silver25
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 743
- 44
Mchungaji Christopher Mtikila wa DP amesema atafungua kesi mahakamani kupinga uamuzi wa Nec kumuengua katika kinyanganyiro cha urais.
Mtikila, ambaye alienguliwa kwa madai ya kutotimiza masharti ya kuwa na wadhamini 200 katika mikoa 10 ya Tanzania Bara, alisema kuwa Watanzania zaidi ya milioni 10 ambao hawakupiga kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka huu, walifanya hivyo kwa kuwa hakugombea urais.
Ndio; waliojiandisha kupiga kura walikuwa watu karibu milioni 20, lakini waliojitokeza kupiga kura walikuwa milioni 8.4, kati ya hao waliomchagua aliyekuwa mgombea wa CCM walikuwa milioni 5.8. Sasa hawa ambao hawakujitokeza kupiga kura wangenichagua mimi kwa sababu ya itikadi na sera zangu za kuleta ukombozi nchini Tanzania, alisema Mtikila.
Mtikila alisema kutokana na hali hiyo ameiandika Nec barua akiitaka kufanya upya uchaguzi wa urais kwa kuwa haikumtendea haki.
Mtikila, ambaye alienguliwa kwa madai ya kutotimiza masharti ya kuwa na wadhamini 200 katika mikoa 10 ya Tanzania Bara, alisema kuwa Watanzania zaidi ya milioni 10 ambao hawakupiga kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka huu, walifanya hivyo kwa kuwa hakugombea urais.
Ndio; waliojiandisha kupiga kura walikuwa watu karibu milioni 20, lakini waliojitokeza kupiga kura walikuwa milioni 8.4, kati ya hao waliomchagua aliyekuwa mgombea wa CCM walikuwa milioni 5.8. Sasa hawa ambao hawakujitokeza kupiga kura wangenichagua mimi kwa sababu ya itikadi na sera zangu za kuleta ukombozi nchini Tanzania, alisema Mtikila.
Mtikila alisema kutokana na hali hiyo ameiandika Nec barua akiitaka kufanya upya uchaguzi wa urais kwa kuwa haikumtendea haki.