Kupitia kisa hiki, kama mume ungechukua hatua gani? Wanawake Je huyu mwenzenu yuko sahihi?

2019

JF-Expert Member
Dec 31, 2018
2,982
4,457
Imemtokea mdogo wangu ukoo mmoja saivi anazidi kukonda tu: umri wa wote ni kati ya 21-27.

Alimpenda dada mmoja 2018,mtoto wa kike nae alimpenda pia jamaa akawa serious nae na kutangaza kuishi nae,huyo dada akadai ana mtu mwenye malengo nae(ndoa) ambaye pia wazazi wanamjua.

Basi dogo akampa option binti achague yeye,ataamua yeye au wazazi watamwamulia,bint akaamua yeye lakin wazazi japo hawakuwa na namna bint akaanza kuishi na jamaa.

Baada ya bint kufanya maamuzi dogo alimpenda sana yani kwa jinsi alivyokuwa anatamba kwa vijana na hata mabinti waliomtaka ilionyesha kabisa mapenzi yake kwa binti.

2019 wakapata mtoto,dogo akaweka malengo ya kwenda kwa wazazi (mkoani)kulipa kabisa mahari,kijana alikua muwaz sababu mimi kama mshauri wake hakunificha baadhi ya mambo.

Ikiwa imebak miezi michache kwenda ile pesa(zaidi ya mil1) ikapotea katika mazingira ya kutatanisha,kijana akawa mpole,akaja kuniambia ile pesa nilichukua kuboost biashara ikapote,kwa hiyo safari nasogeza mbele.

Mapicha picha yakaanza ndani, yule binti akadai kaongea na wazazi wake wamelaumu sababu hawaoni faida yake...lait angeendelea kusoma angepata kaz na akawasaidia nyumbani(aliishia form 4 hakufaulu). Kutokana na lawama hizo ikabidi bint abadili mawazo na kutaka kuendelea kusoma ili awatii wazazi wake...lawama kwa wazazi zilikua nyingi sababu pia dogo ana kipato cha wastani walitaka mtoto wao labda aolewe na mwajiriwa serikalini.

Dogo akapambana kumtuliza binti akakataa katu kata na full migogoro ikaanza dharau kutoka kwa bint,wakati wanavutana mtoto abak na nani ndipo dogo akagundua mengi zaidi sababu waendelee kukaa wote japo hawakuwa wakilana matunda.

Kijana akazidi kukonda anawaza mtoto wake atabak na nani,kama akienda atamtunzaje yan mambo mengi.

Dogo siku moja (nimejaribu kuficha siku na muda ili nisitoe codes) dogo akarudi usiku kidogo akasimama dirishani na kusikiliza ndani, binti alikua akiongea na simu, mazungumzo yalikuwa ya ndani kabisa(mambo ya kikubwa) na jamaa mwingine. Alipoingia ndani akamnyanganya simu,kuchungulia alikua akichat na kidume kingine,kuna sms za ile pesa iliyodaiwa kupotea.

Fujo ikatokea sababu ya ile simu binti akamwaibisha sana dogo lakini dogo hakumgusa,akamtolea shit sana mbele za watu kiasi hata majiran wakamwambia sio vizuri. Akampiga kijana lakin dogo hakumgusa. Akarudasha simu na akapewa hifadhi ya kulala kwa jirani.

Bint akafunga vitu asubuhi akasepa zake.

Hitimisho la ile pesa iliyopotea kumbe mwanzo dogo alinidanganya
Ile pesa,ilidaiwa kuja rafiki yake akaichukua sababu kama angemwambia asingempa,kwa hiyo kwa madai ya bint rafikiye aliingia na kuichukua huku akituma ujumbe kuwa atamrudshia.(bint alimwonyesha dogo sms siku ile iliyopotea).

Maoni yangu binafsi: kupotea kwa pesa ilikua mwisho wangu na yeye,haya likapita,kufikia hatua ya kuniaibisha binafsi ningekuja kutolewa polisi tu nisingekuwa na hatua nyingine zaidi ya kumfundisha tabia.

Wewe ungefanyaje? Elezia
 
Nilichojifunza;
1. Kuchukua fedh za mpenzi wako bila ridhaa yake hiyo ni wizi
2. Wazazi kumruhusu kijana akaishi na binti yako bila kutoa mahari wala Ndoa huko ni sawa na kuruhusu binti yako aje kuwa Singo Mother kirahisi mno.
3. Mtoa mada amesimulia story yake binafsi huku akidanganya ni ya Rafiki yake mara ndugu wa karibu na kusababisha story isieleweke.
 
Imemtokea mdogo( wa ukoo) wangu saivi anazidi kukonda tu: umri wa wote ni kati ya 21-27.

Alimpenda dada mmoja 2018,mtoto wa kike nae alimpenda pia jamaa akawa serious nae na kutangaza kuishi nae,huyo dada akadai ana mtu mwenye malengo nae(ndoa) ambaye pia wazazi wanamjua.

Basi dogo akampa option binti achague yeye,ataamua yeye au wazazi watamwamulia,bint akaamua yeye lakin wazazi japo hawakuwa na namna bint akaanza kuishi na jamaa.

Baada ya bint kufanya maamuzi dogo alimpenda sana yani kwa jinsi alivyokuwa anatamba kwa vijana na hata mabinti waliomtaka ilionyesha kabisa mapenzi yake kwa binti.

2019 wakapata mtoto,dogo akaweka malengo ya kwenda kwa wazazi (mkoani)kulipa kabisa mahari,kijana alikua muwaz sababu mimi kama mshari wake hakunificha baadhi ya mambo.

Ikiwa imebak miezi michache kwenda ile pesa(zaidi ya mil1) ikapotea katika mazingira ya kutatanisha,kijana akawa mpole,akaja kuniambia ile pesa nilichukua kuboost biashara ikapote,kwa hiyo safari nasogeza mbele.

Mapicha picha yakaanza ndani, yule binti akadai kaongea na wazazi wake wamelaumu sababu hawaoni faida yake...lait angeendelea kusoma angepata kaz na akawasaidia nyumbani(aliishia form 4 hakufaulu). Kutokana na lawama hizo ikabidi bint abadili mawazo na kutaka kuendelea kusoma ili awatii wazazi wake...lawama kwa wazazi zilikua nyingi sababu pia dogo ana kipato cha wastani walitaka mtoto wao labda aolewe na mwajiriwa serikalini.

Dogo akapambana kumtuliza binti akakataa katu kata na full migogoro ikaanza dharau kutoka kwa bint,wakati wanavutana mtoto abak na nani ndipo dogo akagundua mengi zaidi sababu waendelee kukaa wote japo hawakuwa wakilana matunda.

Kijana akazidi kukonda anawaza mtoto wake atabak na nani,kama akienda atamtunzaje yan mambo mengi.

Dogo siku moja (nimejaribu kuficha siku na muda ili nisitoe codes) dogo akarudi usiku kidogo akasimama dirishani na kusikiliza ndani, binti alikua akiongea na simu, mazungumzo yalikuwa ya ndani kabisa(mambo ya kikubwa) na jamaa mwingine. Alipoingia ndani akamnyanganya simu,kuchungulia alikua akichat na kidume kingine,kuna sms za ile pesa iliyodaiwa kupotea.

Fujo ikatokea sababu ya ile simu binti akamwaibisha sana dogo lakini dogo hakumgusa,akamtolea shit sana mbele za watu kiasi hata majiran wakamwambia sio vizuri. Akampiga kijana lakin dogo hakumgusa. Akarudasha simu na akapewa hifadhi ya kulala kwa jirani.

Bint akafunga vitu asubuhi akasepa zake.

Hitimisho la ile pesa iliyopotea kumbe mwanzo dogo alinidanganya
Ile pesa,ilidaiwa kuja rafiki yake akaichukua sababu kama angemwambia asingempa,kwa hiyo kwa madai ya bint rafikiye aliingia na kuichukua huku akituma ujumbe kuwa atamrudshia.(bint alimwonyesha dogo sms siku ile iliyopotea).

Maoni yangu binafsi: kupotea kwa pesa ilikua mwisho wangu na yeye,haya likapita,kufikia hatua ya kuniaibisha binafsi ningekuja kutolewa polisi tu nisingekuwa na hatua nyingine zaidi ya kumfundisha tabia.

Wewe ungefanyaje? Elezia
Sijaelewa

Mdogo wa ukoo wako ambaye anazidi kukonda tu... Umri wa wote ni kati ya 21-27.

Nimesoma mwanzo tu karibia nitavune ulimi wangu 😂😂
 
🤣🤣 Mkuu essay ulikuwa unapatamo kweli au ulikuwa unadili na maswali ya kuchagua tu! Maana Kama stori tu ya kawaida ndo unaandika hivi vipi Yale maswali ya kiswahili "fasihi ni ukoko na hadhira ni kijiko,kwangua". Alama(20)..
Humu ulipita kweli..?🤣
 
🤣🤣 Mkuu essay ulikuwa unapatamo kweli au ulikuwa unadili na maswali ya kuchagua tu! Maana Kama stori tu ya kawaida ndo unaandika hivi vipi Yale maswali ya kiswahili "fasihi ni ukoko na hadhira ni kijiko,kwangua". Alama(20)..
Humu ulipita kweli..?🤣
Uandishi kipaji kaka
 
Back
Top Bottom