Kupungua kina Ziwa Viktoria Uganda ina hisa

Mgoyangi

Senior Member
Feb 6, 2008
184
9
Mtaalamu adai Uganda ndiyo inayolihujumu Ziwa Victoria

Paul Mabuga, Mwanza Mei 7, 2008

Sato wamepungua kwa karibu asilimia 80

KUPUNGUA kwa kasi kwa kina cha maji katika Ziwa Viktoria hakusababishwi tu na mabadiliko ya tabianchi (climate change) bali na kuanzishwa kwa mabwawa ya kufua umeme nchini Uganda, utafiti mpya umeonyesha.

“Kwa kiasi kikubwa kupungua kwa maji ya kina cha Ziwa Viktoria kunatokana na shughuli za binadamu na si mabadiliko ya tabianchi. Na hii ni baada ya Uganda kukiuka kanuni za matumizi ya maji ya Ziwa hilo,” anasema mtafiti kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Taifa (TANAPA), Yustina Kiwango katika taarifa ya utafiti wake.

Kwa mujibu wa ripoti ya mtafiti huyo, baada ya Uganda kujenga Bwawa la Kiira mwaka 2000 na hivyo kuwa na mabwawa mawili ya kuzalisha umeme katika mji wa Jinja, jingine likiwa ni lile Nalubaale ( zamani Owen Falls), ilitumia maji kwa wingi kinyume cha makubaliano yake na Misri yaliyofikiwa mwaka 1957 kuhusu matumizi ya maji ya Ziwa Viktoria.

Kulingana na utafiti huo, mabwawa hayo yamekuwa yakifyonza maji kutoka Ziwa Viktoria katika kiwango cha asilimia 20 hadi 50 ambacho ni juu ya kile kilichokubaliwa na nchi hizo mbili. “Ni kutokana na hali hiyo, kina cha maji katika Ziwa Viktoria kilipungua kwa mita mbili na nusu kwa kipindi cha kati ya mwaka 2000 hadi 2006.”

Serikali ya Uganda katika miaka ya 1990 ilitoa kipaumbele katika upanuzi wa huduma ya ugavi wa umeme kama njia ya kukabiliana na umasikini na kuinua uchumi hususani katika maeneo ya vijijini ambako asilimia 90 ya wananchi wanaishi.

Chini ya mpango huo iliamuliwa kuwa Bwawa la Nalubaale lipanuliwe na kuzalisha zaidi umeme kutoka uwezo wa megawatt 180 na kufikia megawatt 380. Bwawa la Kiira lilianza kuzalisha umeme mwaka 2000 kwa uwezo wa megawatt 200.

Kiwango anaeleza katika utafiti wake kuwa mapitio ya mwenendo wa mvua kwa karibu miaka 100 katika eneo la Ziwa Viktoria na vyanzo vyake, yanaonyesha kuwa, hali ya hewa inaweza kuwa inachangia uhaba wa mvua na kupungua kwa kina, lakini si katika kiwango kikubwa kama hicho na hivyo sababu pekee kuwa ni mabwawa haya mawili ya Jinja .

Katika utafiti huo uliosimamiwa na Eric Wolasnki wa Chuo Kikuu cha Cook cha Australia, Kiwango anaonyesha kuwa kupungua huko kwa kina cha Ziwa Viktoria kuna athari kubwa kwa wananchi wanaolitegemea Ziwa hilo kwa ajili ya kipato na chakula, na hivyo kuifanya hali hiyo kuwa hatari kwa maisha ya watu hao. Zaidi ya watu milioni tatu katika Afrika Mashariki huendesha maisha yao kutokana na Ziwa Victoria.

Ufuatiliaji wa takwimu za miaka zaidi ya sita katika Rasi ya Mlaga unaonyesha kuwa samaki wa asili wa ziwa hilo hususan Sato, wamepungua kwa karibu asilimia 80. Hali hiyo, kwa mujibu wa utafiti huo, inasababishwa na kukauka kwa ardhioevu ya Mirutende ikiwa ni matokeo ya kupungua kwa kina hicho.

Ardhioevu ya Mirutende (papyrus wetlands) hutumiwa na samaki wa asili wa Ziwa Viktoria kwa ajili ya kujificha wakati wanapowindwa na pia kama sehemu ya kuzaliana. Samaki hukulia katika maeneo hayo wakila wadudu na mimea iliyopo katika eneo hilo.

Maeneo ya ardhioevu ya Mirutende, kwa mujibu wa utafiti huo, ina hewa ndogo ya oksijeni, kiasi ambacho samaki wakubwa kama Sangara, ambao hula samaki wadogo, hawawezi kuishi na kuwashambulia samaki hao katika maeneo hayo. Pia Mirutende huchuja kemikali zinazoingia ziwani kutoka viwandani. Mimea hiyo imekauka baada ya ziwa kupungua kina.

Ni rai ya Kiwango kwamba maisha ya watu kando kando ya Ziwa Viktoria yanategemea ardhioevu ya Mirutende, na anatoa wito kwa Serikali na mamlaka katika ukanda wa ziwa hilo, kuliangalia suala hilo na kuja na mikakati madhubuti ambayo itadhibiti suala la kupungua kwa kina cha maji katika ziwa hilo.

Lakini wakati utafiti huo unawanyooshea kidole Waganda, lakini pia pameibuka tatizo jingine; nalo linahusu mradi wa kutoa maji Ziwa Viktoria, katika eneo la Ihelele, wilayani Misungwi, Mkoani Mwanza, kwenda katika miji ya Kahama na Shinyanga ambao kwa sasa upo katika hatua za kukamilika.

Mtafiti huyo anaamini, hata hivyo, kwamba kwa Watanzania kuna nafuu ya hoja; kwani mradi huo utakuwa ukifyonza meta za ujazo 80,000 kwa siku, kiwango ambapo ni karibu mara 300 ikilinganishwa na kinachofyonzwa na mabwawa mawili ya umeme ya Uganda ya Nalubaale na Kiira ambayo huchota jumla ya meta za ujazo 25.920,200 kwa siku.

Mradi wa kutoa maji Ziwa viktoria kwenda miji ya Kahama na Shinyanga unatarajia kuwanufaisha wananchi wapatao 420,000 baada ya kukamilika, kiwango ambacho baadaye kinatarajiwa kufikia watu milioni moja katika kipindi cha miaka 20 ijayo.
 
Juhudi za pamoja, lazima zifanyike kuliokoa ziwa Viktoria.La msingi chanzo kimashajulikana so is a matter of taking a critical decision
 
ningekuwa na uwezo,ningehamishia maji yote ya ziwa victoria kuanzia shinyanga, Mwanza, Dodoma, singinda na kwingine. Nisingeogopa au ku be influenced na watafiti wanaodhaminiwa na nchi ya Misri, nchi ambayo siku zote imekuwa ikiwazinguwa nchi za maziwa makuu zisitumie vizuri maji hayo,na kuwatishia kuwa wataanzisha vita na sisi.wajinga kweli wale.
 
Mtaalamu adai Uganda ndiyo inayolihujumu Ziwa Victoria



Kwa mujibu wa ripoti ya mtafiti huyo, baada ya Uganda kujenga Bwawa la Kiira mwaka 2000 na hivyo kuwa na mabwawa mawili ya kuzalisha umeme katika mji wa Jinja, jingine likiwa ni lile Nalubaale ( zamani Owen Falls), ilitumia maji kwa wingi kinyume cha makubaliano yake na Misri yaliyofikiwa mwaka 1957 kuhusu matumizi ya maji ya Ziwa Viktoria.

Mtaalamu je ni kiasi gani cha maji kinachopotea Sdani kutokana na kusambaa kwa maji bila mpangilio? Tuwe wa kweli Uganda haikuingia makubaliano yeyote na Misri kuhusu matumizi ya maji ya mto Nile bali Uingereza kwa manufaa yake ya kupata nafuu kupitsha meli zake Suez.
Tanzania tutakalia ku honour ikataba iliyopitwa na wakati wakati sis tukifa njaa. Misri wanatakiwa, kama kweli wana wasiwasi na maji, kuchngia jinsi ya kuzuia evaporation ya maji Sudani.
Hebu fikiria tunavyonyanyaswa na umasikini kwa kutoruhusu wanachi kuvua samaki wadogo ziwa Victoria ilhali makampuni ya kusindika samaki wakifanya hivyo bila kukalipiwa. Kisa mikataba. Sioni kama kweli wataalamu wetu wanajali kwa nini bado wnaruhusu kujengwa kwa viwanda vya kusindika samaki. Je tunataka Darwin's Nightmare nyigine.
Uganda lazima iangalie maslahi ya watu wake kwanza, kama sisi hatuwezi tufunge mdomo. Tafiti hizi ni funded by interest group as we see the impartiality of the contributors on the subject. The world bank funded the said dam. What was their enviromental impact opinion?
 
Nawasifu uganda kwa kutumia maji waliyopewa na Mungu. sisi kama hatutatumia, na tukae kimya. Mungu katuma maji hadi chumbani, maji yanayotumiwa na wenzetu wengine wengi. wenzetu wakitumia vibaya, sisi tunasema hapana, sisi ni watakatifu, tusitumie sana. kalaga baho. mikoa mikame ya singida, shinyanga, Dodoma na mingine, inahitaji maji ya kunywa, na maji ya kumwagilia ili tupate zabibu kibao kule dodoma, na tuanzishe hata umwagiliaji kule shinyanga na singida. sisi tumenyamaza, tuna toma majicho tu. kalaga baho. uganda wao wamevuta maji yale, na wanatengeneza umeme, wamevuta na kutumia kwa vitu vingi. ndo wanaotumia kwa kiasi kikubwa East africa nzima. sisi tuna toa mimacho tu. kama misri wanataka tusipunguze yale maji, maliasili ambayo Mungu alitupatia kwenye nchi yetu, basi na wao wachimbe mafuta yao yale mengi, watuletee tutumie kwa garama nafuu kwenye magari yetu hapa. wao wanakaa mbali, wana control utumiaji maji kwenye nchi nyingine...upuuzi huu.

kwanza ule mkataba wa waingereza wa kutotumia maji kupita kiasi, kwenye strategic area yao ya ziwa victoria, ulishaenda kutanguliwa na nyerere mda. mimi ninacho kitabu chake cha "nyerere jornal" moja hivi, ule mkataba haupo kabisa. labda kama bado wenzetu wa kenya na ug hawakuutangua. chao.
 
Napenda kuungana na wana JF kuipongeza Uganda kwa kutumia maji kwa manufaa ya taifa lao. Pia naomba huyu mtafiti atuweke wazi au afanye utafiti kuona nia kiasi gani cha maji kutoka katika ziwa hili kinatumika huko Misri. Nafikiri watanzania tuna haki ya kutumia maji haya kwani yapo kwetu. Thanks kwa mradi unaokamilika ningependelea hata sisi tutumie maji haya kwa kuzalisha umeme kwani bado ni tatizo bongo lakini Misri sizani kama ni tatizo kwao. Au bado wana kasumba kwamba wao wamestaarabika na sisi hatujastaarabika hivyo bila huduma muhimu tutaishi tu no no hiyo haipo kunawastaarabu wengi sasa hivi sio kama zamani. Misri ni taifa lilioendelea wanatakiwa kusaidi hasa nchi zilizo ktk bonde la nile na ziwa victoria kwani wanatumia hichi chanzo kwa maendeleo yao.
 
huo mkataba wa 1957 na ule wa 1929 (nadhani) tanzania haiitambui na ndio umekuwa msimamo wa serikali siku zote. waganda waliruhusu timu ya
waegypt kuwepo uganda na kuweka kituo cha utafiti kinachofuatilia
kina cha ziwa viktoria. mimi nashangaa kusikia kina kimepungua
bila ya waegypt kuweka zengwe la nguvu na kwamba waliruhusu
waganda kujenga mabwawa bila zengwe.

tathmini yangu ni kwamba waganda na waegypt wamekubaliana kuhusu matumizi ya maji na kwamba hii chokochoko ya kupungua kwa kina
cha ziwa viktoria inalengwa tanzania ili sisi tusitishe miradi ya matumizi
ya maji ya ziwa viktoria, kisa, kina tayari kinapungua! naweza kuwa
nimekosea lakini nahisi waganda na waegypt lao moja! ni mawazo tuu.
 
huo mkataba wa 1957 na ule wa 1929 (nadhani) tanzania haiitambui na ndio umekuwa msimamo wa serikali siku zote. waganda waliruhusu timu ya
waegypt kuwepo uganda na kuweka kituo cha utafiti kinachofuatilia
kina cha ziwa viktoria. mimi nashangaa kusikia kina kimepungua
bila ya waegypt kuweka zengwe la nguvu na kwamba waliruhusu
waganda kujenga mabwawa bila zengwe.

tathmini yangu ni kwamba waganda na waegypt wamekubaliana kuhusu matumizi ya maji na kwamba hii chokochoko ya kupungua kwa kina
cha ziwa viktoria inalengwa tanzania ili sisi tusitishe miradi ya matumizi
ya maji ya ziwa viktoria, kisa, kina tayari kinapungua! naweza kuwa
nimekosea lakini nahisi waganda na waegypt lao moja! ni mawazo tuu.

Kafara upo sahihi, mikoa ya kati Tanzania bado hatujafaidika na hayo maji ya ziwa kama hawa watu wanavyojifaidisha nayo!...


Since late 2003, Lake Victoria's water level has dropped over 1.1 m from its 10-year average. As of December 27, 2005, it was approximately 10.69 m, reaching the lowest level since 1951 (USDA, 2005). Recent severe drops in Lake Victoria (2004-2005) are approximately 45% due to drought and 55% due to over-releases from the Owen Falls Dam.

Water experts believe there is not enough water in the Nile river to meet the various irrigation goals of the Nile basin nations
. Adding to potential water stress, many large hydropower dams also being considered for the Nile. Some are already built or under construction, including the High Aswan (Egypt), Merowe (Sudan), and Tekeze and Gilgel Gibe in Ethiopia. Others, such as the Bujagali and Karuma dams (Uganda), remain in the planning stages at this time. All of these competing projects combined with the coming impacts of climate change could send the region's already over–tapped water resources into crisis, leave economies weaker rather than stronger, and do little to reduce ongoing conflict over the Nile.

Although specialists have explained away the drop in the level of water to prolonged drought and the engineering mistake done on Kiira dam, it has not prevented a furious debate involving accusations of who is to blame for the mess.

source; http://www.idrc.ca/fr/ev-94284-201-1-DO_TOPIC.html
 
Our problem is looking at part of the whole picture.
What is the list of reasons leading to the problem at hand?
 
Back
Top Bottom