Kurudisha kodi ya kichwa nyakati hizi za ulimwengu ulioendelea ni aibu kubwa. Mwigulu Nchemba kuwa na aibu. Mbona kuna vyanzo mbadala vingi

Kwanza ieleweke wazi kuwa kodi ya itayolipwa na wananchi kupitia manunuzi ya vocha za simu ni sawa na kodi ya kichwa waliokuwa wanatoza wakoloni kisha tukairithi na baadae kuondolewa miaka tisini baada ya kuwa ni kodi inayodhalilisha watu.

Kwamba ukiongeza salio unakatwa pesa ili kuchangia maendeleo hii ni aibu. Yaani hata wanachi wasiojiweza ambao wakiongeza salio la buku watachachangia kodi? Kisa tu tuna miradi mikakati kama Sgr na hatuna pesa

Kama tunahitaji pesa za kukamilisha miradi mkakati kwa nini tusikusanye kodi kupitia uvuvi wa bahari kuu ambako kuna kodi nyingi inapotea kwa kuibiwa na meli kibao za uvuvi toka mataifa ya kigeni?

Kodi ya kichwa ni aibu kubwa karne hii.


Unaweza kuainisha maeneo ambayo yanaweza kuwa vyanzo mbadala ya kodi? Kodi inahitajika sana maana maendeleo yetu na matumizi ya bunge na serikali, yanategemea ukusanyaji kodi.
Tuone aibu kama mpaka leo 40% ya budget inachangiwa na wahisani
 
Uvccm si mkalinde hizo meli zisiibe, au kazi yenu ni kukimbia na mabox ya kura tu?
Ahaaaaa, where have you been young brother tindo? Ahaaaa. Habari za kura zinaingia wapi hapa? Tunatakiwa tukusanye mapato kwa manufaa ya umma kuliko kuwa na kodi zisizo na tija.
 
Kwanza ieleweke wazi kuwa kodi ya itayolipwa na wananchi kupitia manunuzi ya vocha za simu ni sawa na kodi ya kichwa waliokuwa wanatoza wakoloni kisha tukairithi na baadae kuondolewa miaka tisini baada ya kuwa ni kodi inayodhalilisha watu.

Kwamba ukiongeza salio unakatwa pesa ili kuchangia maendeleo hii ni aibu. Yaani hata wanachi wasiojiweza ambao wakiongeza salio la buku watachachangia kodi? Kisa tu tuna miradi mikakati kama Sgr na hatuna pesa

Kama tunahitaji pesa za kukamilisha miradi mkakati kwa nini tusikusanye kodi kupitia uvuvi wa bahari kuu ambako kuna kodi nyingi inapotea kwa kuibiwa na meli kibao za uvuvi toka mataifa ya kigeni?

Kodi ya kichwa ni aibu kubwa karne hii.
Hii kodi safi sana!! Ni njia pekee ya kuhakikisha kuwa kila mtanzania analipa kodi!
 
Ingawa ni kweli bado kuna maeneo mengi ambayo hayajaguswa ili kuwa sehemu ya mapato ya serikali,

Lakini kwenye kodi ya Laini, naunga mkono, watu walipie line zao, Kama mtu ataona mzigo abaki na laini moja, maana hizi laini zimekuwa ni kama sehemu za weengi sana kujipatia kipato kwa njia ya udanganyifu, ingawa pia hilo TCRA inaweza kuwa sehemu ya kulaumiwa
Kwahyo ikitozwa kodi, hakutakuwa na makosa ya kujipatia kipato kwa njia ya udanganyifu??
 
Lazima kila raia alipe kodi ndiyo uzalendo wa kweli ila watoto, vikongwe au walio na ulemavu wa kushindwa kufanya shughuli wao hawawajibiki kulipa kodi.

Mfano Tanzania daftari la wapiga kura mamilioni wenye kazi sekta kama waajiri serikalini, sekta binafsi na waliojiajiri wauza mitumba, wakulima, wavuvi , wafugaji , madalali, mishemishe za mjini n.k ambao wote hawa wanaendesha maisha yao kwa kazi zao lazima walipe kodi inayofanana na ya PAYE. Jumla yao ni 29,000,000 Idadi ya wapiga kura Tanzania waongezeka

Nadhani hakuna namna nyingine hata hawa kina babu na bibi wanatakiwa kuwa wazalendo hawaoni mabarabara, ma-flyover, stendi za mabasi wilaya zote, hospitali za wilaya / rufani, shule zikichipuka kama uyoga kila kona ya nchi lazima kuna ulazima kuvichangia tunaambiwa hatuna mjomba ktk nchi za Mabeberu alete misaada wakati rasilimali watu mamilioni waTanzania wanaoendesha maisha yao kila siku wapo, na bila kusahsu maliasili, utalii, makampuni n.k vipo nchini Tanzania.

Tupewe elimu ya kweli walipa kodi ya "kichwa" tunaofikia watu 29,000,000


Itakuwa vizuri mishahara yao hao wabunge nayo ikatwe kodi, wachangie BIMA ya afya, pia wachangie kiinua mgongo maana wanahubiri uzalendo lakini hakuna wanachochangia kutoka kwenye mishahara yao japo wanalipwa mamilioni, na bado nyumba bure, bima bure, kiinua mgongo wanapewa bure japo hawachangii, na mafta ya gari bure, yani kila kitu bure
 
Kwanza ieleweke wazi kuwa kodi ya itayolipwa na wananchi kupitia manunuzi ya vocha za simu ni sawa na kodi ya kichwa waliokuwa wanatoza wakoloni kisha tukairithi na baadae kuondolewa miaka tisini baada ya kuwa ni kodi inayodhalilisha watu.

Kwamba ukiongeza salio unakatwa pesa ili kuchangia maendeleo hii ni aibu. Yaani hata wanachi wasiojiweza ambao wakiongeza salio la buku watachachangia kodi? Kisa tu tuna miradi mikakati kama Sgr na hatuna pesa

Kama tunahitaji pesa za kukamilisha miradi mkakati kwa nini tusikusanye kodi kupitia uvuvi wa bahari kuu ambako kuna kodi nyingi inapotea kwa kuibiwa na meli kibao za uvuvi toka mataifa ya kigeni?

Kodi ya kichwa ni aibu kubwa karne hii.
Sasa weye hicho kichwa chako kina faida gani kwa ujinga huo ulioandika?Unatakiwa ulipishwe mara mbili zaidi!
 
Hivi ni lazima kila raia alipe kodi? Nini maana ya kuwa na vyanzo vya kodi vyenye nguvu?

Kodi ya voucher ni rahisi kukusanya lakini haina udugu. Maana hata bibi asiye na uwezo akiweka vocha anatozwa kodi.
Kila raia ni lazima alipe kodi. Kiprinciple inabidi iwe hivyo. Haujaja duniani ili uishi kwa jasho la wengine. Sasa linapokuja kiutekelezaji wote tunaelewa siyo kila mtu anaweza kulipa kodi: kwa mfano kodi kwa watoto itabebwa na wazazi wao, kodi kwa wazee na wasiojiweza inaweza kuwa compensated kutoka vyanzo vingine vya mapato.

Lakini serikali haikufuta kodi ya kichwa ili huo mzigo uwaelemee watu wachache sana -- wafanyabiashara na wafanyakazi tena sekta rasmi. Kufikiri nje ya box katika kuhakikisha kila mtu (anayestahili kulipa kodi) amelipa kodi inatakiwa sana, na kama kuja na kodi za voucher za simu ni moja ya fikra hizo basi nakubaliana nalo.
 
Itakuwa vizuri mishahara yao hao wabunge nayo ikatwe kodi, wachangie BIMA ya afya, pia wachangie kiinua mgongo maana wanahubiri uzalendo lakini hakuna wanachochangia kutoka kwenye mishahara yao japo wanalipwa mamilioni, na bado nyumba bure, bima bure, kiinua mgongo wanapewa bure japo hawachangii, na mafta ya gari bure, yani kila kitu bure

Mapato ya ubunge kwa ujumla pamoja na marupurupu ni kiasi cha shilingi milioni 12 kwa mwezi kwa mbunge. Hiki ni chanzo kingine cha kuongezea makusanyo ya uzalendo kuchangia kodi.
"Mshahara wa mbunge ni milioni 3.8 kwa mwezi, Posho ya Ubunge ni milioni 8 kwa mwezi, Posho ya
 
Direct taxes anazolipa mtumiaji wa Simu Tanzania:
1. VAT
2. Excise Duty
3. Kodi ya hilo chotora la Ilala
 
Kwanza ieleweke wazi kuwa kodi ya itayolipwa na wananchi kupitia manunuzi ya vocha za simu ni sawa na kodi ya kichwa waliokuwa wanatoza wakoloni kisha tukairithi na baadae kuondolewa miaka tisini baada ya kuwa ni kodi inayodhalilisha watu.

Kwamba ukiongeza salio unakatwa pesa ili kuchangia maendeleo hii ni aibu. Yaani hata wanachi wasiojiweza ambao wakiongeza salio la buku watachachangia kodi? Kisa tu tuna miradi mikakati kama Sgr na hatuna pesa

Kama tunahitaji pesa za kukamilisha miradi mkakati kwa nini tusikusanye kodi kupitia uvuvi wa bahari kuu ambako kuna kodi nyingi inapotea kwa kuibiwa na meli kibao za uvuvi toka mataifa ya kigeni?

Kodi ya kichwa ni aibu kubwa karne hii.
Kwani ni kipi bora kodi ya kichwa ama kodi ya kupora..
 
15 Juni 2021

Prof. Lipumba nchi haina uwezo wa kukusanya fedha za ndani kutosha kugharamia bajeti ya MAENDELEO YA 2021 / 2022



Prof. Lipumba ampa ushauri mzito Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kuwa bajeti ya 2021 / 2022 hakuna uhalisia wa kuweza kukusanya kodi kugharamia miradi mikubwa iliyopo.

Sovereign credit rating ya Tanzania inazidi kuporomoka, riba ya kulipia mikopo ya kibiashara kupanda kutokana na kushindwa kulipa madeni kwa wakati, ukuaji wa Money supply / ujazo wa fedha umepungua katika ya mwaka 2016 - 2020, mikopo kwenye sekta binafsi imepungua sana huku riba imeongezeka marudufu na kupelekea biashara kuyumba na maana yake makusanyo ya kodi kupungua.

Mtu binafsi mwananchi kufungua akaunti ya akiba benki analipwa riba ndogo ya 2.3%, mtu binafsi akienda kukopa benki kama atapata bahati ya kukubaliwa atatozwa riba asilimia 20% .....

Hali siyo nzuri.. kodi za majengo haziwezi kuwa za serikali kuu kama waziri Dr. Mwigulu Nchemba alivyotangaza ktk bajeti ya 2021 / 2022 ilitakiwa zikusanywe na Halmashauri za wilaya ili zitumike huko wilayani.

Prof. Lipumba anatizama lengo la serikali kuongeza Tozo za miamala kuwa karata ya turufu ya kuongeza mapato makubwa ya serikali, ni sawa na serikali kuzuia ukuaji wa kiuchumi wa kidijitali hivyo serikali imepotoka.

Source : ICON TV TZ
 
11 March 2021

Mh. Philip Mpango : Bajeti ya 2021 / 2022 inaweka wazi Misingi Jumla na kufafanuliwa , kupanua wigo wa walipa kodi, serikali yataka kuelewa kwanini wafanyabishara wadogo hawataki kulipa Kodi, sababu za Masharti magumu ya mikopo kwa serikali, kulipa deni la serikali, gharama za uendeshaji serikali, uchaguzi mkuu 2020 ulioendeshwa kwa mara ya kwanza kwa kutumia fedha za ndani, kuleta nidhamu ktk matumizi ya serikali ....


 
20 Juni 2021
Dar es Salaam, Tanzania

Ukosefu wa Fedha na Ubadhirifu Manispaa ya Kinondoni wakwamisha miradi 3 mikubwa Dar es Salaam


Miradi mitatu Kinondoni ya Makao Makuu ya Manispaa Kinondoni, Uwanja wa Michezo Mwenge, Kituo cha Mabasi Mwenge
Source: ITV Tanzania
 
Hivi ni lazima kila raia alipe kodi? Nini maana ya kuwa na vyanzo vya kodi vyenye nguvu?

Kodi ya voucher ni rahisi kukusanya lakini haina udugu. Maana hata bibi asiye na uwezo akiweka vocha anatozwa kodi.
Atatozwa kodi lakini atapata huduma nzuri za kijamii alafu mtu asiye na uwezo hata matumizi yake ya voucher yanakuwa ya nadira hivyo haitamuumiza huku na yeye anafanikisha kupata huduma nzuri, kama kusogezewa maji, umeme, barabara, shule kwa watoto na wajukuu na hospital karibu, inatakiwa huyo Bibi au babu asiwe mbinafsi kuacha kuandaa kizazi atakachokiacha kuishi kwenye jamii yenye mahitaji muhimu.
 
Tuna bahari, tuna maziwa makuu, tuna bandari zinazohudumia hata Nchi jirani, tuna mbuga za wanyama, tuna madini mengi yakiwemo Tanzanite na Uranium,tuna vivutio vingi vya watalii, tuna samaki wengi, tuna ardhi kubwa na misitu mingi.

Rasilimali hizo zote tumeshindwa kuzisimamia ili kupata fedha za kuendeshea miradi mpaka tunakimbilia kwenye njia hii?

Watanzania wenzangu, nani alituroga sisi?
Hivyo vitatumika kuongeza ufanisi kwenye vile tutavyojenga kama kuongeza umeme, madaraja, shule nzuri, hospital nzuri, stendi nzuri na vitu vingine vizuri.
 
22 Jun 2021

Bunge lapitisha Bajeti ya Serikali 2021/2022 kwa 'kishindo'


Bunge limepitisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/22 ambapo wabunge 361 sawa na asilimia 94 wamekubali huku wabunge 23 sawa na asilimia 6 hawakuamua

Source : mwananchi digital
 
22 Juni 2021
Dodoma, Tanzania

Bunge lapitisha Bajeti kuu ya Serikali ya mwaka 2021 / 2022 Shs.36,681,897,765,000​


Bunge limepitisha Bajeti Kuu ya Serikali ya shilingi trilioni 36.68 kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ambapo Wabunge 361 sawa na asilimia 94 wamepiga kura ya ndio.

Akitangaza matokeo ya upigaji wa kura mara baada ya mjadala wa Bajeti ya Serikali uliofanyika kwa takribani wiki moja Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai amesema kuwa Wabunge waliopiga kura ni 385 ambapo waliopiga kura ya Ndio ni 361 sawa na asilimia 94, waliopiga kura isiyo ya maamuzi (hawajakataa wala kukubali) ni 23 sawa na asilimia 6 na Wabunge watano (5) hawakuwepo wakati wa zoezi hilo la upigaji kura.

Aidha, mara baada ya upigaji huo wa kura Bunge lilipitisha Muswada wa Sheria ya kuidhinisha Matumizi ya Serikali wa mwaka 2021 (The Appropriation Bill, 2021) wenye dhumuni la kuidhinisha Matumizi ya jumla ya Shilingi 36,681,897,765,000.

Mara baada ya kupitisha Bajeti zote za Wizara pamoja na Bajeti kuu ya Serikali, Mkutano wa Tatu wa Bunge unatarajia kuendelea na ukamilishaji wa shughuli zilizobaki za Kiserikali na Kamati kabla ya kuahirishwa Juni 30 2021 . Source : Parliament of Tanzania
 
Fikiria kodi ya majengo ilivyo kuwa,unaacha shughuli zako unaenda benk saa mbili na nusu asubuhi unapata huduma ya kulipa sh.10000 saa nane mchana,umesimama karibu masaa saba, hivi kweli wangapi watakuwa tayari kupata mateso kama hayo bado wanatoa pesa zao kwa mateso ya kiwango hicho, no bora hivi karibuni kuna wakala Ila bado ilikuwa shifts.
Mkuu Vessel kulalamika ni sifa ambayo sisi watanzania tuna haki ya kuiandika ndani ya CV zetu tukiwa tunaomba kazi, yaani ni sifa ya asili tuliyonayo.

Hizo foleni za kulipa shilingi elfu kumi zimeikosesha serikali pesa nyingi kwani wengi hawapendi hiyo kero ya kusimama siku nzima nje ya dirisha halafu shughuli nyinginezo ziwe zinakwama.
 
Back
Top Bottom