Kupitia kwa ‘Baraka ‘ za Vyeo ‘ Mfululizo ‘ alivyopata kwa muda mfupi Afande Charles Mbuge tunajifunza yafuatayo

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,054
107,538
Ukidharauliwa na Mabosi wako na Wafanyakazi wenzako usiumie wala kusikitika.
Ukinyanyasika na Mabosi / Wakubwa wako usihuzunike wala usikate tama.
Hata kama Mabosi / Wakubwa watakuchukia Wewe tekeleza tu Majukumu yako Kiufanisi
Unaweza ukachukiwa na wengi ( hasa Mabosi / Wakubwa wako ) ila Mwenyezi Mungu atambariki Mtu Mmoja ambaye hukumtegemea na atakuwa ndiyo Mkombozi wako na atakuinua na kukufanya uwe Binadamu kamili katika Watu.
Uvumilivu unalipa japo unaweza ukayapata hayo Malipo yako kwa Kuchelewa.
Kama ipo ipo tu hata kama Mabosi / Wakubwa wako watakuwa mara kwa mara kwa Chuki zao tu wanakuandikia Ripoti mbaya.
Kusali sana na Kujikabidhi kwa Mwenyezi Mungu ni jambo la muhimu mno katika Maisha ya sasa ya Mwanadamu ambayo yamejaa Chuki, Wivu, Majungu na Fitina.

Kwa tuliobahatika kidogo Kuyasikia mambo aliyokuwa akifanyiwa huyu Brigedia Jenerali ambaye naamini sasa atakuwa ni Meja Jenerali na Wakubwa zake hasa alipokuwa Mlalakuwa miaka ya nyuma na kwa Majungu tu ya baadhi wakaamua Kumuondoa hapo na Kumtupa kabisa Ruvu acheni tu Afande Charles Mbuge sasa ‘ atambe ‘ na Yeye ale Bata.

Ama hakika Mungu ni Mwema.
 
Amina Amina.

Mwenyezi Mungu akikupangia Jambo lako litakuwa tu hata kama kuna Watu wanakuchukia, wanakusambazia maneno mabaya, wanakuzushia, wanakuchafua na hata wengine wanaweza wakawa wanataka Kukuua kwakuwa wanakuona Wewe ni Tishio Kwao ama kwa huo muda au kwa baadae kupitia Nafasi zao ( Vyeo vyao )

Na huyu Afande nahisi Mwenyezi Mungu anazidi Kumfungulia njia za Mafanikio na Kumpa Baraka nyingi kwakuwa huwa hajui Kulipiza Kisasi bali humuachia kila Kitu Mola / Maulana. Na alivyo Muungwana kila alipokuwa akipangiwa kwenda Kufanya Kazi zake ( Kituo cha Kazi ) kama njia ya ' Kumkomoa ' ndiyo Kwanza alikuwa hakatai, anaonyesha Ushirikiano na huko atakapokuwa alikuwa akichapa Kazi hata kuliko pale alipokuwepo awali.

Maisha ya Kikazi / Kimajukumu ya Afande Charles Mbuge yawe ni Somo Kwetu hasa huko sehemu zetu za Kujipatia Riziki.
 
Hard work pays off! Congrats kamanda!

Amiri Jeshi Mkuu alipompandisha Cheo mwaka huu nilifurahi mno na baada ya leo tena kusikia amekuwa Boss mpya wa JKT ndiyo nimefurahi sana tu Ndugu. Mimi sijapita huko katika Umedani / Jeshini ila kwa Maelezo ya Watu ' Waandamizi ' kama Watatu hivi waliokuwa nae Kikazi / Kimajukumu waliwahi kuniambia kuwa Jamaa ( Afande ) alikuwa akinyanyasika na hata akidharaulika mno na Wakubwa hasa hasa ile Awamu iliyopita kiasi kwamba hata wana Medani wengine wakawa wanaumia kuona Jamaa akifanyiwa Mtima Nyongo huo.

Nina uhakika tokea Siku ile alivyopandishwa Cheo na Rais JPM na hivi leo tena amekuwa Boss wa JKT wale ' Maadui ' zake Wakuu Kikazi ambapo kati yao 75% wameshastaafu Kazi ila 25% bado wapo ingawaje nao Kustaafu Kwao hakuko mbali kutoka sasa naamini Baraka hizi na Afande Charles Mbuge Kupandishwa Cheo kunaweza kuwafanya ama wakose Usingizi au na Wao sasa wakajiandaa Kumpigia Simu za Kumuomba Msamaha kama ulivyokuwa Utaratibu wa hivi karibuni wa Watanzania au hata Maadui zake wengine kuomba ' appointment ' nae pale Mlalakuwa au Dodoma ili wakamuombe Msamaha ' mubashara ' kabisa.

Acheni Mungu aitwe Mungu tu Ndugu zangu na hapa duniani kamwe tusidharauliane wala tusikomoane kwani huwezi jua Kesho huyu unayemfanyia hivyo Mwenyezi Mungu atambariki na kumfanya awe nani hapo Kazini au katika Eneo fulani ambapo unaweza nawe ukajikuta unaumbuka na unaona hata Aibu kama hata si kutamani Ardhi ipasuke kabisa utokomee nayo.
 
Bado kuna kizazi cha wapumbavu wanaoamini katika upigaji.
Nchi hii ilifika mahali ukiwa mchapa kazi na muadilifu unaundiwa zengwe na kupotezwa
Hilo kundi ni kubwa mno na linahaha sasa hivi, waliokubali kubadilika wanaishi kwa hofu ya waliyoyafanya huko nyuma.
Tunapoona wachapakazi wakiinuliwa hakika ni faraja kwa wazalendo lakini ni pigo kubwa kwa wapiga dili.
Hongera Brigedia Mbuge.
 
Hizo fitina na figisu alizofanyiwa na hao wakubwa wake ni zipi?

Naongozwa na Maadili na sijawa na Akili za ' Kipa Katoka ' halafu nikaziweka hapa ila naamini wale wote waliowahi kuwa nae Afande hasa pale Mlalakuwa watakuwa wananielewa vyema tu kile ninachokimaanisha kwani ilifikia muda hadi Watu wengine walikuwa wakiona jinsi Mpiganaji huyu alivyokuwa akinyanyasika kwakuwa tu hakuwa Mnafiki, mpenda Kujipendekeza, hakuwa Muoga na alikuwa akitekekeleza vyema Majukumu yake na sishangai ndiyo maana Askari wengi wanampenda na anakubalika mno hadi sasa huyu Afande Charles Mbuge japo amepitia Mitihani mingi mno tu.

Ama kweli Mungu ni mkubwa na akilipanga lake linakuwa tu hata kama Walimwengu watalichelewesha.
 
Ukidharauliwa na Mabosi wako na Wafanyakazi wenzako usiumie wala kusikitika.
Ukinyanyasika na Mabosi / Wakubwa wako usihuzunike wala usikate tama.
Hata kama Mabosi / Wakubwa watakuchukia Wewe tekeleza tu Majukumu yako Kiufanisi
Unaweza ukachukiwa na wengi ( hasa Mabosi / Wakubwa wako ) ila Mwenyezi Mungu atambariki Mtu Mmoja ambaye hukumtegemea na atakuwa ndiyo Mkombozi wako na atakuinua na kukufanya uwe Binadamu kamili katika Watu.
Uvumilivu unalipa japo unaweza ukayapata hayo Malipo yako kwa Kuchelewa.
Kama ipo ipo tu hata kama Mabosi / Wakubwa wako watakuwa mara kwa mara kwa Chuki zao tu wanakuandikia Ripoti mbaya.
Kusali sana na Kujikabidhi kwa Mwenyezi Mungu ni jambo la muhimu mno katika Maisha ya sasa ya Mwanadamu ambayo yamejaa Chuki, Wivu, Majungu na Fitina.

Kwa tuliobahatika kidogo Kuyasikia mambo aliyokuwa akifanyiwa huyu Brigedia Jenerali ambaye naamini sasa atakuwa ni Meja Jenerali na Wakubwa zake hasa alipokuwa Mlalakuwa miaka ya nyuma na kwa Majungu tu ya baadhi wakaamua Kumuondoa hapo na Kumtupa kabisa Ruvu acheni tu Afande Charles Mbuge sasa ‘ atambe ‘ na Yeye ale Bata.

Ama hakika Mungu ni Mwema.
Sort of MAJUNGU


kunyanyasika
kudharauliwa
kuchukiwa... na nani?

Weka hapa hizo chuki , majungu na dharau,,,


Ukishindwa,, basi nakwambia "ACHA MAJUNGU"
 
Sort of MAJUNGU


kunyanyasika
kudharauliwa
kuchukiwa... na nani?

Weka hapa hizo chuki , majungu na dharau,,,


Ukishindwa,, basi nakwambia "ACHA MAJUNGU"

Kwani lazima? Na kwanini unaonekana Kuteseka sana na Mafanikio ya ghafla na Kuinuliwa Kimamlaka kwa Afande Charles Mbuge Ndugu? au na Wewe ndiyo wale wale mliokuwa mkinyanyasa Baba wa Watu Kipindi kile alipokuwa pale Mlalakuwa na hadi alivyohamishiwa Ruvu? Basi kwa sasa ndiyo mtamkoma na Mwenyezi Mungu anawaumbueni hapa hapa kwa Kumuinua na nyie Kubakia hapo hapo. Tubuni upesi na muanze Kujipanga Kupanga Mistari ya kwenda Kumuomba Msamaha. Mna bahati Baba wa Watu huwa hana Malipizi ( Visasi ) ila hili ' Zali ' ndiyo lingenikuta Mimi ' Maadui ' zangu wote mngenikoma na ndipo mngejua ni kwanini Wimbo wa Taifa hadi leo hauna Video na kwanini Nyoka hana Ugoko.
 

Similar Discussions

30 Reactions
Reply
Back
Top Bottom