Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,690
- 20,445
Alitimuliwa na nani, na kanisa au serikali?...Tunakumbuka kwamba matokeo mojawapo ni kutimuliwa kwa Katibu Mkuu wa TEC wakati huo, Raymond Sabas, na kutangazwa siyo raia.
Alitimuliwa na nani, na kanisa au serikali?...Tunakumbuka kwamba matokeo mojawapo ni kutimuliwa kwa Katibu Mkuu wa TEC wakati huo, Raymond Sabas, na kutangazwa siyo raia.
Serikali, ila naamini Pengo alimtoa kafara. Sikusikia Kanisa likihangaika juu yake. Wala Askofu NiweMugizi hakupata utetezi wowote. Ni pale Magu alipogundua kwamba kama anafariki, atazikwa na NiweMugizi. Hapo ndio akaachia paspoti yake, siku za mwishoAlitimuliwa na nani, na kanisa au serikali?
Unaamini sio! Kwamba hauna uhakika wala uthibitisho, ila unaamini!Serikali, ila naamini Pengo alimtoa kafara.
UsinipangieKKKT hii hii ya Chadema ndo unaona Ni Bora kuliko RC kwenye kukemea watawala?
Usilete siasa kwenye huu uzi.
Hakuna anayelitaka Kanisa Katoliki libebe majukumu ya mtu mmoja mmoja, taasisi za kiraia za kupigania haki au vyama vya siasa. Lakini kutowajibika kwa mtu mmoja mmoja au vyama vya siasa au taasisi nyingine, hakuhalalishi kwa Kanisa Katoliki kutofanya yaliyo sehemu ya wajibu wake kwa kuzingatia nafasi yake kwa sisi waumini wake, hata kama ingekiwa ni nchi ya chama kimoja au nchi isiyo na chama chochote cha siasa.Umeshawekewa ujumbe wa kanisa Katoliki juu kule ambao umekiri ulikuwa huufahamu, lakini nakushangaa bado unapiga kelele tu, au ndio vile hutaki uzi wako ukose wachangiaji?
Hii tabia mnayoendekeza kulaumu Katoliki kwa kila jambo kama vile nyie hamna midomo ya kujisemea na kuwasemea hao mnaoona wanaonewa itawadumaza akili, haki za watu zitazidi kuporwa huku nyie mmezubaa tu kulisubiri Kanisa Katoliki.
Msipojinasua kwenye hili tope la fikra mlilokwama, huku mkijiita GT, CCM itatawala milele, amka badala ya kulaumu kila siku anzeni kudai haki zenu privately, au kwa makundi, mjue namna mtakavyo organise ili mfikie malengo, sio kulia lia kila siku kwa Katoliki, lisingekuwepo mngefanyaje?
Walio kemea ni Dini gani au madhehebu gani?Kanisa Katoliki halijawahi kukemea dhuluma kokote kule lilipo;
Slave Trade
World War I & II
Nazi Regime
Mussolini Regime
Apartheid
Rwanda Genocide
etc
Jamani wanasiasa pambaneni tu kwa nguvu za wanasiasa,tatizo siasa inausaliti mkubwa sana,viongozi wa dini wanaweza kusimama lakini mwisho wa siku haohao ambao wanaoneka kuonewa,wakipata madaraka wanasau au kubadirika kabisa.Kiukweli, ndani ya kanisa katoliki kuna misigano. Ndio maana hata kipindi ule waraka maarufu wa "Ujumbe wa Kwaresima" ambao Kanisa Katoliki lilitoa makaripio kwa serikali katika maeneo ya Demokrasia, uhuru wa kujieleza na utawala bora, Kardinali Pengo, wakati huo akiwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, alitangaza kujiweka kando na waraka huo. Tunakumbuka kwamba matokeo mojawapo ni kutimuliwa kwa Katibu Mkuu wa TEC wakati huo, Raymond Sabas, na kutangazwa siyo raia.
Ni kweli kwamba, kama asemavyo Tundu Lissu, Makanisa ya Tanzania kwa ujumla yamejitenga na mapambano ya kudai haki na Uhuru wa kujieleza. Mara chache Kanisa Katoliki lilipojikakamua, KKKT nao wamewaunga mkono, hasa kupitia Askofu wao mkuu Shoo.
Haya malalamiko yenu nimekuja kugundua wale wote wa aina yako mnakiri ukuu wa Kanisa Katoliki ndio maana wote bila kujali madhehebu au dini zenu hamuishi kulipelekea lawama, ni kama vile inavyokuwa kwa baba na watoto nyumbani.Hakuna anayelitaka Kanisa Katoliki libebe majukumu ya mtu mmoja mmoja, taasisi za kiraia za kupigania haki au vyama vya siasa. Lakini kutowajibika kwa mtu mmoja mmoja au vyama vya siasa au taasisi nyingine, hakuhalalishi kwa Kanisa Katoliki kutofanya yaliyo sehemu ya wajibu wake kwa kuzingatia nafasi yake kwa sisi waumini wake, hata kama ingekiwa ni nchi ya chama kimoja au nchi isiyo na chama chochote cha siasa.
Yawezekana mchango wangu ukawa mdogo, lakini kwa nafasi yangu kama mtu mmoja na siyo taasisi, naridhika kuwa nimetimiza wajibu wangu;Haya malalamiko yenu nimekuja kugundua wale wote wa aina yako mnakiri ukuu wa Kanisa Katoliki ndio maana wote bila kujali madhehebu au dini zenu hamuishi kulipelekea lawama, ni kama vile inavyokuwa kwa baba na watoto nyumbani.
Kule juu nimekusoma unakiri mahali ulikuwa huujui au hujawahi kuuona waraka wa Kanisa Katoliki wa Kwaresma uliotolewa enzi za mwendazake na kuzua sintofahamu mpaka baadhi ya mapadri wakaitwa sio watanzania, lakini pamoja na hayo, bado unalia tu unataka zaidi, sasa nikuulize, kabla hujapewa hiyo zaidi wewe na wenzio mmechangia nini kuondoa hali iliyopo?
Hakuna kanisa siku hizi. Kila mtu anaangalia Tumbo lake tu.Tangu kale, tangu enzi za manabii, Kanisa lilisimama katika ukweli, lilifundisha, lilikemea na kuwaonya watawala dhidi ya dhuluma. Mifano ipo mingi.
Muelekeo huo wa Kanisa uliwaongezea imani kubwa waumini, wasio waumini na hata watawala waliheshimu sana kauli za Kanisa kwa sababu waliamini kuwa wakati wote Kanisa lilisimama katika haki na ukweli ambao msingi wake mkubwa ni Kristo mwenyewe. Kristo, hata alipokuwa pekee yake dhidi ya maelfu ya wayahudi, aliendelea kusimama katika ukweli. Kuna maneno mawili ambayo yametokea mara nyingi katika biblia kuliko mengine yote. La kwanza ni upendo (mara 320) na la pili ni ukweli (mara 222).
Kanisa Katoliki katika mataifa mengi liliweza kuwasemea wanaodhulumiwa, na hata hapa kwetu, wakati TEC ilipokuwa ikiongozwa na baadhi ya viongozi (Rais wa TEC), kanisa lilikuwa na msimamo na kauli zilizo thabiti kwa watawala dhidi ya dhuluma.
Kanisa Katoliki lilianza kuwa kimya kabisa, na kwa namna fulani kuonekana kubariki matendo ya dhuluma kama vile kupotezwa watu, kutekwa, kuuawa, kubambikiwa watu kesi tangu TEC iliporidhia kumchagua kiongozi wake mwenye mahusiano ya karibu na watawala, eti kwaajili ya kupunguza tension kati ya Serikali na Kanisa. Kanisa limeondoka kutoka kwenye jukumu lake la msingi la kuwa sauti ya wasio na sauti wanapoonewa, mpaka kuwa mwandani wa Serikali hata pale serikali inapofanya dhuluma. Hali hii inaendelea kudhoofisha sana imani yetu kwa kanisa la Kristo na viongozi waliostahili kuyaishi maandiko.
Kuhusu haki za wananchi, Kanisa la Ulimwengu linasema yafuatayo:
The dignity of human life
Christians believe that all human life is sacred, unique and God-given. They also believe that all humans are made in the image of God.
Then God said, “Let us make mankind in our image, in our likeness, so that they may rule over the fish in the sea and the birds in the sky, over the livestock and all the wild animals, and over all the creatures that move along the ground.Genesis 1:26-27
Christians believe this to mean that many of the characteristics of God are reflected in humans. As a result, Christians believe that all human life should be treated with respect and dignity.
The belief that all humans are special can be seen in a document known as The Universal Declaration of Human Rights, which sets out all the different rights that every human should be entitled to.
As a result of the belief that all human life is special and God-given, Christians will try to do all they can to promote human rights. Human rights refer to the basic freedoms and rights of every human being in the world. Christians do this in many different ways including supporting charities such as Amnesty International who campaign for human rights.
Kanisa Katoliki la Tanzania, kwa kutokemea matendo yasiyo ya haki, limeendelea kuwa sehemu ya familia ya wakatoliki Duniani au limejitenga na jamii nyingine za wakatoliki?
you nailed it.. ila Inamaana kanisa halijui ujinga wa watawaliwa hata liamue kunyamaza bila kukemea watawala? najua, linajua.Sasa kama anayetawaliwa kwa dhulma anaona sawa,kanisa lifanyeje sasa ndugu yangu? Wanaopaswa kusimama kwa dhati haswa ni wananchi
Unaposema hujawahi kuuza utu wako licha ya vishawishi vingi vya kupewa cheo huku ukiwa na fake id, hakuna anayekujua, hii kwangu ni kujikweza tu, hebu andika hoja zenye mantiki hapa.Yawezekana mchango wangu ukawa mdogo, lakini kwa nafasi yangu kama mtu mmoja na siyo taasisi, naridhika kuwa nimetimiza wajibu wangu;
1) Sijawahi kuuza utu wangu, licha ya vishawishi vingi vya kupewa cheo, na nitasimama hivyo daima.
2) Sijawahi kukosa kuwa mkweki wa nafsi yangu katika mambo ninayoyaamini ni sahihi au siyo sahihi.
3) Mara kadhaa nimetoa kile nilicho nacho kuwagharamia wale wanaoteswa na watawala pasipo haki.
4) Sijawahi kuunga mkono ugandamizaji wa aina yoyote dhidi ya yeyote kwa kauli au matendo.
Zaidi ya hapo, unahitaji nguvu za taasisi, vinginevyo utapotezwa na wala isijulikane kama ulikuwa ukitetea chochote.
Kanisa Katoliki ni taasisi kubwa, imara na yenye nguvu Duniani. Ni kweli kuna waraka uliwahi kutolewa dhidi ya utawala kuhusiana na uonezi. Lakini hata kauli ile ilikosa nguvu kutokana na mgawanyiko miongoni mwa viongozi wa Kanisa. Hata wale mapadre na Askofu walioanza kuandamwa na dola kulitokana na mgawanyiko ndani ya Kanisa lenyewe lakini Kanisa Katoliki lisingeweza kupuuzwa kama kusingekuwa na mgawanyiko, na wala wale mapadre na Askofu wasingeweza kuzongwa na Serikali kama ilivyotokea.
Kuna dalili ya taasisi hii kukosa mwelekeo thabiti. Kanisa Katoliki linalojulikana kwa nidhamu, inawezekanaje baada ya kauli ya TEC, Askofu Mkuu mmoja anatoka na kusema, mimi siyo sehemu ya hiyo kauli ya Kanisa???
Waraka wa Kwaresma niliuona na ninaufahamu. Nilidhani kuna mwingine zaidi ya ule ambao mmoja wa maaskofu wakuu aliukataa.Unaposema hujawahi kuuza utu wako licha ya vishawishi vingi vya kupewa cheo huku ukiwa na fake id, hakuna anayekujua, hii kwangu ni kujikweza tu, hebu andika hoja zenye mantiki hapa.
Unaposema hujawahi kuunga mkono ukandamizaji kwa wengine unamaanisha Kanisa Katoliki ndio linaunga mkono? na huo waraka wa Katoliki kukemea utawala uliopita hukuuona? au ndio umeuona ila umeutafutia sababu ya kitoto kisa ulipingwa na Askofu mmoja ndio unaukataa?
Habari ya msimamo wa Kanisa na kutaka kila mmoja aukubali ili wakufurahishe wewe nayo kwangu hata siielewi mantiki yako, naamini Kanisa halifanyii kazi maoni yako binafsi, linafanyia kazi kero zinazoikumba jamii kwa ujumla.
Mwisho, kama mapadri wengi walitoa msimamo wa kuandaa waraka na ukatolewa hiyo kwangu inatosha, inakwenda na dhana ya wengi wape, lakini wewe mwenzangu, unamtumia huyo mmoja alieukataa waraka kama kigezo cha kupinga msimamo wa Kanisa Katoliki ili kuhalalisha madai ya uzi wako, hii judgement yako kwangu naiona ya kitoto.
Huu uzi wako in real sense hauna mantiki, unaulazimisha tu uendelee kuwepo hapa kwa hoja zako za kibinafsi, unatafuta "vijisababu" kupinga mambo ya msingi yanayofanywa na Kanisa Katoliki, nikiamini fika wakati unaanzisha huu uzi, hata Waraka wa Kwaresma wa Kanisa Katoliki ulikuwa hujui kama upo, umeujulia hapa.
Tunachohitaji ni Katiba ambayo itawezesha serikali iliyoko madarakani iwajibike kwa wananchi, kama sivyo wananchi wawe na uwezo wa kuiondoa madarakani. Katiba Mpya. Kwa hiyo hata CHADEMA wakiingia madarakani, watawajibika kwa Katiba hiyoJamani wanasiasa pambaneni tu kwa nguvu za wanasiasa,tatizo siasa inausaliti mkubwa sana,viongozi wa dini wanaweza kusimama lakini mwisho wa siku haohao ambao wanaoneka kuonewa,wakipata madaraka wanasau au kubadirika kabisa.
Muongo mkubwaYawezekana mchango wangu ukawa mdogo, lakini kwa nafasi yangu kama mtu mmoja na siyo taasisi, naridhika kuwa nimetimiza wajibu wangu;
1) Sijawahi kuuza utu wangu, licha ya vishawishi vingi vya kupewa cheo, na nitasimama hivyo daima.
2) Sijawahi kukosa kuwa mkweki wa nafsi yangu katika mambo ninayoyaamini ni sahihi au siyo sahihi.
3) Mara kadhaa nimetoa kile nilicho nacho kuwagharamia wale wanaoteswa na watawala pasipo haki.
4) Sijawahi kuunga mkono ugandamizaji wa aina yoyote dhidi ya yeyote kwa kauli au matendo.
Zaidi ya hapo, unahitaji nguvu za taasisi, vinginevyo utapotezwa na wala isijulikane kama ulikuwa ukitetea chochote.
Kanisa Katoliki ni taasisi kubwa, imara na yenye nguvu Duniani. Ni kweli kuna waraka uliwahi kutolewa dhidi ya utawala kuhusiana na uonezi. Lakini hata kauli ile ilikosa nguvu kutokana na mgawanyiko miongoni mwa viongozi wa Kanisa. Hata wale mapadre na Askofu walioanza kuandamwa na dola kulitokana na mgawanyiko ndani ya Kanisa lenyewe lakini Kanisa Katoliki lisingeweza kupuuzwa kama kusingekuwa na mgawanyiko, na wala wale mapadre na Askofu wasingeweza kuzongwa na Serikali kama ilivyotokea.
Kuna dalili ya taasisi hii kukosa mwelekeo thabiti. Kanisa Katoliki linalojulikana kwa nidhamu, inawezekanaje baada ya kauli ya TEC, Askofu Mkuu mmoja anatoka na kusema, mimi siyo sehemu ya hiyo kauli ya Kanisa???