assadsyria3
JF-Expert Member
- Apr 9, 2013
- 6,904
- 4,050
Njoro wameokota kura 448 ltkt mfuko wa rambo, za CCM, wameokota katika pori huko Njoro.
Chanzo: Channel ten
Wakazi wa kata ya njoro katika wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro wameokota kura zipatazo 448 ,zikiwa kwenye mfuko uliyotupwa kandokando ya msitu wa asili wa njoro uliyopo katika kata ya hiyo ,baada ya kupata taarifa kutoka kwa mtua ambaye hakuweza kufahamika mara moja.
Akizungumza katika eneo la tukio ,katibu wa chama cha mapinduzi wilaya ya Moshi mjini Loti Olenesele amesema baada ya kupata tarifa walifika katika eneo hilo ,na kuzikuta kura hizo ambazo ni miongoni mwa kura zilizopigwa October 25 mwaka huu katika nafasi ya ubunge na urais kupitia CCM ,na kwamba zilikuwa na mhuri halali wa tume ya uchaguzi.
Mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro Aggy Mariale amesema awali kulikuwa na malalalamiko ya kupotea kwa masanduku mawili ya kura na kwamba baadhi ya mawakala halishatoa malaamiko kuhusu hujuma zilizo kuwa zikifanyika kwenye uchaguzi wa octoer 25 mwaka huu lakini hawakuweza kusikilizwa .
Chanzo: Channel ten