Kupinga serikali tatu ni sawa na kupinga rasimu yote

sajosojo

JF-Expert Member
Apr 14, 2010
1,017
619
rasimu imetoka ikiwa na mapendekezo juu ya serikali 3 tu, hakuna njia nyingine ya kupinga zaidi ya kuikataa rasimu yote or kuunga mkono serikali tatu na kuziboresha zaidi i.e hizi serikali za zanzibar na tanzania bara ziongozwe na waziri mkuu or gavana japo kwa ccm ni ngumu kumeza
 
Siyo sawa kwani rasimu ina mapendekezo ya mabadiliko mengi, siyo serikali tatu tu. Kuna suala la spika, tume huru ya uchaguzi nk. Ninachoona mimi nikuwa watu wanakimbilia sual la serikali tatu wengine wanapinga na wengine wanaunga mkono.
Nikiangalia Taifa la Tanzani kwa sasa na miaka ijayo suala la serikali tatu haliepukiki labda kama ni kuunda serikali moja yaani nchi moja. Ukangalia vuguvugu lililopo Zanzibar, niwazi wazanzibari wanahitaji serikali yao yenye madaraka kamili na wamefikia mahali pa kutaka mambo yote na kujikuta wanaacha suala moja tu la ulinzi katika muungano, Watanganyika nao wamechoka kuendeshwa na kanchi kadogo kama Zanzibar, wanaona hakunia uwiano stahili, Angalia hata katika hii tume ya mabadiliko, wajumbe ni 50, 50 kati ya Zanzibara na Tanganyika; watanganyika wanaona si sawa kwa watu 1.2m kuwa na maamuzi sawa na watu 43m. Ni wazi linchi likubwa kama Tanganyika lina resources nyingi na pia matumizi makubwa; pia kanchi kadogo kama Zanzibar kana resources kidogo lakini pia na matumizi kidogo.
UNapotaka watu 1.2m waamue sawa na watu 43m kwa usawa, ni wazi hawa 1.2m utakuwa unawapa sauti kubwa juu ya resources za hawa 43m.
Waanzibar imekuwa inapata karibu kila kitu inachohitaji na silaha yao kubwa imekuwa ni kutishia kuuvunja muungano. Ebu mwenye kumbukumbu atukumbushe ni vitu gani alivyokuwa anadai rais wa Zanzibar Abdu Jumbe Mwinyi vilivyosababisha kuchafuka kwa hali ya kisiasa Zanzibar; na je ni vingapi wamepata na vingapi bado?
Baba wa Taifa aliwahi kusema tutafute sababu za sasa za kuwa na muungano tena katika sura ile ya 1964. Maana yake ni kuwa kama hazipo, tubadilishe sura ya Muungano au tusiwe nao kabisa.
 
Siyo sawa kwani rasimu ina mapendekezo ya mabadiliko mengi, siyo serikali tatu tu. Kuna suala la spika, tume huru ya uchaguzi nk. Ninachoona mimi nikuwa watu wanakimbilia sual la serikali tatu wengine wanapinga na wengine wanaunga mkono.
Nikiangalia Taifa la Tanzani kwa sasa na miaka ijayo suala la serikali tatu haliepukiki labda kama ni kuunda serikali moja yaani nchi moja. Ukangalia vuguvugu lililopo Zanzibar, niwazi wazanzibari wanahitaji serikali yao yenye madaraka kamili na wamefikia mahali pa kutaka mambo yote na kujikuta wanaacha suala moja tu la ulinzi katika muungano, Watanganyika nao wamechoka kuendeshwa na kanchi kadogo kama Zanzibar, wanaona hakunia uwiano stahili, Angalia hata katika hii tume ya mabadiliko, wajumbe ni 50, 50 kati ya Zanzibara na Tanganyika; watanganyika wanaona si sawa kwa watu 1.2m kuwa na maamuzi sawa na watu 43m. Ni wazi linchi likubwa kama Tanganyika lina resources nyingi na pia matumizi makubwa; pia kanchi kadogo kama Zanzibar kana resources kidogo lakini pia na matumizi kidogo.
UNapotaka watu 1.2m waamue sawa na watu 43m kwa usawa, ni wazi hawa 1.2m utakuwa unawapa sauti kubwa juu ya resources za hawa 43m.
Waanzibar imekuwa inapata karibu kila kitu inachohitaji na silaha yao kubwa imekuwa ni kutishia kuuvunja muungano. Ebu mwenye kumbukumbu atukumbushe ni vitu gani alivyokuwa anadai rais wa Zanzibar Abdu Jumbe Mwinyi vilivyosababisha kuchafuka kwa hali ya kisiasa Zanzibar; na je ni vingapi wamepata na vingapi bado?
Baba wa Taifa aliwahi kusema tutafute sababu za sasa za kuwa na muungano tena katika sura ile ya 1964. Maana yake ni kuwa kama hazipo, tubadilishe sura ya Muungano au tusiwe nao kabisa.
 
Back
Top Bottom