Kurudisha heshima ya Polisi kwa jamii iundwe tume

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,606
8,744
Mimi ni mtoto wa Polisi na wazazi wangu wote walikuwa kwenye jeshi hili kwa miaka mingi sana. Kwa ufupi wazazi wangu hawajawahi kufanya kazi nyingine.

Ukweli kumekuwa na malalamiko mengi sana ya unyanyasaji wa Polisi wa hali ya juu. Hii sio kwa wanasiasa pekee tumesikia haya malalamiko kutoka kwa raia wa kawaida . Zamani tulikuwa hatusikii haya malalamiko ya unyanyasaji.

Hivyo kurudisha heshima ya jeshi hili la raia inabidi iundwe tume ili wale walionyanyaswa waweze kusema na kutoa machungu yao na kuondoa chuki kwa jeshi nzima. Hii itasaidia vitu viwili (1) kuhakikisha Polisi wenyewe wanafuata utaratibu na sheria (2) Itawafanya raia wajue kwamba serikali inajali haki za binadamu. Inashangaza sana wakati hayati Magufuli alivyokuwa anasema wananchi wasionewe ndiyo wakati huohuo Polisi wametesa watu kuliko wakati mwingine wowote.

Vilevile hakuna sababu ya Polisi kutumia machine gun kulinda hata kwenye traffic wakati mwingine wakati siku hizi kuna bastola ambazo sio mzigo na zinaweza kuchukuwa risasi za kutoka na bei sio ya juu sana. Polisi wa raia wanatakiwa kuheshimiwa na sio kuogopwa na wananchi wasio na haki.

Serikali ifikirie kuunda tume ya watu kusema machungu yao hasa wale walio teshwa bila sababu
 
Sahau hilo, inaonekana hata kotaz hujui zipo wapi hapo ulipo. Hii ni africa

Wajinga nchini ni zaidi ya asilimia 80.
So kuwaongoza lazima weledi uuweke pembeni kidogo.

Ila si maanishi baadhi ya ujambazi unaofanywa na maaskari wetu wasio waaminifu.
 
... sahihi kabisa; Police Independent Oversight Commission (PIOC). Sijui wajumbe wake watachaguliwa na mamlaka gani ila sio makada aina ya Mutungi.

Tume ilindwe na Katiba ya nchi na kuwe na kitengo maalum ndani ya JWTZ kukamata mapolisi watakaotuhumiwa; vinginevyo watalindana hawa. Mdogo mdogo polisi wanaelekea kuwa genge fulani la wahuni badala ya chombo adhimu cha wananchi.
 
Tiba ni KATIBA mpya sio viraka vya tume,suala hili ni lazima liwe ndani kisheria,na mifano ipo mingi tu angalia polisi wa Namibia,Botswana wapo fair sana na wanaheshimika sio kuogopwa na Botswana wana road blocks zinazokua zinalindwa na jeshi nao wapo very friendly,helpful mradi tu fuata sheria zao,na hakuna woga hata ukipata road breakdown getini kwao !sasa wewe gari yako izimike mbele ya kambi ile ya jeshi letu...utatamani uibebe gari mgongoni.
 
Siku hizi upo Salama ukikamatwa na Boko haram kuliko uwapo mikononi mwa PT hasa hawa aina ya Kingai, Goodluck na Mahita.

Jeshi la Polisi lifumuliwe lote liundwe upya ila kwa kuwa wanalinda maslahi ya wanasiasa hili haliwezi kufanyika.

NAWACHUKIA SANA POLISI YAANI MNOOO SIO KWA ULE UNYAMA WALLAH.
 
Mimi ni mtoto wa Polisi na wazazi wangu wote walikuwa kwenye jeshi hili kwa miaka mingi sana. Kwa ufupi wazazi wangu hawajawahi kufanya kazi nyingine.

Ukweli kumekuwa na malalamiko mengi sana ya unyanyasaji wa Polisi wa hali ya juu. Hii sio kwa wanasiasa pekee tumesikia haya malalamiko kutoka kwa raia wa kawaida . Zamani tulikuwa hatusikii haya malalamiko ya unyanyasaji.

Hivyo kurudisha heshima ya jeshi hili la raia inabidi iundwe tume ili wale walionyanyaswa waweze kusema na kutoa machungu yao na kuondoa chuki kwa jeshi nzima. Hii itasaidia vitu viwili (1) kuhakikisha Polisi wenyewe wanafuata utaratibu na sheria (2) Itawafanya raia wajue kwamba serikali inajali haki za binadamu. Inashangaza sana wakati hayati Magufuli alivyokuwa anasema wananchi wasionewe ndiyo wakati huohuo Polisi wametesa watu kuliko wakati mwingine wowote.

Vilevile hakuna sababu ya Polisi kutumia machine gun kulinda hata kwenye traffic wakati mwingine wakati siku hizi kuna bastola ambazo sio mzigo na zinaweza kuchukuwa risasi za kutoka na bei sio ya juu sana. Polisi wa raia wanatakiwa kuheshimiwa na sio kuogopwa na wananchi wasio na haki.

Serikali ifikirie kuunda tume ya watu kusema machungu yao hasa wale walio teshwa bila sababu



Naona wazo lingine limefanyiwa kazi na tume mpya
 
Back
Top Bottom