Kupotea kwa Dkt. Cyrilo na ukimya wa media za Tanzania

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
48,776
102,133
242840835_4424551550969836_8204023089223661494_n.jpg
Nimesikitika sana kuona @dr_chriscyrilo yupo ndani siku 3 lakini hakuna main stream media iliyojishughulisha kuripoti zaidi ya @bbcswahili. Yani media za Ulaya zinaumizwa na matukio ya uonevu na zinaonesha kujali zaidi utu wetu kuliko media zetu? Seriously? Mnataka nani "akamatwe" ndio mripoti?

@dr_chriscyrilo daktari wa binadamu, baba wa mtoto mmoja, ndugu na rafiki wa wengi. Hospitali anayofanyia kazi inafahamika, nyumba anayoishi inafahamika. Kwanini hamkumpelekea arresting warranty kazini au nyumbani kwamba anahitajika polisi ili aende mwenyewe? Kwanini mnamvizia na kumkamata kama jambazi? Na media zetu zinaona ni sawa tu? Daktari anakamatwa kama jambazi kwenu sio story?

Na hii si mara ya kwanza kukalia kimya matukio ya watu kukamatwa, kutekwa au kupotezwa. Wakati wa #BenSaanane tulipiga kelele wenyewe huku mitandaoni. Hakuna media iliyojishughulisha kuripoti. Baadae sana baada ya matumaini ya kumpata kupotea ndio media zikaanza kuripoti, but was too late.

Waandishi walipoanza kutekwa na kupotezwa ndio main stream zikaanza kuzipa uzito habari za watu kutekwa.

Kwenye "awamu hii" waandishi mnaweza kujiona salama kwa sababu hamjaanza "kushughulikiwa". Kwahiyo mnaona ni mambo yanayowahusu wakosoaji wa mitandaoni tu. Lakini amin amin nawaanbia, ipo siku itatokea kwenu na hakutakua na mtu wa kuwatetea. No one is safe in the situation of injustice.

Mchungaji Martin Niemöller aliwahi kusema "Waliwaua wajamaa, sikuwatetea kwa sababu sikua mjamaa. Kisha wakaenda kwa wafanyakazi, sikuzungumza kwa sababu sikua mfanyakazi. Wakaenda kwa wayahudi, sikuwatetea kwa sababu sikuwa Myahudi. Mwishowe wakaja kwangu, na hapakuwepo na aliyesalia kunitetea"

Credit: Malisa

My Take
Akipotea mwandishi wenu au kudakwa na polisi makelele kama yote. Ila kwa wengine mnakuwa kimyaaaa. Vita ya dhidi ya udhalimu haipiganwi hivyo.
 
Shida waliopo sasa hivi jikoni ni mabingwa wa kutoa bahasha za khaki kwenye media ili serikali isiandikwe vibaya.

Wakati wa Jiwe alikuwa hatoi baahadha, Bali alitumia ubabe. Hawa wa sasa hivi ni mabingwa, usisubiri kuona serikali ikiandikwa vibaya.

Pia Hawa wa sasa Wana vijana wao mitandaoni wa ku-cover ukosoaji wowote kwa serikali. Fikiria hadi dada wa US naye yumo kwenye list yao, ndio maana huoni akisema chochote kuhusu kesi ya mbowe.

Shida itakuka pale ambapo hangaya atataka kwenda nao tofauti. Ila akiwakumbatia basi humu mitandaoni na kwenye media hutaona ukosoaji.
 
Kuna tatizo kubwa Tanzania. Taasisi za kijamii zimetekwa, husikii hata moja iknyanyua kidole. Zipo tu sasa kufaidi uhondo wa viporo wanavyotupiwa.

Vyombo vya habari ni biashara, kazi yao kubwa ni kutengeneza pesa, hasa kutoka huko wanakotakiwa wapapigie kelele.

Lakini naamini matumaini ya mabadiliko makubwa sasa yapo na hakuna mwenye uwezo wa kuyazuia yasitokee.
 
Hatuna media sisis zote zinaangalia upande wa maslahi media zenyew zinasuguana vikali ata kwenye mambo yasiyokuwa ya msingi zitakuwa kweli na nguvu ya kuchunguz na kureplrt taarifa za upande wa yanga
 
Shida waliopo sasa hivi jikoni ni mabingwa wa kutoa bahasha za khaki kwenye media ili serikali isiandikwe vibaya...
Hii umeiweka vizuri sana.

Mama yupo kwenye kampeni 'mode' muda kitambo, sijui kwa nini watu hawalitambui hili. Tazama wasanii walivyopangwa, wanawake wanawekwa tayari na makundi mengine yote yanatazamwa, hakuna anayestuka, hasa hawa wenzetu wanasiasa wanaojipambanua kuwa ni wapinzani.

Wanasubiri hadi waje wastuliwe wakati mwenzao alishamaliza kazi tayari!

Vyama vya upinzani, hasa CHADEMA wanatakiwa wawe wanafuatilia kwa karibu kabisa yanayoendelea chini kwa chini juu ya kampeni hii ya kimya kimya, huku wao wakivurugwa.

Inaonyesha baada ya chama kuwapoteza wabunge, na sasa Mwenyekiti wao kuwa mahakamani huko ndani ya chama mambo yamekuwa baridi kabisa!

Taarifa kama hii iliyoletwa hapa wao ndio wangekuwa mbele kuiibua na kuwataarifu wananchi waone mambo yanavyoendelea kama zamani.
 
Ni Mwanaharakati wa muda mrefu na rafiki wa viongozi wa chadema, Ila pia ni daktari. Ali-tweet jambo kuhusu serikali, ndio akakamatwa kwa uchochezi.
Asante mkuu tweet yake ilisemaje ? Ndio namsikia Leo huyu mtu.
 
Kuna wat weng san wamekamatwa ila wanaopewa attention sana n wale maaruf na wale viongoz wa chama Basi, Tena hata wao wakitoka kweny matatzo hawashughuliki na wanachama walio kamatwa.

Mfano mzur n walinz wa mbowe wale jamaa wamekamatwa siku nyng sana lakn hakuna aliejaribu kupiga kelele kuhusu suala lao hata Mbowe mwenyewe alikausha kama hamna kilicho tokea yan pona yao n hiv Mbowe kakamtwa na wao ndo wanatajwatajwa la svyo wangeozea huko

Kma siyo maaruf huna jina ukipata janga la kisiasa utateseka peke yako na familia yako
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom