Kupita bila kupingwa - is this democracy too?

Mzee Mwanakijiji

Kwanza nakupongeza barua hii uliyoandika kwa umakini mkubwa.

Pili, nashauri wakati tume inaendelea kuifanyia kazi, uitume kwa vyombo vya habari- hasa magazeti yenye nia njema kwa nchi yetu yanayowafikia wengi, kama bado hujafanya hivyo. Ili mawazo mazuri haya uliyoibua yawafikie wengi mapema iwezekanavyo.
 
Last edited by a moderator:
Pongezi Mzee Mwanakijiji kwa kutoa mawazo muhimu sana.

  1. Mwalimu Nyerere alikuwa mgombea pekee kwenye chaguzi za wakati wake. Hakuna mtu alisema ameshashinda mpaka achaguliwe kwanza. Iweje leo wanaokuwa wagombea pekee waseme tayari ni wabunge?
  2. Unaweza kuwa mgombea pekee na ukashindwa. Kama hupati hata kura moja unakuwa hujashinda.
  3. NEC au Mwanasheria Mkuu wa Serikali alitakiwa awe ameshauri kuwa mgombea pekee bado ni mgombea na sio tayari mbunge. Lakini watu wenyewe ni vilaza.
  4. Kutokuwa na ushindani kwenye kugombania ni ruksa ya kugombania. Sio tayari ushindi.
 
Last edited by a moderator:
Shukrani kwa kufungua macho wengi. Naamini barua hiyo itafungua wengi ufahamu wao kuhusu suala hilo kuliko kuendelea kujipigia makofi. Ni imani yangu kuwa tume ya uchaguzi itaizingatia. Thanks

hapo ndipo tunapoona upungufu mkubwa katika Wizara mama ya Katiba na Mambo ya sheria, hapo kama sheria itafata mkondo wake kuna uwezekano mkubwa wa hayo majimbo kurudiwa uchaguzi wake,
 
Yaani hapa tungekuwa mahakama huru na tume huru, mambo yangebadilika mara moja. Lakini kwa hali ilivyo watadharau na kuyatupilia mbali. Lakini wakati umefika wa watanzania wenye nia njema kwenda mahakamani hata kama mahakama yenyewe haiko huru.

Mchezo unaochezwa hapa ni wa mahesabu. Wagombea wa CCM wamechoka kuombwa rushwa na wapiga kura, kwa hiyo mgombea mwenye fedha akimaliza kura za maoni, anawatafuta wagombea na upinzani na kuwakatia chao ili abki peke yake. Ni afadhali kuhonga mtu mmoja kuliko kuhonga makundi mbalimbali. Haiwezekani mtu apite bila kupingwa wakati hata kura za maoni alipitia kwa taabu. Kwani hao wa chama chake waliomkataa hawana haki ya kupiga kura?

Huu ni mchezo mchafu kuliko yote katika siasa.
 
Mzee Mwanakijiji, asante kwa hili. Hii ni hoja ya nguvu iliyobeba nguvu ya hoja ambayo kisheria, Tume ya Taifa ya Uchaguzi, haina mahali pa kuipangulia.

Ila kila sheria huwa inatungiwa regulations za utekelezaji wa sheria husika, sijabahatika kuziona regulations za mwaka huu, ila kwa mwaka 2005, kwenye regulations, zilimpa mamlaka msimamizi wa uchaguzi (RO) kumtangaza mgombea aliyepita bila kupingwa kuwa tayari ni mbunge/diwani mtarajiwa. Kitu ambacho bado sijakijua, hiyo regulation ili derive wapi mamlaka hayo ya kiimla!.

Regulation hiyo ilisema iwapo hakuna upinzani kwenye nafasi ya urais, mgombea aliyejitokeza, atapigiwa kura za ndiyo au hapana, kama enzi ya chama kimoja, kuweka sura na kivuli., sijui kwa nini utaratibu huu, usitumike, kwa hao wanaodaiwa kupita bila kupingwa.

Kwa kawaida kabla ya uchaguzi, document ya regulations ndio hutoka kwanza, na vyama vyote lazima visaini hizo rules of the game,ndipo kipenga kipulizwe, kwa vile kipenga kimeshapulizwa, na wakuu wa vyama vyote wameshasaini kanuni za mchezo, nadhani, there is nothing that can be done to rectify this serious anomality ili ni hoja muhimu ya kuishikia bango, katika madai ya tume huru ya uchaguzi.

Asante tena.

Pasco.
 
Kuipangua hawatashindwa. Kwani sheria ngapi zinakinzana na katiba? Watabez kwenye sheria ya uchaguz. Lakini Ukweli unabakia kuwa sheria hii haitoi haki kwa wananchi, wala sio ya kidemokrasia.

NYONGEZA: Kwa siku za baadae- hata kama kuna wagombea zaidi ya mmoja, bado kuwe na nafasi ya mtu kuchagua "siridhiki na hata mmoja" ili kama wote waliopitishwa na wananchi wao hawakubaliki basi wapewe nafasi ya kumtafuta mwingine...
 
Asante MKJJ, ni kweli wengi tulikuwa hatujaliona hili. Ni matarajio yetu kuwa vyama husika pamoja na wanaharakati wataliona hili suala kama fursa ya kuirudisha demokrasia halisi katika mkondo wake.
Wakitangazwa tu kama wabunge, kesi zifunguliwe mahakamani. Au ikiwezekana kesi ifunguliwe sasa ktk mahakama ya katiba kupata interpretation ya kisheria
 
Kwanza, nakupongeza Mwanakijiji kwa kutuelimisha thru hii barua yako. Kazi nzuri.

Pili, hawa jamaa the so called "Wabunge waliopita bila kupingwa" wajiandae kwani kampeni ni hakuna kuchagua chama kilichohasi ukweli na wabunge wasio na vision hivyo kampeni lazima ipigwe na kama hakuna anayechagulika hata kama hana mpinzani watapigia kivuli. Lakini lazima kura ipigwe.

Tatu, hii tume huwa wanajifanya vitu fulani hawavioni especially vinapowahusu CCM lazima kuwa na fair ground na ni lazima haki itendeke kwa wote siyo watu wanawekewa mapingamizi ya kitoto then jamaa wanakubali tu kisa wapinzani. Mbona CCM watu wana kesi za maadili hawajaondolewa? PIGA CHINI HAWA WABUNGE FEKI.
 
Elimu daima! Ni muhimu, kwani hao "waliopita bila kupingwa" wengi wao wamepita kwa mizengwe ya chama tawala! Kazi nzuri, endelea kuwapa somo Wadanganyika!

2010 HATUDANGANYIKI!
 
Ahsante MM lakini kama alivyoshauri Dopas barua hii isambae.
 
Last edited by a moderator:
Hoja hii ni nzito na ina ukweli ndani yake, nashauri nakala ya barua hii itolewe kwa vyama vya siasa na makundi ya wanaharakati yanayotetea demokrasia ya kweli hapa Tanzania
 
Ahsante Mzee Mwanakijji,

Hapa sasa ndipo anatakiwa mtu kama Mtikilla, kufungua kesi mahakamani, hawa watu wasiingie bungeni mpaka wachaguliwe, huku kwetu watu wamechukia sana huyu mbunge wetu ambaye kwa njama tu ametangazwa kupita bila kupingwa na matokeo yake mabango ya Chagua Kikwete yamechanwa chanwa, na hii inaweza kusababisha uvunjifu wa amani.
 
Last edited by a moderator:
Pongezi MMM kwa wazo lako. Naona kuanzia mwaka huu sheria za Tz zinapata mtihani wa mock na ujanja wa siasa unaanza kupimwa kisheria. Trend hii ni mwelekeo chanya kwa afya ya nchi yetu. Naomba pia wawekewe pingamizi na au yaandaliwe mashtaka dhidi ya wabunge hao baada ya kuapishwa bungeni rasmi
 
Thumbs up! Keep it up brother. I know your efforts will be rewarded with interest! May God bless you
 
Na endapo Tume yako itawatambua watu hawa ambao hawajachaguliwa kuwa ni "wabunge" kinyume na matakwa ya Katiba yetu ya Muungano ambayo uliapa kuilinda, mimi kama Mtanzania nikitumia haki yangu ya Kikatiba ya kudumisha hifadhi ya Katiba yetu natangaza katika dhamira safi na mapema kabisa kutowatambua watu hao ambao wataingizwa bungeni bila ya kuchaguliwa na mwananchi mmoja au kuteuliwa Rais; kwamba ninawakataa kuwatambua kama Wabunge halali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hadi pale watakapopigiwa kura na kuchaguliwa kwa namna moja au nyingine ili wapate uhalali kwa mujibu wa Katiba.

Kuna haja ya kufanya utaratibu wa kuwawekea pingamizi la kisheria ili wasiapishwe iwapo hali hiyo itajitokeza
 
Hope tutaiona hii barua via Tz daima,mwanahalisi na Raia mwema ikiwezekana watumie na wahusika
I strongly believe ipo siku kitaeleweka
 
Thumbs up! Keep it up brother. I know your efforts will be rewarded with interest! May God bless you

Ohoo dear... Mwanakijiji anazidi kujitofautisha na wengi wetu hapa JF ambao huwa tunafikiri kuandika ''vi-ingereza'' vigumu, ndio usomi na ujanja!! Hii ndio michango inayotakiwa JF. Ahsante sana na Mungu akubariki na akulinde!!
 
Asante sana kwa mawazo yenu, nimepitia mawazo na hoja zenu na kutokana nazo nimeongeza sababu nyingine 3 (ya nane, tisa na kumi). Shukrani.
 
Shukrani kwa kufungua macho wengi. Naamini barua hiyo itafungua wengi ufahamu wao kuhusu suala hilo kuliko kuendelea kujipigia makofi. Ni imani yangu kuwa tume ya uchaguzi itaizingatia. Thanks
Mwanakijiji anastahili sifa nyingi. Ni wachache sana, kama wapo, ambao walikuwa wameliona hili. Wengi tulikuwa tumejiunga na mkumbo wa kudhani kuwa CCM imewapiga mabao wapinzani bila kuangalia matakwa ya Katiba. Sasa kazi siyo kuishawishi Tume ya Uchaguzi kuchukua hatua bali vyama vya upinzani vichukue hatua za kisheria/kikatiba kuhakikisha kuwa utapeli huu wa CCM haufanikiwi. Hasante M.M.
 
Back
Top Bottom