Kurudisha kodi ya kichwa nyakati hizi za ulimwengu ulioendelea ni aibu kubwa. Mwigulu Nchemba kuwa na aibu. Mbona kuna vyanzo mbadala vingi

Hivi ni lazima kila raia alipe kodi? Nini maana ya kuwa na vyanzo vya kodi vyenye nguvu?

Kodi ya voucher ni rahisi kukusanya lakini haina udugu. Maana hata bibi asiye na uwezo akiweka vocha anatozwa kodi.

Lazima kila raia alipe kodi ndiyo uzalendo wa kweli ila watoto, vikongwe au walio na ulemavu wa kushindwa kufanya shughuli wao hawawajibiki kulipa kodi.

Mfano Tanzania daftari la wapiga kura mamilioni wenye kazi sekta kama waajiri serikalini, sekta binafsi na waliojiajiri wauza mitumba, wakulima, wavuvi , wafugaji , madalali, mishemishe za mjini n.k ambao wote hawa wanaendesha maisha yao kwa kazi zao lazima walipe kodi inayofanana na ya PAYE. Jumla yao ni 29,000,000 Idadi ya wapiga kura Tanzania waongezeka

Nadhani hakuna namna nyingine hata hawa kina babu na bibi wanatakiwa kuwa wazalendo hawaoni mabarabara, ma-flyover, stendi za mabasi wilaya zote, hospitali za wilaya / rufani, shule zikichipuka kama uyoga kila kona ya nchi lazima kuna ulazima kuvichangia tunaambiwa hatuna mjomba ktk nchi za Mabeberu alete misaada wakati rasilimali watu mamilioni waTanzania wanaoendesha maisha yao kila siku wapo, na bila kusahsu maliasili, utalii, makampuni n.k vipo nchini Tanzania.

Tupewe elimu ya kweli walipa kodi ya "kichwa" tunaofikia watu 29,000,000

 
Tuna bahari, tuna maziwa makuu, tuna bandari zinazohudumia hata Nchi jirani, tuna mbuga za wanyama, tuna madini mengi yakiwemo Tanzanite na Uranium,tuna vivutio vingi vya watalii, tuna samaki wengi, tuna ardhi kubwa na misitu mingi.

Rasilimali hizo zote tumeshindwa kuzisimamia ili kupata fedha za kuendeshea miradi mpaka tunakimbilia kwenye njia hii?

Watanzania wenzangu, nani alituroga sisi?
 
October 8 2014
Historia : Wananchi wengi walikuwa wakikwepa kulipa kodi ya kichwa.


Serikali za mitaa ni chombo cha utawala wa umma, kilichopewa madaraka ya kuamua na kuendesha shughuli zake katika sehemu ndogo ya nchi au Taifa. Ifuatayo ni sehemu ya pili ya makala inayoelezea historia ya Serikali za mitaa Tanzania.

Baada ya uhuru, Serikali za baadhi ya nchi za Afrika kama vile Zaire (Congo Kinshasa), Uganda, Senegal na nyingine nyingi ama zilifuta mfumo wa serikali za mitaa au kubadilisha mfumo wake ulioanzishwa na Serikali za Kikoloni.
Kwa mfano, Serikali ya Tanganyika ya wakati huo haikufuta mfumo huo mara moja. Badala yake ilizirithi serikali za mitaa na kuzitumia kama nyenzo za kuleta maendeleo kwa misingi ya kidemokrasia.

Katika kipindi cha miaka ya mwanzo ya uhuru, yalikuwapo makundi matatu ya serikali za mitaa.

Miongoni mwao ni zile zilizoundwa chini ya Sheria Namba 72 ya mwaka 1926 zilizokuwa 47.

Aidha, chini ya Sheria Namba 333 ya mwaka 1953, zilikuwa 9 kwa mijini na 10 kwa vijijini.

Kundi la tatu lilikuwa ni la Manispaa ya Dar es Salaam, iliyoundwa na Sheria Na. 105 ya mwaka 1946.

Mwaka 1962 Sheria na 333 ilirekebishwa kwa kuondoa mamlaka za wenyeji na mwaka 1963 Sheria Namba 13/62 ilipitishwa kusitisha utawala wa machifu nchini.

Inaelekea kuwa uamuzi wa kufuta utawala wa machifu nchini ulitokana na sababu kuu tatu. Serikali ya wananchi ilitaka kujenga mfumo wa kidemokrasia wa Serikali za mitaa. Aidha, ilionekana utawala wa machifu uliendeleza fikra za ukabila badala ya utaifa. Pia ikumbukwe kwamba wengi wa machifu waliwekwa madarakani na serikali ya kikoloni.

Kwa mantiki hiyo, machifu walikuwa kama mawakala wa serikali ya kikoloni. Mfumo huu usingeweza kukubalika katika Serikali iliyochaguliwa na wananchi.

Serikali ya wananchi ilikuwa na sera yake madhubuti juu ya serikali za mitaa. Ilibidi ichukue hatua kadhaa katika kutekeleza sera hiyo.

Na hatua zilizochukuliwa ni:-

Kuanzishwa kwa uchaguzi wa madiwani katika halmashauri zote zilizokuwa zimeandikishwa na serikali ya kikoloni, Kuundwa kwa Halmashauri katika wilaya au miji ambayo zilikuwa hazijaundwa.

Mafanikio ya Serikali za mitaa 1961- 1972
Katika kipindi kati ya mwaka 1962 na 1972 Serikali za mitaa zilipata mafanikio machache na matatizo kuwa mengi.


Majukumu ya halmashauri yaliongezeka kama vile usimamizi wa elimu ya msingi, matibabu, barabara na maji.

Ingawa halmashauri za wilaya zilikuwa na majukumu mazito zaidi kuliko yale ya halmashauri za miji, inashangaza kuona kuwa sehemu kubwa ya ruzuku kutoka Serikali Kuu kwenda kwa Serikali za mitaa ilitolewa kwa halmashauri za miji.

Licha ya hali hiyo ya upendeleo kwa halmashauri za miji, kwa jumla halmashauri za wilaya ziliweza kutekeleza majukumu yake vizuri kwa kujikusanyia mapato kutokana na kodi na ushuru wa mazao na wakati huo huo kuhudumia miradi mbalimbali ya huduma za jamii.

Katika kipindi hiki mapato ya halmashauri yalishuka sana. Kushuka kwa uwezo wa halmashauri za wilaya kukusanya mapato ni ishara ya kukumbwa na matatizo katika utekelezaji wa majukumu yake.

Hivyo, halmashauri zikashindwa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Hali hiyo ndiyo iliyojitokeza kwa serikali nyingi za mitaa katika kipindi hiki cha mwaka 1962-1972.

Matatizo yaliyozikabili serikali za mitaa yalitokana na sababu zifuatazo:
Kama ilivyoelezwa hapo awali kwamba, serikali za mitaa zilipewa majukumu mara baada ya uhuru na kwamba Serikali Kuu ilikuwa na nia ya kuleta maendeleo ya haraka kwa watu wake. Lakini vyanzo vya mapato kwa Serikali za mitaa vilikuwa vichache.

Halmashauri za wilaya, kwa mfano, ziliruhusiwa kukusanya mapato kutokana na kodi na ushuru wa mazao.

Ukusanyaji wa kodi kutoka kwa wananchi ulikuwa mgumu. Wananchi wengi walikuwa wakikwepa kulipa kodi ya kichwa.

Ilikuwa kama kero kwao na kusababisha matukio ya aibu na hata maafa. Kutokana na matukio hayo, Serikali Kuu iliamua kufuta kodi ya kichwa.

Aidha, ilipofika Mei, 1969 ushuru wa mazao nao ulifutwa. Uamuzi huo katika masuala mawili uliathiri kwa kiasi kikubwa mapato ya serikali za mitaa nchini.

Licha ya kwamba Serikali za mitaa zilitegemea zaidi misaada na ruzuku kutoka Serikali Kuu baada ya vyanzo kadhaa vya mapato yake kufutwa, pia katika kipindi hicho hicho Serikali Kuu ilipunguza ruzuku kwa serikali za mitaa.

Uamuzi huu ulitokana na sababu kwamba Serikali Kuu ilichukua baadhi ya majukumu ambayo hapo awali yalikuwa ya serikali za mitaa. Mifano ya majukumu hayo ni ulipaji wa mishahara ya walimu wa shule za msingi wa Daraja “A” na “B” na ununuzi wa vifaa vya kufundishia na kusomea.

Wizara nyingine, kama Afya, Ujenzi na Madini nazo pia zilichukua baadhi ya majukumu ya Serikali za Mitaa. Kutokana na upungufu wa mapato, halmashauri nyingi zilishindwa kutekeleza majumumu yao kwa ufanisi, hali ambayo ililaumiwa sana na Serikali Kuu

Source : kwa hisani kubwa ya : Ijue historia ya Serikali za mitaa Tanzania-2 | Mwananchi

Source : Historia ya Serikali za Mitaa na mkakati wa kupeleka madaraka kwa wananchi | Mwananchi
c.c Idugunde
 
October 20, 2016
 
Julai 12 2018
Songea, Tanzania

Mchango wa elimu Songea wafananishwa na kodi ya kichwa​

Manispaa hiyo Songea ilibandika tangazo kueleza nia ya kutunga sheria ndogo kuanzisha Bodi ya Mfuko wa Elimu ambao kila mwananchi atachangia Sh10,000 kwa mwaka.

Songea. Wananchi wamepinga mchango wa Sh10,000 kwa ajili ya mfuko wa elimu wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, wakiufananisha na kodi ya kichwa iliyofutwa miaka mingi na Serikali.

Juzi, manispaa hiyo ilibandika tangazo kueleza nia ya kutunga sheria ndogo kuanzisha Bodi ya Mfuko wa Elimu ambao kila mwananchi atachangia Sh10,000 kwa mwaka.

Vyanzo vinavyokusudiwa katika tangazo kwa wananchi lililosainiwa na mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya Songea, Tina Sekambo, halmashauri imetangaza nia ya kutunga sheria ndogo sita za ada na ushuru; ushuru wa masoko na kodi ya vibanda vya biashara; ushuru wa maegesho ya magari; ushuru wa madini ya ujenzi; kilimo cha kahawa na uanzishwaji wa Bodi ya Mfuko wa Elimu.
Halmashauri imesema mtu yeyote mwenye maoni au pingamizi anatakiwa kuwasilisha kwa maandishi kwa mkurugenzi wa manispaa ndani ya siku 14 tangu siku ya tangazo hilo, ambayo ni juzi.

Baadhi ya wananchi walijikusanya kwenye vikundi jana kusoma tangazo hilo lililobandikwa maeneo kadhaa wakilalamikia mchango kwa ajili ya elimu.

Akizungumza na Mwananchi, mkazi wa Majengo, Aidan Rwena baada ya kusoma tangazo lililobandikwa eneo la Soko Kuu alisema ushuru wa elimu iwapo utapitishwa utawafanya waishi kwa shaka kwa kuwa wengi wao hawana uwezo wa kulipa fedha hizo.

Napinga ushuru huu, una lengo la kutukomesha wananchi. Tuna michango mingi na hali zetu ni ngumu ukisema kila mtu alipe Sh10,000 ni kuturudisha kwenye kodi ya kichwa, huu ni uonevu kwa wananchi wanyonge,” alisema.

Violeth Rungu, mkazi wa Namanyigu katika Manispaa ya Songea aliyesoma tangazo lililopo eneo la manispaa alisema limemsikitisha kwa kuwa kuna kodi nyingi za kulipa.

“Kuna kodi kibao, za majengo, ardhi, biashara bado tulipie na hii inayofanana na kodi ya kichwa, hapana! Watuonee huruma. Sina uhakika wa kupata fedha, familia ni kubwa Sh10,000 kwa watu kumi ni fedha nyingi,” alisema Violeth.

Diwani wa Ruhuwiko, Wilbroad Mahundi alisema hayatambui mapendekezo hayo kwa kuwa hakuna kikao kilichoyapendekeza.
“Siungi mkono kodi hiyo, kama mkurugenzi anadai ni kwa ajili ya mfuko wa kuchangia elimu tayari Serikali inatoa elimu bure. Waache kuwaumiza wananchi kwa kuwa hizo kodi ambazo ni kero tulishazikataza,” alisema.

Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Ruvuma, Tito Mbilinyi maarufu Mwilamba alisema wanashangazwa na manispaa kuwarundikia kodi ambazo waliiomba Serikali Kuu kuwapunguzia zile ambazo zimekuwa kero.

Alipotafutwa na Mwananchi, mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya Songea, Tina Sekambo alisema elimu ni gharama hivyo iwapo wananchi wataridhia Sh10,000 zitaingizwa kwenye mfuko wa elimu.

Tina alisema hayo ni mapendekezo ya sheria ndogo za halmashauri na iwapo wananchi watayakataa hawatatozwa.

“Naomba muwaelimishe wananchi wawe na amani, nawasiliana na mwanasheria ili kuondoa tangazo kwa kuwa naona limezua malalamiko mengi na linatukosesha amani,” alisema Tina.

Source: Mchango wa elimu Songea wafananishwa na kodi ya kichwa | Mwananchi
 
Ingawa ni kweli bado kuna maeneo mengi ambayo hayajaguswa ili kuwa sehemu ya mapato ya serikali,

Lakini kwenye kodi ya Laini, naunga mkono, watu walipie line zao, Kama mtu ataona mzigo abaki na laini moja, maana hizi laini zimekuwa ni kama sehemu za weengi sana kujipatia kipato kwa njia ya udanganyifu, ingawa pia hilo TCRA inaweza kuwa sehemu ya kulaumiwa

Nchii hii ina shida sana. Kama kuna watu wengi wako kama wewe - itatuchukua vizazi vingi sana kutoka hapa! Kwa hiyo unadhani shilingi 100 kwa laini 1 nyingine ni gharama kubwa sana kiasi mhalifu wa mamilioni ataacha kufanya uhalifu?? Ama kweli elimu ya nchi hii ina kiwango cha kusikitisha kama na wewe utasema umeelimika!
 

More than 4.4 Million Kenyans file returns despite the prevalent Covid-19 pandemic​

PRESS RELEASE 03/07/2020

Despite the prevailing Covid-19, pandemic, more than 4.4 Million Kenyans filed their 2019 tax returns as the filing period officially closed at midnight on Tuesday 30thJune 2020.

This year, more than eight hundred thousand taxpayers filed their 2019 tax returns compared to last year, where 3.6 million Kenyans filed their returns by 30th June. This is equivalent to a 25% increment equated to the same time last year.

The growth in the numbers show positive progress in tax compliance, a move that is anticipated to drive the country towards economic recovery.

Similar to last year, Kenya Revenue Authority (KRA) Service Centers did not experience long ques during the last days of filing, an improvement that is attributed to efficiency of the iTax platform.
KRA has progressively enhanced the iTax system for a better user experience.

For instance, iTax has been enhanced to include an auto-populated return for taxpayers with employment income as the only source of income. Taxpayers in this category, whose annual tax returns constitute the bulk of all annual tax returns, are only required to fill in annual pension and tax relief details in the respective fields provided to complete the return process.

KRA acknowledges and appreciates all taxpayers who turned up to file their annual tax returns. Taxpayers are also reminded that penalty for late filing of annual returns for Income Tax Individual is Ksh.2000 or 5% of tax due whichever is higher, while Income Tax for Non-Individual is Ksh.20,000 or 5% of tax due whichever is higher.

Kenyans are urged to file returns early, beginning January of every calendar year, to avoid last minute rush that comes around the 30th June deadline. Just like tax payment, filing of tax returns is an important tax compliance tenet, which is put into account in the measure of a taxpayer’s compliance.

Source : More than 4.4 Million Kenyans file returns despite the prevalent Covid-19 pandemic - KRA

c.c idugunde
 

Magufuli - Tanzania ina walipa kodi milioni 2.2 tu na ndiyo sababu ya Tanzania kutokuwa na mapato makubwa ya kodi​

Daniel Samson   Disemba 10, 2018 Biashara
  • Rais John Magufuli amesema hali hiyo inatokana na mapungufu yanayojitokeza katika mifumo na taratibu za ukusanyaji kodi ikiwemo wigo mdogo wa kulipa kodi usioendana na idadi ya watanzania.
  • Amesema vyanzo vya ukusanyaji kodi havitumiwi vizuri jambo linalotoa mwanya kwa wafanyabiashara kukwepa kodi wakishirikiana na baadhi ya wafanyakazi wa TRA.
  • Ameagiza kuchukuliwa hatua mbalimbali ikiwemo kutengeneza mazingira ya ulipaji kodi, kupitia upya viwango vya kodi na taasisi za biashara na uwekezaji ikiwemo TPA na TIC kuondoa urasimu katika shughuli zao.

Dar es Salaam. Rais John Magufuli amesema Tanzania haifanyi vizuri katika ukusanyaji wa mapato ikilinganishwa na nchi jirani kutokana na mapungufu yanayojitokeza katika mifumo na taratibu za ukusanyaji kodi ikiwemo wigo mdogo wa kulipa kodi usioendana na idadi ya Watanzania.

Rais Magufuli amesema licha ya takwimu kuonyesha kuwa uchumi unakua kwa kasi na mfumuko wa bei kushuka mpaka asilimia tatu, bado ukusanyaji wa mapato hauridhishi na jitihada zaidi zinahitajika kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi kulipa kodi ili kukamilisha miradi ya maendeleo kwa wakati.

Wizara ya Fedha na Mipango inaeleza kuwa makusanyo ya mapato yameongezeka hadi kufikia wastani wa Sh1.3 trilioni kwa mwezi tangu mwaka 2016 ukilinganisha na Sh850 bilioni iliyokuwa inakusanywa kabla ya ujio wa Serikali ya awamu ya tano.

Dk Magufuli, aliyekuwa akizungumza katika kikao kazi cha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na wakuu na makatibu wa mikoa kinachofanyika Jijini Dar es Salaam leo (Desemba 10, 2018), amesema Tanzania yenye idadi kubwa ya watu kuliko nchi nyingine za Afrika Mashariki, ina dadi ya walipa kodi wapatao 2.27 milioni ambapo uwiano wa kodi ukilinganisha na Pato la Taifa (GDP) ni asilimia 12.8.

“Tax-base (wigo) yetu ya makusanyo ni ndogo mno, ikiwa nchi jirani ya Msumbiji wako milioni 27, walipa kodi ni milioni 5.3. Sisi Tanzania tuko milioni 55, walipa kodi ni milioni 2.2 lazima tufike mahali tujiulize, kwa hiyo utaona kwamba kuna mahali tumeshindwa,” amehoji Magufuli.
9f17ea1efc0565cee91d3983e0f541d6cf9eb65b.jpg

Rais John Magufuli akihutubia wakati wa kikao kazi cha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na wakuu na makatibu wa mikoa kinachofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. Picha| Michuzi.

Sababu za Tanzania kuwa na uwiano mdogo wa walipa kodi
Rais Magufuli ameweka wazi kuwa hali hiyo inatokana na Tanzania kutotumia vizuri fursa ya vyanzo vya mapato vilivyopo katika kukusanya kodi ikiwemo sekta ya uvuvi katika bahari kuu, madini na uchimbaji wa gesi asilia.

Sababu nyingine ni kushindwa Tanzania kama nchi kurasimisha sekta isiyo rasmi hasa wafanyabiashara wadogo na kuifungamanisha na sekta rasmi ili kuwatambua na kuwafikia walipa kodi katika maeneo waliyopo nchini.

Sekta isiyo rasmi Tanzania , kwa mujibu wa Rais Magufuli, inakaribia kufikia asilimia 60 hadi 70 ambapo Serikali inakusanya mapato kutoka sekta rasmi yanayofikia kati ya asilimia 30 hadi 40, ikiwa na maana kuwa kodi nyingi za nyumba, maghala, hoteli zinapotea.

Kuhusu ufanisi wa ukusanyaji wa mapato, Rais amesema ni mdogo licha ya takwimu kuonyesha makusanyo ya kodi yanaongezeka kila mwaka jambo linaloirudisha nchi nyuma ikilinganishwa na Kenya ambayo inafanya vizuri katika kukusanya kodi zake.

Nitoe mfano, mwaka 2013/14 wenzetu wa Kenya walipanga kukusanya Dola za Marekani bilioni 9.74 lakini walikusanya Dola za Marekani bilioni 9.64. Sisi katika mwaka huo tulipanga kukusanya Dola za Marekani bilioni 4.8 na tutakusanya Dola za Marekani bilioni 4.4,” amesema Rais.

Dk Magufuli hakuacha pia kuzungumzia kodi kubwa wanayotozwa wananchi hasa kodi ya majengo ambayo imesababisha wananchi wengi kukwepa kodi na kuikosesha Serikali mapato na hili linajidhihirisha katika idadi ndogo ya majengo yanayosajiliwa na kuingizwa katika mfumo wa kodi kila mwaka.

“Mathalani katika kipindi cha miaka miwili iliyopita tumekusanya Sh74.5 bilioni na hapo wameniambia katika miezi sita iliyopita tumekusanya Sh8 bilioni na majengo yaliyosajiliwa mpaka sasa ni majengo milioni 1.6 hiki pia ni kichekesho,” amesema Rais akionyesha kushangazwa na idadi ndogo ya majengo yaliyosajiliwa ukilinganisha na idadi ya watanzania wanaofikia milioni 55.


Dk Magufuli ametuhumu ukwepaji wa kodi unaofanywa na wafanyabiashara wanaoshirikiana na baadhi ya wafanyakazi wa TRA wasio waaminifu ambao hutumia mwanya wa mawasiliano hafifu na mifumo ya makusanyo ya kodi ambayo haijaimarishwa kujipatia fedha zinazotakiwa kuingia katika mfumo rasmi wa Serikali.

Kutokana na hali hiyo, Rais Magufuli ameagiza kuchukuliwa hatua mbalimbali ikiwemo kutengeneza mazingira ya ulipaji kodi, kupitia upya viwango vya kodi, taasisi za biashara na uwekezaji ikiwemo Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kuondoa urasimu katika shughuli zao ili kuharakisha uwekezaji nchini.

Kamishna Mkuu wa TRA, Charles Kichere amesema mamlaka hiyo imefanikiwa kuunganisha mifumo ya kodi ya forodha na kodi za ndani ili kudhibiti upotevu wa mapato na kuongeza ufanisi wa ukusanyaji mapato.

Amesema wataendelea kusisitiza nidhamu na maadili kwa wafanyakazi wa TRA ili kuziba mianya yote ya rushwa na kuhakikisha ukusanyaji wa kodi unaongezeka kufikia malengo yanayowekwa na Serikali kila mwaka.

“Tunaendelea kukusanya kodi ya majengo ambapo mpaka sasa tumekusanya kiasi cha Sh8.8 bilioni wakati lengo likiwa shilingi bilioni 21 tuna uhakika tutafikia lengo la kukusanya kodi hii,” amesema Kichere.

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema kama wizara watahakikisha wanasimamia matumizi sahihi ya mashine ya EFD, kutanua wigo wa ulipaji kodi kwa wananchi, kudhibiti misamaha ya kodi isiyo na tija na kurahisisha taratibu za kulipa kodi, ada na tozo mbalimbali.

Source : Nukta | Sababu za Tanzania kutokuwa na mapato makubwa ya kodi

c.c idugunde
 
11 June 2021

MWAKA WA FEDHA 2021 / 2022 : BAJETI YA KENYA 78 trilioni WAKATI YA TANZANIA 34 trilioni


 
Wachuuzi
Kuna kada fulani fulani wakiwamo sungu sungu, wapiga debe, boda boda, mama lishe na wa namna hiyo wanataka wengine tu walipe kodi na ikibidi wafilisiwe kabisa!

Wakiwekewa kodi ya hata shs 1 kwa mwaka panachimbika balaa.

Hawa ndiyo wale wanyonge wenye serikali yao iliyokwenda zake.
 
Kuna kada fulani fulani wakiwamo sungu sungu, wapiga debe, boda boda, mama lishe na wa namna hiyo wanataka wengine tu walipe kodi na ikibidi wafilisiwe kabisa!

Wakiwekewa kodi ya hata shs 1 kwa mwaka panachimbika balaa.

Hawa ndiyo wale wanyonge wenye serikali yao iliyokwenda zake.

Brazaj,

Yaani hapo ndipo sera ya kodi ya serikali ya CCM ilipojikwaa.

Maana kundi hili la waTanzania wenye maisha ya kujitegemea kama wengine lakini hawalipi kodi stahili na hawa ndiyo asilimia 70 ya waTanzania wanajiendeshea maisha mijini na vijijini ya kawaida wanauwezo wao kabisa kifedha lakini serikali inaogopa kuwaelimisha walipe kodi.

Hata Mzee Mwinyi alipokuwa Masasi alisema waTanzania wa kawaida maisha yao kwa sasa ni mazuri zaidi hata anaona kila mtu amevaa kiatu. Wakati enzi zao kiatu cha aina chochote ilikuwa mtihani mkubwa.
29 Jul 2020
Stori ya Mzee Mwinyi kuhusu Viatu vyake yawafanya waombolezaji kuangua kicheko. Tazama zaidi hapa.
 
Mfumo mbovu wa elimu ya kukaririshana umezalisha viongozi ambao sio wabunifu.
 
Kuna eneo kodi haikusanywi ni kwenye mishahara na miposho ya waheshimiwa sana wabunge ni vizuri nao wakawa wazalendo wakachangia Maendeleo siyo kututungia sheria sisi wanyonge ambazo wao waheshimiwa haziwahusu as if wanaoshi korea kaskazini.
 
Kwanza ieleweke wazi kuwa kodi ya itayolipwa na wananchi kupitia manunuzi ya vocha za simu ni sawa na kodi ya kichwa waliokuwa wanatoza wakoloni kisha tukairithi na baadae kuondolewa miaka tisini baada ya kuwa ni kodi inayodhalilisha watu.

Kwamba ukiongeza salio unakatwa pesa ili kuchangia maendeleo hii ni aibu. Yaani hata wanachi wasiojiweza ambao wakiongeza salio la buku watachachangia kodi? Kisa tu tuna miradi mikakati kama Sgr na hatuna pesa!

Kama tunahitaji pesa za kukamilisha miradi mkakati kwa nini tusikusanye kodi kupitia uvuvi wa bahari kuu ambako kuna kodi nyingi inapotea kwa kuibiwa na meli kibao za uvuvi toka mataifa ya kigeni?

Kodi ya kichwa ni aibu kubwa karne hii.
Legacu ya mwendazake hiyo. Hao ndiyo vijana wake
 
Nchii hii ina shida sana. Kama kuna watu wengi wako kama wewe - itatuchukua vizazi vingi sana kutoka hapa! Kwa hiyo unadhani shilingi 100 kwa laini 1 nyingine ni gharama kubwa sana kiasi mhalifu wa mamilioni ataacha kufanya uhalifu?? Ama kweli elimu ya nchi hii ina kiwango cha kusikitisha kama na wewe utasema umeelimika!
Kwa tarifa yako, wasomi hawako kama unavyojisemea, Wasomi na walioelimika, hupinga hoja kwa hoja

Lakini wewe ulichofanya hapa kwenye mchango wako ni kumponda mtu na sio kuboresha hoja ama kuipinga kwa hoja!!

Ndiyo nyinyi maprof wetu, ndiyo maana Msukuma anawananga
 
Hivi ni lazima kila raia alipe kodi? Nini maana ya kuwa na vyanzo vya kodi vyenye nguvu?

Kodi ya voucher ni rahisi kukusanya lakini haina udugu. Maana hata bibi asiye na uwezo akiweka vocha anatozwa kodi.
Lipa kodi wewe kwa maendeleo ya Taifa lako. Acha kulia lia hapa. Kwani hao wabibi wasio na uwezo wamekutuma kuwasemea?

Hizi tozo zinapitishwa na Serikali ya ccm! Na wewe ni Mataga mtiifu wa hicho chama. Hivyo hutakiwi kupingana na msimamo Serikali ya chama chako. Huo ni usaliti. Hata kama ni upuuzi, wewe sifia tu.

Mitano mingine kwa Mama!
 
Nikiweka 1000 inachukuliwa tsh. 152 VAT. Sifahamu hii kodi mpya ya Mwigulu Nchemba ni nini hasa! Eti anasema anatuhurumia; aache kuhurumia familia yake atuhurumie sisi!. Mwanasiasa hubadilika kulingana na wakati na mtawala aliyepo.
152 VAT, 50 KYU.....yaani hiyo fifty ndo kodi ya uzalendo iliyopendekezwa na zungu ikashadadiwa na mwigulu...tunaenda kuendesha nchi kiupatu upatu wakati tumekalia rasilimali za kutosha....
 
Lipa kodi wewe kwa maendeleo ya Taifa lako. Acha kulia lia hapa. Kwani hao wabibi wasio na uwezo wamekutuma kuwasemea?

Hizi tozo zinapitishwa na Serikali ya ccm! Na wewe ni Mataga mtiifu wa hicho chama. Hivyo hutakiwi kupingana na msimamo Serikali ya chama chako. Huo ni usaliti. Hata kama ni upuuzi, wewe sifia tu.

Mitano mingine kwa Mama!
Ahaaa, lack of common sense is a big problem
 
Back
Top Bottom