa watu wengine na hasa kwa blog ya mwananchi mmoja anayeitwa Muhidin Issa Michuzi.

Mara ya kwanza sikuona sababu ya kuchangia hoja hiyo wala kuitolea ufafanuzi ama jibu, lakini kwa mara nyingine shutuma hiyo imejirudia katika mitandao mingine ya kijamii, hivyo nikajikuta nashawishika kuchangia hoja hiyo na kumweleza aliyeijenga na kuitoa:-

Kwanza, naamini kuwa Kurugenzi imesikia na inaifanyia kazi hoja hii. Isipokuwa niseme mawili tu ambayo nayaelewa kiundani:

· Kubwa ambalo nina uhakika nalo ni kwamba kamwe haijapata na haitatokea kwa Kurugenzi ya IKULU kuuza ama kukasimisha kimaslahi habari za Rais na Ikulu kwa mtu ama kwa kikundi cha watu. Madai haya ni sehemu tu ya politics za kawaida za media scene ya hapa kwetu Tanzania. Kila mtu anamtafuta mtu, kama vile hakuna mambo ya maana zaidi ya kuhangaika nayo.


· Jambo moja ni dhahiri sana. Ndani ya Kurugenzi ile wanaofanya kazi ni binadamu kama alivyo mjenga hoja mwenyewe. Hivyo, wanaweza wasiwe watu wenye uwezo wa kupindukia sana. Lakini Kurugenzi ile ina watu makini sana, wenye kuelewa wanafanya nini na wenye maadili ya msingi kabisa ya utumishi wa umma. Madai kwamba wanaweza kuuza habari za Rais ni completely laughable.

Tuendelee kujadili kwa hoja na weledi, uzushi na tuhuma zisizo na msingi kila wakati hazina maana.

Nape kumbe wewe ni mwenezi na msemaji mpaka ikulu kazi kweli kweli. Hebu tufafanulie pia yale maelezo aliyoyatoa Rais pale JNIA kuhusu tezi dume ndio ilikua hotuba ya mwisho wa mwezi?
 
Ila binafsi sipendezwi na tabia ya kuanika anika habari za rais , ni kumdhalilisha rais. Mfano picha zile rais kapigwa anabembea kule Jamaica, zile za kupiga na 50 cent , mm naona anayezipiga au kusambaza hamfanyii fea rais wa nchi!!
 
Back
Top Bottom