Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,185
- 307
Kero ya Fixed Charge kwenye ankara za Tanesco ni miongoni mwa kero nyingi ambazo zimekuwepo muda mrefu lakini hakuna hata kiongozi mmoja anayeelekea kuitatua.
Ukitaka kuweka umeme kwenye jengo lako na ukawafuata Tanesco watakwambia ulipe gharama za kuweka huo umeme, ambazo ni pamoja na gharama za kufungua file, utanunua meter, na gharama nyinginezo; na wakati mwingine utalipia nguzo ambayo baada ya hapo inakuwa mali ya Tanesco. Hizi kabla hujaweka gharama za kuwapoza wahusika ili kusudi file lako lisipotee au kuwekwa kwenye foleni na mizimu ambayo inaweza kukuchukua hata miaka mitano kama hautawatoa wahusika.
Cha kushangaza ukianza kutumia huo umeme wanacharge, pamoja na mambo mengine FIXED CHARGE, hii ni gharama ya kudumu na sijui ni kwa ajiri ya kugharimia kitu gani.
Miujiza haishii hapo tu, lakini inaongezeka na kuwa mauza uza pale shirika hili linapolitiwa kuwa linaendeshwa kwa hasara!!!
Sijasikia hata mgombea yeyeto wa ngazi ya urais au ubunge ambaye anataka kuishughulikia kero hii.
Jana nilinunua umeme wa luku wa sh.30,000 na jumla ya kodi mbali mbali nilizolipa zilikuwa ni 10,150 hii ina maana kuwa ninachangia kodi za serikali kwa takribani asilimia 49% ya kila umeme ninaonunua . Hii ni kodi kubwa sana na ninastahili kupata huduma stahili siyo kukatiwa umeme bila taarifa, kupata umeme chini ya kiwango (low voltage), kuchelewa kurejeshewa umeme pindi linapotokea tatizo kwenye mfumo wa usambazaji au uzalishaji.
Ninaomba kero hii ipatiwe majibu
Ukitaka kuweka umeme kwenye jengo lako na ukawafuata Tanesco watakwambia ulipe gharama za kuweka huo umeme, ambazo ni pamoja na gharama za kufungua file, utanunua meter, na gharama nyinginezo; na wakati mwingine utalipia nguzo ambayo baada ya hapo inakuwa mali ya Tanesco. Hizi kabla hujaweka gharama za kuwapoza wahusika ili kusudi file lako lisipotee au kuwekwa kwenye foleni na mizimu ambayo inaweza kukuchukua hata miaka mitano kama hautawatoa wahusika.
Cha kushangaza ukianza kutumia huo umeme wanacharge, pamoja na mambo mengine FIXED CHARGE, hii ni gharama ya kudumu na sijui ni kwa ajiri ya kugharimia kitu gani.
Miujiza haishii hapo tu, lakini inaongezeka na kuwa mauza uza pale shirika hili linapolitiwa kuwa linaendeshwa kwa hasara!!!
Sijasikia hata mgombea yeyeto wa ngazi ya urais au ubunge ambaye anataka kuishughulikia kero hii.
Jana nilinunua umeme wa luku wa sh.30,000 na jumla ya kodi mbali mbali nilizolipa zilikuwa ni 10,150 hii ina maana kuwa ninachangia kodi za serikali kwa takribani asilimia 49% ya kila umeme ninaonunua . Hii ni kodi kubwa sana na ninastahili kupata huduma stahili siyo kukatiwa umeme bila taarifa, kupata umeme chini ya kiwango (low voltage), kuchelewa kurejeshewa umeme pindi linapotokea tatizo kwenye mfumo wa usambazaji au uzalishaji.
Ninaomba kero hii ipatiwe majibu