Kupitia kwa ‘Baraka ‘ za Vyeo ‘ Mfululizo ‘ alivyopata kwa muda mfupi Afande Charles Mbuge tunajifunza yafuatayo

Tupeni hivyo visa alivyokuwa anafanyiwa
Ukidharauliwa na Mabosi wako na Wafanyakazi wenzako usiumie wala kusikitika.
Ukinyanyasika na Mabosi / Wakubwa wako usihuzunike wala usikate tama.
Hata kama Mabosi / Wakubwa watakuchukia Wewe tekeleza tu Majukumu yako Kiufanisi
Unaweza ukachukiwa na wengi ( hasa Mabosi / Wakubwa wako ) ila Mwenyezi Mungu atambariki Mtu Mmoja ambaye hukumtegemea na atakuwa ndiyo Mkombozi wako na atakuinua na kukufanya uwe Binadamu kamili katika Watu.
Uvumilivu unalipa japo unaweza ukayapata hayo Malipo yako kwa Kuchelewa.
Kama ipo ipo tu hata kama Mabosi / Wakubwa wako watakuwa mara kwa mara kwa Chuki zao tu wanakuandikia Ripoti mbaya.
Kusali sana na Kujikabidhi kwa Mwenyezi Mungu ni jambo la muhimu mno katika Maisha ya sasa ya Mwanadamu ambayo yamejaa Chuki, Wivu, Majungu na Fitina.

Kwa tuliobahatika kidogo Kuyasikia mambo aliyokuwa akifanyiwa huyu Brigedia Jenerali ambaye naamini sasa atakuwa ni Meja Jenerali na Wakubwa zake hasa alipokuwa Mlalakuwa miaka ya nyuma na kwa Majungu tu ya baadhi wakaamua Kumuondoa hapo na Kumtupa kabisa Ruvu acheni tu Afande Charles Mbuge sasa ‘ atambe ‘ na Yeye ale Bata.

Ama hakika Mungu ni Mwema.
 
Tupeni hivyo visa alivyokuwa anafanyiwa

Kuna ' Mpuuzi ' Mwenzako mmoja hivi aliniuliza Swali kama hili na nikamjibu hivyo nakuomba itafute ' post ' niliyomjibu na acha Kunipotezea muda tafadhali.
 
Mpaka umesoma Uzi wote huu na ukaamua Kuujibu hivi ina maanisha kuwa hiyo ' point ' ya Msingi umeshaielewa labda tu uwe na Akili za ' Kipa Katoka ' ndiyo unaweza usielewe.
Ofcz nimeelewa sana lakin nilipenda uweka taarifa za zaid mfano history ya utendaji wake toka alipoanzia pia vikwazo na hizo figisu ambazo amefanyiwa na wenzake.Alama za utendaji kaz wake aliouacha katika placement mbali mbal alipopita n.k n.k
 
Nyepesi nyepesi ni kwamba anaandaliwa kuchukua nafasi ya mabeyo..

Wewe Jamaa una Akili Kubwa sijapata Kuona. Ulichokisema ndiyo sahihi kabisa Ndugu na nimedokezwa pia kuwa kumbe hata aliyempendekeza awe anapandishwa Vyeo kwakuwa anamkubali ni huyu huyu Bosi wake Mkuu wa sasa japo kuna zingine za chini kwa chini ambazo naendelea Kuzithibitisha Kiumakini zinasema kuwa Watu wa Idara Nyeti ndani ya hiyo Taasisi yenye dhamana kubwa ya Usingizi na Ustawi wetu hadi Mipakani kwa Kila Siku ilifanya Uchunguzi wake na ikagundua ya kwamba Bosi wa sasa hakubaliki kabisa karibia na 85% ya Watendaji wake ( japo Bosi Mkuu kabisa Kikatiba nchini ) anamkubali na ukizingatia kuwa wanatokea Ukanda mmoja na wanazungumza Lugha moja. Hivyo umetolewa Ushauri kuwa abadilishwe haraka au abakishwe hadi muda wake wa Kustaafu utakapofika lakini hapa katikati atafutwe Mtu ambaye ataweza Kutuliza ' Munkari ' ya Watendaji hao na ambaye pia anakubalika nao kwa 99% na ndiyo maana ameanza taratibu Kumpandisha Vyeo ili aanze Kuzoea na Kuyajua mengi kisha muda ukifika anampandisha kuwa Boss Kamili. Uko vizuri Ndugu heko.
 
Amiri Jeshi Mkuu alipompandisha Cheo mwaka huu nilifurahi mno na baada ya leo tena kusikia amekuwa Boss mpya wa JKT ndiyo nimefurahi sana tu Ndugu. Mimi sijapita huko katika Umedani / Jeshini ila kwa Maelezo ya Watu ' Waandamizi ' kama Watatu hivi waliokuwa nae Kikazi / Kimajukumu waliwahi kuniambia kuwa Jamaa ( Afande ) alikuwa akinyanyasika na hata akidharaulika mno na Wakubwa hasa hasa ile Awamu iliyopita kiasi kwamba hata wana Medani wengine wakawa wanaumia kuona Jamaa akifanyiwa Mtima Nyongo huo.

Nina uhakika tokea Siku ile alivyopandishwa Cheo na Rais JPM na hivi leo tena amekuwa Boss wa JKT wale ' Maadui ' zake Wakuu Kikazi ambapo kati yao 75% wameshastaafu Kazi ila 25% bado wapo ingawaje nao Kustaafu Kwao hakuko mbali kutoka sasa naamini Baraka hizi na Afande Charles Mbuge Kupandishwa Cheo kunaweza kuwafanya ama wakose Usingizi au na Wao sasa wakajiandaa Kumpigia Simu za Kumuomba Msamaha kama ulivyokuwa Utaratibu wa hivi karibuni wa Watanzania au hata Maadui zake wengine kuomba ' appointment ' nae pale Mlalakuwa au Dodoma ili wakamuombe Msamaha ' mubashara ' kabisa.

Acheni Mungu aitwe Mungu tu Ndugu zangu na hapa duniani kamwe tusidharauliane wala tusikomoane kwani huwezi jua Kesho huyu unayemfanyia hivyo Mwenyezi Mungu atambariki na kumfanya awe nani hapo Kazini au katika Eneo fulani ambapo unaweza nawe ukajikuta unaumbuka na unaona hata Aibu kama hata si kutamani Ardhi ipasuke kabisa utokomee nayo.
Hizo fitina na figisu alizofanyiwa na hao wakubwa wake ni zipi?
Kwa mnaomjua na kufanya nae kazi tupeni CV yake
 
Ofcz nimeelewa sana lakin nilipenda uweka taarifa za zaid mfano history ya utendaji wake toka alipoanzia pia vikwazo na hizo figisu ambazo amefanyiwa na wenzake.Alama za utendaji kaz wake aliouacha katika placement mbali mbal alipopita n.k n.k

Narudia tena Kusisitiza Kwako kuwa acha Kunipotezea muda na Kunisumbua tafadhali. Naona Watu wa ' Kitengo ' hapo Upanga / Dodoma wamekupa Kazi hapo unichokonoe / unidadisi / unipeleleze ili nifunguke zaidi lakini nakuhakikishia hakuna utakachokipata kutoka Kwangu ila tambueni tu ya kwamba Afande Charles Mbuge ndiyo ameshaukata / ameshaula hivyo. Najua wengi wenu mnaumia sana hapo baada ya kuona Jamaa kila mara JPM anampandisha tu Vyeo wakati nyie hapo enzi zenu mlikuwa mnampuuza, mnamchukia na hata kumdharau. Sasa ndiyo anaenda kuwa Boss wenu Mkuu kabisa Siku si nyingi. Mtakoma na Kupasuka kwa Kununa.
 
Upuuzi wa kiwango cha lami
Wewe Jamaa una Akili Kubwa sijapata Kuona. Ulichokisema ndiyo sahihi kabisa Ndugu na nimedokezwa pia kuwa kumbe hata aliyempendekeza awe anapandishwa Vyeo kwakuwa anamkubali ni huyu huyu Bosi wake Mkuu wa sasa japo kuna zingine za chini kwa chini ambazo naendelea Kuzithibitisha Kiumakini zinasema kuwa Watu wa Idara Nyeti ndani ya hiyo Taasisi yenye dhamana kubwa ya Usingizi na Ustawi wetu hadi Mipakani kwa Kila Siku ilifanya Uchunguzi wake na ikagundua ya kwamba Bosi wa sasa hakubaliki kabisa karibia na 85% ya Watendaji wake ( japo Bosi Mkuu kabisa Kikatiba nchini ) anamkubali na ukizingatia kuwa wanatokea Ukanda mmoja na wanazungumza Lugha moja. Hivyo umetolewa Ushauri kuwa abadilishwe haraka au abakishwe hadi muda wake wa Kustaafu utakapofika lakini hapa katikati atafutwe Mtu ambaye ataweza Kutuliza ' Munkari ' ya Watendaji hao na ambaye pia anakubalika nao kwa 99% na ndiyo maana ameanza taratibu Kumpandisha Vyeo ili aanze Kuzoea na Kuyajua mengi kisha muda ukifika anampandisha kuwa Boss Kamili. Uko vizuri Ndugu heko.
 
Nipo kwenye system muda mrefu

Haya si mambo ya kujitapa hapa

Hata Mimi najua uko huko muda mwingi Ndugu. Vipi hakuna nafasi huko ili unipigie pande na Mimi hata niwe Muosha Magari au Mzururaji wa Majalalani Kutwa tu Ndugu? Nisalimie sana wana ' System ' wenzako hapo Ndugu. Mkeo pale Ubalozini huwa ana hisa napo au kuna Mchongo huwa anaufanya Ndugu? Dar es Salaam Kwetu huku unatutimbia lini Ndugu? Nakukubali mno Mzee wa System.
 
From chief staff to CDF wewe ni raia mkongwe nakuuuza
CV yake Kuu ni kwamba hapo JKT atakaa kwa muda mfupi tu kisha anaweza Kuteuliwa tena kuwa Chief of Staff muda si mrefu kutoka sasa au akateuliwa moja kwa moja kuwa CDF.
 
Unajua maana ya Xenophobia? Na je ulipolitumia katika haya maelezo yako unadhani lilistahili Kutumika au labda kwakuwa una matatizo yako Sugu ya Kutokujua vyema Lugha ya Kiingereza ndiyo ukaamua ulitumie ili mradi tu kila Member wa JF ajue kuwa na Wewe umeenda Shule halafu unayajua yanayoendelea huko Afrika Kusini?
Nimetumia kama chagizo tu.....
na sio kwamba nimeonyesha msuli wa shule.....
don't feel offended....
 
Kwani lazima? Na kwanini unaonekana Kuteseka sana na Mafanikio ya ghafla na Kuinuliwa Kimamlaka kwa Afande Charles Mbuge Ndugu? au na Wewe ndiyo wale wale mliokuwa mkinyanyasa Baba wa Watu Kipindi kile alipokuwa pale Mlalakuwa na hadi alivyohamishiwa Ruvu? Basi kwa sasa ndiyo mtamkoma na Mwenyezi Mungu anawaumbueni hapa hapa kwa Kumuinua na nyie Kubakia hapo hapo. Tubuni upesi na muanze Kujipanga Kupanga Mistari ya kwenda Kumuomba Msamaha. Mna bahati Baba wa Watu huwa hana Malipizi ( Visasi ) ila hili ' Zali ' ndiyo lingenikuta Mimi ' Maadui ' zangu wote mngenikoma na ndipo mngejua ni kwanini Wimbo wa Taifa hadi leo hauna Video na kwanini Nyoka hana Ugoko.
nawatakoma kweli
 
Charles Mbuge juhudi zake zimechangia kufika hapo alipo jamaa ni mtu peace sana,
Nadhani kwao ni watu makini sana Mwaka flan nilifanya kibarua katika kampuni ya ujenzi iliyokuwa na ufungamano na jeshi na moja ya ma_boss wakuu alikuwapo Johannes Mbuge ambaye ni kaka wa damu wa huyu Charles,Johannes alikuwa mtu makini sana kias kwamba hata jeshi walitaka wamchukue kama muajiliwa wao....
 
Hadi jehini kuna kuoneana wivu hayo si mambo ya kinamama uswahilini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom