Kupona kwa Lissu: Mchango wa Mange Kimambi na Wema Sepetu hautosahaulika

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,439
50,957
Sote ni binadamu, tuna mapungufu yetu lakini tuna mazuri yetu mengi

Huwezi kulitaja suala la kushambuliwa Lissu na mobilization ya Umma katika kujaribu kunusuru maisha ya Lissu bila kuwataja madada wawili, Mange Kimambi na Wema Sepetu.

Mange alitumia ushawishi wake mkubwa kuhimiza michango kwa ajili ya Lissu, binafisi nilichanga hela ndefu tu

Pia huwezi kumsahau mwanadada Wema Sepetu katika kumobilize michango kwa ajili ya Lissu

Kwa hakika nyinyi madada kuna wakati mlichukua responsibility kubwa sana kwa ajili ya kulitetea Taifa hili. Kwa hakika mchango wenu katika point ile ya wakati haitosahaulika!. Mlikuwa wanawake wa shoka kwelikweli!

Mlisimama pale wanaume wengi waliposhindwa
Mliweka pembeni muda wenu halali wa kujali mambo ya ulimbwende, mkasimama kulitaka Taifa liwe bora, la haki, uhuru. Na kwa hakika mlitimiza wajibu wenu

Pamoja na hali iliyowakumba sasa ya dissapointment, kujiweka mbali na struggle lakini kwa kuwa nyinyi ni mabinti wa Kiislamu na Mtume wenu alifundisha kuwa ukiona udhalimu uondoe kwa mkono wako, Kama huwezi Ukemee kwa kauli zako, na kama ukishindwa basi Chukia udhalimu huo japokuwa kuchukia bila action ni udhaifu wa kiimani! basi nawaomba huko mliko katika ukimya wenu muendeleze struggle kadri mtakavyoweza!. Udhalimu huwa hauishi kwa jaribio moja, struggle ya muda mfupi , kiufupi mtu anayeamini katika struggle inabidi mtu aendelee kustruggle hata kama amebaki yeye peke yake na wengine wote hawamuelewi.

Mwisho kabisa niseme tu
Nyie madada wawili, Asanteni sana kwa kazi ile mliyoifanya ya kusaidia kuokoa maisha ya Raisi ajaye ndugu Tundu Antipas Lissu

Pia namshauri ndugu Lissu kuendelea kuwashukuru madada hawa wawili regardless mitizamo yao ya kisiasa ya sasa au lifestyle waliyochagua!. Hawa ni maaskari wa miavuli waliokupigania kwa medani iliyotukuka!
 
Sote ni binadamu, tuna mapungufu yetu lakini tuna mazuri yetu mengi

Huwezi kulitaja suala la kushambuliwa Lissu na mobilization ya Umma katika kujaribu kunusuru maisha ya Lissu bila kuwataja madada wawili, Mange Kimambi na Wema Sepetu.

Mange alitumia ushawishi wake mkubwa kuhimiza michango kwa ajili ya Lissu, binafisi nilichanga hela ndefu tu

Pia huwezi kumsahau mwanadada Wema Sepetu katika kumobilize michango kwa ajili ya Lissu

Kwa hakika nyinyi madada kuna wakati mlichukua responsibility kubwa sana kwa ajili ya kulitetea Taifa hili. Kwa hakika mchango wenu katika point ile ya wakati haitosahaulika!. Mlikuwa wanawake wa shoka kwelikweli!

Mlisimama pale wanaume wengi waliposhindwa
Mliweka pembeni muda wenu halali wa kujali mambo ya ulimbwende, mkasimama kulitaka Taifa liwe bora, la haki, uhuru. Na kwa hakika mlitimiza wajibu wenu

Pamoja na hali iliyowakumba sasa ya dissapointment, kujiweka mbali na struggle lakini kwa kuwa nyinyi ni mabinti wa Kiislamu na Mtume wenu alifundisha kuwa ukiona udhalimu uondoe kwa mkono wako, Kama huwezi Ukemee kwa kauli zako, na kama ukishindwa basi Chukia udhalimu huo japokuwa kuchukia bila action ni udhaifu wa kiimani! basi nawaomba huko mliko katika ukimya wenu muendeleze struggle kadri mtakavyoweza!. Udhalimu huwa hauishi kwa jaribio moja, struggle ya muda mfupi , kiufupi mtu anayeamini katika struggle inabidi mtu aendelee kustruggle hata kama amebaki yeye peke yake na wengine wote hawamuelewi.

Mwisho kabisa niseme tu
Nyie madada wawili, Asanteni sana kwa kazi ile mliyoifanya ya kusaidia kuokoa maisha ya Raisi ajaye ndugu Tundu Antipas Lissu

Pia namshauri ndugu Lissu kuendelea kuwashukuru madada hawa wawili regardless mitizamo yao ya kisiasa ya sasa au lifestyle waliyochagua!. Hawa ni maaskari wa miavuli waliokupigania kwa medani iliyotukuka!
Rais ajaye!!!! Kua serious mtoa mada, RAIS AJAYE!!
Hta belize tu hawampi uprime minister mtu kiutani hivi.
Urais ni mada beyond your imagination,kwingine nahis ipo sawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa wameshaamini wazungu watawasaidia waingie Ikulu, ha ha ha.

Mchonga mwenyewe aliomba msaada kwa mzungu ili asipinduliwe mwaka 1964.
Kama siyo jeshi la mkoloni kuja kuwatuliza akina kamanda Ilogi wa Cirrito baracks mchonga angekuwa byebye toka 1964.

Sasa kama Mchonga mwenyewe alimlilia mzungu amlinde asing'olewe na waafrika wenzie "wakorofi" ni nini cha ajabu Wazalendo wa leo kuwasemea waonevu katika nyakati hizi kwa mzungu huyohuyo?
 
Nachukua nafasi hii kuwashukuru wote walijitolea kwa hali na mali kuchangia matibabu ya Lissu , Mungu awazidishie
 
Ndiyo ukweli huo, kwani wewe hujui mchonga alimuomba mzungu aulinde utawala wake mwaka 1964?
Kwanza sio cirito barracks bali Colito Barracks (ilipo Lugalo kwa sasa). Tatizo unafikiri unaongea na mtoto mwenzako. Kama ndio hiyo si uende kuomba kazi ya ushambaboy kwa hao wazungu basi?
 
Kwanza sio cirito barracks bali Colito Barracks (ilipo Lugalo kwa sasa). Tatizo unafikiri unaongea na mtoto mwenzako. Kama ndio hiyo si uende kuomba kazi ya ushambaboy kwa wazungu basi?

Good! kumbe unajua hiyo issue!
Basi ndo hivyo, Beberu, mkoloni, Mzungu alinusuru utawala wa mwasisi!.
Hii ikuonyeshe kuwa siyo wakati wote Mzungu anakuwa na Hiyana!

Usikariri!!
 
Good! kumbe unajua hiyo issue!...
Sio tu kwamba naijua. Nimeshudia hayo majaribio, kwani nilikua darasa la tano shule ya Wailesi (Wireless Temeke) wakati huo. Kama unawahusudu sana wazungu nenda kawaombe kazi ya ushambaboy wakuajiri ufurahishe roho yako. Inaonekana unapenda sana kujikomba kwao.
 
Sio tu kwamba naijua. Nimeshudia hayo majaribio, kwani nilikua darasa la tano shule ya Wailesi (Wireless Temeke) wakati huo. Kama unawahusudu sana wazungu nenda kawaombe kazi ya ushambaboy wakuajiri ufurahishe roho yako. Inaonekana unapenda sana kujikomba kwao.

Unadhani kwa nini mchonga alienda kuomba msaada wa Mzungu ili asiondolewe madarakani?
 
Mchango wao ni kiasi gani in T.shs? Kama hujui basi wewe ni nothing but a drama queen seeking attention not unlike the shitty female personalities you so much admire.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom