Ni lugha tu za kisheria Mwanakijiji. Hatma ya wote wawili ni kuondoka/ kuondolewa madarakani. Si unajua wanasheria wanavyopenda kupamba lugha yao ili angalau kuonyesha tofauti za watu hao wawili. Nafasi ya WAZIRI MKUU wetu imekuwa pambo kupita kiasi. WM wetu ni kama kiranja mkuu wa shule ambaye hawezi kumwadhibu kiranja mwingine halafu tunamtwisha zigo la hawa wateule wabovu wa Rais. Bunge liwe wazi.Bunge haliwezi kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais; hakuna mfumo huo. Linaweza kumshtaki Rais kibunge (impeachment).