Kupima Virusi vya Ukimwi kabla ya miezi mitatu!!!!! Suluhisho

Zogwale

JF-Expert Member
Jul 10, 2008
15,287
10,839
Wana JF,
Tarehe 1 Desemba kila mwaka ni siku ya Ukimwi Duniani na Tanzania tunaungana na dunia kusheherekea siku hiyo. Kauli mbiu ya mwaka huu ilikuwa ni pamoja na kupunguza vifo, maambukizi mapya na unyanyapaa!! (nimechukua key words tu). Ukiangalia maongezi mengi kila mtu anasisitiza upande wa maambukizi mapya ni shurti kuwa na mpenzi mmoja mliyepima na kukuta mko safi na hakuna pepesa pepesa tena nje, ya pili ni kutumia kondomu. Hili la kondomu bado nina tabu nalo kwa sababu kuna watu wameambukizwa virusi na huku walitumia kondomu. Hii inawezekana kutotumia kondomu kwa usahihi lakini pia kuna wengine kondomu zinapasuka ndani ya game!! Sasa ninashauri kuwe na vipimo vya haraka ambavyo vinaweza kuonesha virusi vya ukimwi kwa mtu kabla ya miezi mitatu wanayosema wataalam ili ukikutana na aliyekuzingua basi hapo hapo mpelekane kwa pilato mkapimane ili angalao kama kondom itapasuka usipate madhara. Hili suala la kupima halafu uambiwe urudi baada ya miezi 3 maana kama mtu umepata virusi leo au mwezi uliopita na haviwezi oneekana kwa vipimo vyetu ni hatari sana. Ila pia nasikia kuna hospital Tanzania ambazo huwa zina vipimo sensitive ambavyo vina uwezo wa kuona virusi hata cha mwezi mmoja!! Kwa nchi za wenzetu nasikia vipo na vimeokoa wengi. Kwa kuwasaidiana hapa je hapa Tanzania kuna hizo hospital ambazo unaweza kupima virusi vikaonekana kabla ya miezi mitatu? Kama zipo ni zipi? Na bei yake ni kiasi gani? Tafadhali toa maoni au majibu ya kuwasaidia watu hapa ikiwemo na wewe maana hapa tunapeana elimu pia. Post za kejeli hazitafurahiwa. Asante na karibuni kuelimishana.
 
vipimo vimekuja vipo tanzania vinatoa majibu ya maambukizi ya wiki tatu (determine)

Asante Mkuu Masoud Nyumbanyingi kwa taarifa. Kwa kuwa nimeomba kila mtu achangie mawazo ili kupata elimu tunaomba utuelimishe vipimo vinakopatikana, yaani hospitali au centre zipi na gharama ni kiasi gani. Ni bora mtu ugharimie kuliko kwenda kupima hivyo vya miezi mitatu ambavyo watu wengi wanashindwa kuvumilia. At the same time hata kama utatumia condom but ni vizuri utumie na mtu ambaye angalao ni salama so kuwa na vipimo vya fasta ni muhumu sana.
 
hospitali za serikali zote vipo na kupima ni bureeeeeeeee kabisa hakuna charges zozote zile, pia private hospital zilizoruhusiwa vinapatikana ila kwa huko wanatoza pesa mkuu
 
Wakati unapoenda kupima maambukizi ya ukimwi hospital kinachopimwa ni antibodies. Hizi ni 'kinga' inayotengenezwa na mwili wako kama jibu ya mashambulizi ya virusi vya ukimwi. Hizi antibodies zinaweza kuchukua muda kuonekana kutegemeana na kwamba virusi vimejificha wapi. Huwa hatupimwi kile kirusi chenyewe unless umeenda kupimwa DBS/PCR ambayo huwa inapima DNA ya virusi.

Hii DNA ya virus huwa inapimwa hospital kuu nne Tanzania Muhi2, Bugando, Mbeya referral na KCMC ila ni special kwa ajili ya watoto tu na huwa wanapimwa wanapofikisha mwezi mmoja. Sisi wengine wote huwa tunapimwa na Determine na Unigold ambazo zinacheck antibodies and therefore you just need to wait for the three months to confirm status yako ya maambukizi.

Hope I have shed some light on your issue.
 
Wakati unapoenda kupima maambukizi ya ukimwi hospital kinachopimwa ni antibodies. Hizi ni 'kinga' inayotengenezwa na mwili wako kama jibu ya mashambulizi ya virusi vya ukimwi. Hizi antibodies zinaweza kuchukua muda kuonekana kutegemeana na kwamba virusi vimejificha wapi. Huwa hatupimwi kile kirusi chenyewe unless umeenda kupimwa DBS/PCR ambayo huwa inapima DNA ya virusi.

Hii DNA ya virus huwa inapimwa hospital kuu nne Tanzania Muhi2, Bugando, Mbeya referral na KCMC ila ni special kwa ajili ya watoto tu na huwa wanapimwa wanapofikisha mwezi mmoja. Sisi wengine wote huwa tunapimwa na Determine na Unigold ambazo zinacheck antibodies and therefore you just need to wait for the three months to confirm status yako ya maambukizi.

Hope I have shed some light on your issue.

Asante sana mkuu kwa elimu nzuri. Hata jana kwa bahati nilikutana na mtaalam mmoja kati ya wale wanaopima na tukawa tunaelezana issue za hapa na pale hasa kuwa bado suala la virusi limekuwa gumu kwa kuwa watu wanapima mara ya kwanza na wakikuta safi huwa wanajisahau na kutorudi kupima after three months ili kupata uhakika. Naye alikiri tatizo na akasema ni kweli kuwa zile antibody haziwezi kuanza kuzalishwa kabla ya miezi mitatu. Kwa mantiki hii teknolojia iliyopo ndiyo hiyo kwa sasa. Ila tu kwa pamoja tukubali kuwa condom zinasaidia ila ni hakika zaidi kama utapima na mpenzi wako ili kuwa na uhakika na mtu unaye deal naye kuliko kuwa na hatari ya kutembea na ambaye tayari ana maambukizi kwa kuwa huwezi jua siku moja kishawishi kinakupata unaamua kurukia bila kinga kisa eti tumekuwa katika upenzi kwa muda mrefu. Salama ni kupima hata kama uko fit but condom ni must kwa mtu ambaye awali wote mnakaa mbali na hujui anachokifanya nje ya macho yako!!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom