GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,054
- 107,538
Ukidharauliwa na Mabosi wako na Wafanyakazi wenzako usiumie wala kusikitika.
Ukinyanyasika na Mabosi / Wakubwa wako usihuzunike wala usikate tama.
Hata kama Mabosi / Wakubwa watakuchukia Wewe tekeleza tu Majukumu yako Kiufanisi
Unaweza ukachukiwa na wengi ( hasa Mabosi / Wakubwa wako ) ila Mwenyezi Mungu atambariki Mtu Mmoja ambaye hukumtegemea na atakuwa ndiyo Mkombozi wako na atakuinua na kukufanya uwe Binadamu kamili katika Watu.
Uvumilivu unalipa japo unaweza ukayapata hayo Malipo yako kwa Kuchelewa.
Kama ipo ipo tu hata kama Mabosi / Wakubwa wako watakuwa mara kwa mara kwa Chuki zao tu wanakuandikia Ripoti mbaya.
Kusali sana na Kujikabidhi kwa Mwenyezi Mungu ni jambo la muhimu mno katika Maisha ya sasa ya Mwanadamu ambayo yamejaa Chuki, Wivu, Majungu na Fitina.
Kwa tuliobahatika kidogo Kuyasikia mambo aliyokuwa akifanyiwa huyu Brigedia Jenerali ambaye naamini sasa atakuwa ni Meja Jenerali na Wakubwa zake hasa alipokuwa Mlalakuwa miaka ya nyuma na kwa Majungu tu ya baadhi wakaamua Kumuondoa hapo na Kumtupa kabisa Ruvu acheni tu Afande Charles Mbuge sasa ‘ atambe ‘ na Yeye ale Bata.
Ama hakika Mungu ni Mwema.