Kuporomoka Hadhi ya Tanzania kwenye Diplomasia ya Kimataifa: Awamu ya 5 Imetuangusha

Stuxnet

JF-Expert Member
Feb 12, 2011
10,233
17,457
Haya matukio yanaonyesha kuporomoka kwa hadhi ya Ki-diplomasia kwa Tanzania.

1. Tanzania imekaa bila Balozi kamili wa USA kuanzia Oktoba 2016 alipoondoka Mark Bradley hadi Novemba 2019 alipoteuliwa Dr Don Wright. Kwa miaka 3 tulikuwa unafanya kazi na Inmi Patterson ambaye kicheo ni Charge D'affaire.

2. EU ilimuita nyumbani Mkurugenzi wake wa Tanzania Roeland van De Geer mnamo Novemba 2018, ilikuwa mwaka mzima hadi ilipomteua Manfredo Fanti kujaza nafasi hiyo.

3. Waziri wa Mambo ya Nje (Secret of State) wa USA Mike Pompeo amekwishaanza kutoa majina ya watu wasioruhusiwa kwenda USA. Ameanza na Paul Makonda kutokana na rekodi yake mbaya kwenye kunyang'anya haki ya kuishi ya Watanzania wengine, kudhibiti upinzani, kukandamiza uhuru wa kujieleza nk

4. Donald Trump ameitaja Tanzania pamoja na Kirgystan, Eritrea, Nigeria na Sudan kati ya nchi ambazo wananchi wake hawatoshiriki green card lottery na watadhibitiwa wanapoingia USA

5. Taasisi zisizo za Kiserikali za Amnesty International, Transparency International na Human Rights Watch zimeiorodhesha Tanzania kama nchi ambayo imeporomoka katika usimamiaji wa haki za Binadamu na Ufisadi. Kwa mfano Transparency International inaiorodhesha Tanzania kama nchi ya 99 katika nchi 180 kwenye corruption Index

6. Mashirika ya misaada ya kimataifa kama WB, EU, USAID, SIDA wamekuwa yakisita au yakipunguza msaada ya Maendeleo kwa Tanzania

Hayo sita ni machache kati ya mengi ambayo yanaifanya nchi yetu ambayo ilikuwa ni Tegemeo kwa amani na utulivu wa eneo la maziwa makuu ionekane nchi ya kawaida tu kama Burundi au Malawi. Toka tupate Uhuru mwaka 1961 Tanzania iliheshimika sana katika duru za diplomasia ya kimataifa kutokana na juhudi za Baba wa Taifa Mwl Nyerere na Marais wote 3 waliomfuata. Hali ilivyo kwa kipindi cha JPM siyo nzuri kabisa na siyo jambo la kuacha lipite hivi hivi.

*SULUHISHO*
Tufanye mabadiliko uchaguzi wa 2020, twende na Bernard Camilius Membe iwe ndani ya CCM au Upinzani.
 
Athari zipo hata kwenye sekta ya Afya. Miradi mingi ambayo ilikuwa inafadhiliwa na UNFPA, USAID, PEPFAR iko kwenye "standstill". Haijafutwa bali wanajiuluza kama kweli tunastahili?
 
Hata ile lugha kuwa tanzania ni kisiwa cha amani sikuhizi haiongelewi tena. Si kwa mwana ccm wala mpinzani wote wanaugulia ndani kwa ndani
 
Wewe sisi sio watu wakujipendekeza kwa hao mabeberu aka mabwana zenu, hii nchi ni tajiri na ina uwezo wa Kujitegemea, make Tanzania great again..
 
Sasa kama bado tupo vizuri kwenye ufisadi,hizo kelele tunazosikia toka Lumumba kwamba magufuli anapambana na ufisadi,ni ufisadi gani huo anapambana nao?
Kwa mapambano ya ufisadi ni uwongo mtupu. Wafisadi aliokuwa anapanga kuwaundia Mahakama ya Mafisadi hajawagusa na as such hata Mahakama yenyewe imekuwa "IRREREVANT".

Sana sana wale anaowachukua kwa sababu mbali mbali ametupa rumande bila dhamana kwa miaka 4 sawa kwa makosa ya kutakatisha fedha. Wakati huo huo DPP anasema upelelezi haijakamikika.
 
Siongezi "MSHAHARA" kwa watumishi wowote, mimi mwenyewe "MSHAHARA" haunitoshi.

Licha ya kodi kuwa maradufu na kubambikizana kodi hovyo hovyo, Trafic na Waendesha Mashtaka wa Serikali kugeuzwa TRA.
Unaweza danganya watu wote na ukasimama na kufoka huku ukionyesha umwamba wako laki kamwe hauwezi idanganya nafsi yako. Haswa pale inapokukumbusha kuwa wewe ni muoga na mwongo ktk hii dunia.
 
Diplomasia ni kitu gani wewe? mbona diplomasia haikutuletea flyover, ndege, mradi wa kinyerezi etc.
 
Haya matukio yanaonyesha kuporomoka kwa hadhi ya Ki-diplomasia kwa Tanzania.

1. Tanzania imekaa bila Balozi kamili wa USA kuanzia Oktoba 2016 alipoondoka Mark Bradley hadi Novemba 2019 alipoteuliwa Dr Don Wright. Kwa miaka 3 tulikuwa unafanya kazi na Inmi Patterson ambaye kicheo ni Charge D'affaire.

2. EU ilimuita nyumbani Mkurugenzi wake wa Tanzania Roeland van De Geer mnamo Novemba 2018, ilikuwa mwaka mzima hadi ilipomteua Manfredo Fanti kujaza nafasi hiyo.

3. Waziri wa Mambo ya Nje (Secret of State) wa USA Mike Pompeo amekwishaanza kutoa majina ya watu wasioruhusiwa kwenda USA. Ameanza na Paul Makonda kutokana na rekodi yake mbaya kwenye kunyang'anya haki ya kuishi ya Watanzania wengine, kudhibiti upinzani, kukandamiza uhuru wa kujieleza nk

4. Donald Trump ameitaja Tanzania pamoja na Kirgystan, Eritrea, Nigeria na Sudan kati ya nchi ambazo wananchi wake hawatoshiriki green card lottery na watadhibitiwa wanapoingia USA

5. Taasisi zisizo za Kiserikali za Amnesty International, Transparency International na Human Rights Watch zimeiorodhesha Tanzania kama nchi ambayo imeporomoka katika usimamiaji wa haki za Binadamu na Ufisadi. Kwa mfano Transparency International inaiorodhesha Tanzania kama nchi ya 99 katika nchi 180 kwenye corruption Index

6. Mashirika ya misaada ya kimataifa kama WB, EU, USAID, SIDA wamekuwa yakisita au yakipunguza msaada ya Maendeleo kwa Tanzania

Hayo sita ni machache kati ya mengi ambayo yanaifanya nchi yetu ambayo ilikuwa ni Tegemeo kwa amani na utulivu wa eneo la maziwa makuu ionekane nchi ya kawaida tu kama Burundi au Malawi. Toka tupate Uhuru mwaka 1961 Tanzania iliheshimika sana katika duru za diplomasia ya kimataifa kutokana na juhudi za Baba wa Taifa Mwl Nyerere na Marais wote 3 waliomfuata. Hali ilivyo kwa kipindi cha JPM siyo nzuri kabisa na siyo jambo la kuacha lipite hivi hivi.

*SULUHISHO*
Tufanye mabadiliko uchaguzi wa 2020, twende na Bernard Camilius Membe iwe ndani ya CCM au Upinzani.
Naunga mkono hoja..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mapambano ya ufisadi ni uwongo mtupu. Wafisadi aliokuwa anapanga kuwaundia Mahakama ya Mafisadi hajawagusa na as such hata Mahakama yenyewe imekuwa "IREREVANT".

Sana sana wale anaowachukua kwa sababu mbali mbali ametupa rumande bila dhamana kwa miaka 4 sawa kwa makosa ya kutakatisha fedha. Wakati huo huo DPP anasema upelelezi haijakamikika.
Na kumfyekelea mbali Prof ASSAD CAG ili ufisadi anaopambana kuutamarakisha Tanzania usijulikane kwa wanyonge
 
Na kumfyekelea mbali Prof ASSAD CAG ili ufisadi anaopambana kuutamarakisha Tanzania usijulikane kwa wanyonge
Kuna mkataba wa Open Government Partneship (OGP) ambao nchi 78 zilizo chini ya UN ziliridhia na Tanzania ikiwa mojawapo. Mkataba huu ulikuwa una husu utendaji kazi wa Serikali kwa uwazi. Nanukuu vision yake kwa kiingereza;

"OGP’s vision is that more governments become sustainably more transparent, more accountable, and more responsive to their own citizens, with the ultimate goal of improving the quality of governance, as well as the quality of services that citizens receive"

Lakini mwaka 2016, Serikali ya Awamu ya 5 ilijitoa kwenye huu mkataba wa utendaji kazi kwa uwazi. Jiuluze kwa nini tunaficha mambo yetu kama ni mazuri??

Ni wachawi to ndiyo hufanya shughuli zao gizani.
 
Kuna mkataba wa Open Government Partneship (OGP) ambao nchi 78 zilizo chini ya UN ziliridhia na Tanzania ikiwa mojawapo. Mkataba huu ulikuwa una husu utendaji kazi wa Serikali kwa uwazi. Nanukuu vision yake kwa kiingereza;

"OGP’s vision is that more governments become sustainably more transparent, more accountable, and more responsive to their own citizens, with the ultimate goal of improving the quality of governance, as well as the quality of services that citizens receive"

Lakini mwaka 2016, Serikali ya Awamu ya 5 ilijitoa kwenye huu mkataba wa utendaji kazi kwa uwazi. Jiuluze kwa nini tunaficha mambo yetu kama ni mazuri??

Ni wachawi to ndiyo hufanya shughuli zao gizani.
Sasa wanao msifu na kumwabudu magufuli wanafanya hivyo kwa sababu zipi?Kujitoa kwenye mkataba wa aina hii ni dalili kwamba tuna serikali ya hovyo na iliyojaa wezi
 
Back
Top Bottom