Kurudisha Heshima, Mchague Sitta kuwa Waziri Mkuu

popiexo

JF-Expert Member
Oct 26, 2010
742
182
Katika kipindi hiki ambacho tumepoteza imani na Serikali chini wa waziri mkuu Pinda, Ni vyema JK akamteua Samwel Sita awe waziri mkuu. Hii itamsaidia angalau kumaliza muda wake wa urais kwa heshima mbele. Huu ni wakati muafaka kwa JK kufanya maamuzi magumu kuipa heshima nafasi aliyonayo.
 
Kuna watu wanaogopwa na mafisadi, na wanaweka shinikizo wasipate nafasi nyeti. lakini wanamuharibia raisi wetu.

Mfano:
1. Six
2. Pombe M
3. Mwakembe
4. Mwamri

Nafikiri hivi vyote ni vichwa vizuri na vina msimamo, at least 50% ya Sokoine. Lakini wanaogopwa hao!!!!
 
Hawezi kumchagua hata siku moja. Sita ni mtu anayependa kuongea lililo kichwani bila kujali athari 'loose cannon'. akiwa msaidizi wa Kikwete kutakuwa na mkanganyiko wa ajabu sana.

Katika kipindi hiki ambacho tumepoteza imani na Serikali chini wa waziri mkuu Pinda, Ni vyema JK akamteua Samwel Sita awe waziri mkuu. Hii itamsaidia angalau kumaliza muda wake wa urais kwa heshima mbele. Huu ni wakati muafaka kwa JK kufanya maamuzi magumu kuipa heshima nafasi aliyonayo.
 
Hawezi kumchagua hata siku moja. Sita ni mtu anayependa kuongea lililo kichwani bila kujali athari 'loose cannon'. akiwa msaidizi wa Kikwete kutakuwa na mkanganyiko wa ajabu sana.
Ni kweli kabisa kookolikoo, na ndio maana nikasema ni wakati wake wa kufanya maamuzi magumu, yatakayo mrudishia heshima na angalau kujenga mstakabali mzuri kwa chama chake, nadhani hajachelewa sana.
 
Hawezi kumchagua sitta sababu ana kinyongo naye baada ya kutibua deal lake na EL la Richmond baada ya kuruhusu ile hoja bungeni.Ndiyo maana bibi kiroboto atasita kuruhusu hoja ya Mh.Zitto ili naye yasije mkuta.
 
Tatizo la Sitta bana, ni mnafiki! Ila utendaji wake angalau anaweza kumzidi Pinda . Huyu mtoto wa mkulima hajajitambua kama yeye ni waziri mkuu, hawezi hata kukemea mtendaji kata?. Mi sijui kizuri alichokifanya pinda ukiacha pale alipowadhalilisha wanaume kwa kulia hadharani kisa eti alitoa kauli za kutatanisha kuhusu mauaji ya albino. Mi Nikafikri analia kuwaonea huruma albino waliokuwa wanauawa kumbe laa! alilia kuona waandishi wa habari wanataka kumtilia mchanga kitumbua chake. Bora aondoke tu.
 
JK hajiamini hawezi kumchagua mtu ambaye atamzidi katika utendaji
 
... Sita ndo ataweza fanya kazi na JK..? Nani kakwambia Pinda ni tatizo...?

As a great thnker wapaswa fahamu tatizo ni nani...
 
... Sita ndo ataweza fanya kazi na JK..? Nani kakwambia Pinda ni tatizo...?

As a great thnker wapaswa fahamu tatizo ni nani...
Tatizo linajulikana ni JK na Pinda, ila tunaangalia kwa maslahi ya taifa nini kifanyike, unapokuwa na watu wawili kwenye uongozi wa nchi wsio na uwezo wa kufanya maamuzi kwa maslahi ya taifa ni tatizo kubwa.
 
... Sita ndo ataweza fanya kazi na JK..? Nani kakwambia Pinda ni tatizo...?

As a great thnker wapaswa fahamu tatizo ni nani...

yaani sitta alivo mjeuri atakuwa anakata simu za JK na hajibu message zake ...email akimtumia hajibu ...hahaaa nani anataka viungulia vya sitta..akiulizwa atasemaa aaah nilikuwa mbali na simu mara aaah simu iliisha chaji...
 
labda mwanri anaweza fanya jambo la msingi kama akimchagua coz huwa anasimammia yale anayoamini ni bora,
 
Kuna watu wanaogopwa na mafisadi, na wanaweka shinikizo wasipate nafasi nyeti. lakini wanamuharibia raisi wetu.

Mfano:
1. Six
2. Pombe M
3. Mwakembe
4. Mwamri

Nafikiri hivi vyote ni vichwa vizuri na vina msimamo, at least 50% ya Sokoine. Lakini wanaogopwa hao!!!!

Kuchagua waziri mkuu wa ku serve miaka miwili it's a waste of resources ....na kodi zetu kuendelea kuwalipia mafao...Kama hataki Pinda ..basi afanye recycling kwenye mawaziri wakuu waliopita..Kati ya Frederick sumaye,Salim Ahmed Salim ...,cleopa David msuya etc..Hawa at least wana nguvu ya kumalizia miaka miwili iliyobakia....mzee malecela naona umri na mwili vinachoka though bado Ana akili safi.....
 
Kuchagua waziri mkuu wa ku serve miaka miwili it's a waste of resources ....na kodi zetu kuendelea kuwalipia mafao...Kama hataki Pinda ..basi afanye recycling kwenye mawaziri wakuu waliopita..Kati ya Frederick sumaye,Salim Ahmed Salim ...,cleopa David msuya etc..Hawa at least wana nguvu ya kumalizia miaka miwili iliyobakia....mzee malecela naona umri na mwili vinachoka though bado Ana akili safi.....
Kwenye red, kwa upande mwingine tuangalie ambavyo nchi inapata hasara kwa hawa waliopo wanavyoendelea kutafuna nchi kama mchwa.
 
Back
Top Bottom