Jana nilienda kupima HIV pale Angaza Mnazi MMoja. Lengo ilikuwa nijijue hali yangu kiafya ili niadhimishe siku ya ukimwi duniani "while I'm informed".
Nimengia hapo angaza saa 2 asubuhi, nikakuta kundi la watu wa kutosha tu. Basi ndio tumewekewa video kwenye TV wakati tukisubiri vipimo (Video ilikuwa na mikwara mingi sana kuhusiana na mambo ya ukimwi). Baadaye kidogo, akaja dada mmoja, ni mrembo, katupa semina na watu wakauliza na kujibu maswali kadha wa kadha.
Angaza sio mchezo! Nilikuwa mtu wa kati katika mfuatano wa kwenda kupima. Waliotangulia, kuna watu walitoka wanacheka, wengine walitoka na nyuso zimebadilika, wengine wanalia, n.k.!
Muda huo, wakati wengine tukisubiria kwenda kupima, wenye roho nyepesi walitoka na kusepa kimojaa. Ukitoka, ilikuwa ni lazima utoke na macho ya watu wote waliokuwepo hapo! Watu wakisikia purukushani kama za mtu kutaka kutoka, hasa kama alikuwa amekaa viti vya nyuma, walikuwa wakigeuka kimyakimya bila kusema chochote na kukupiga macho paa!
Mie nilitoka kwenda kupokea simu nje, walinikata macho, halafu nikasikia wadada fulani wawili wakisema amejibeep huyo! Dah, watu tulikuwa hatuaminiani kabisa! Niliwajibu, kwa taarifa yenu narudi!
Ikafika zamu yangu kwenda kuchukuliwa damu. Maongezi yangu na Dada mtoa damu yakawa hivi:
Dada: Karibu, kaa kwenye kiti (sikusalimia, maana hapo unasahau mengi), jina lako, taja majina matatu
Mimi: Simplicity. XXXX YYYY
Dada: Umri wako
Mimi: XXX
Dada: Unaishi wapi?
Mimi: Dar, Nimehamia Mbezi Kimara hivi karibuni
Dada: Kiwango chako cha elimu?
Mimi: Nimemaliza chuo, VETA
Dada: Umeoa/una mke?
Mimi: Sijaoa/sina mke
Dada: Unaishi na mwanamke/wanawake?
Mimi: Hapana, naishi mwenyewe
Dada: Namaanisha una mahusiano ya kimapenzi na wanawake?
Mimi: Hapana, nina mahusiano tu ya kawaida
Dada: Una mchumba/girlfriend?
Mimi: Sina mchumba wala girlfriend
Dada: Mara ya mwisho kushiriki ngono ilikuwa lini?
Mimi: Sijawahi kushiriki ngono
Dada: Wewe kaka, acha masihara, umekuja kufanya mzaha eee! Tafadhali umeshiriki ngono lini, mara ya mwisho, na ulitumia condom au haukutumia?
Mimi: Labda zamani, wakati tunacheza michezo ya utotoni, na sidhani hata kama nilimfanya mdada fulani enzi hizo tunacheza michezo ya baba na mama, kondomu sidhani kama zilikwepo enzi hizo. Sikumbuki chochote
Dada: Wewe kaka, naona umekuja kunipotezea muda! Sasa kama hujashiriki ngono unapima nini?
Mimi: Kwani ngoma inaambukizwa kwa kujamiana tu!
Dada: (Kwa hasiri kidogo) Haya leta mkono nichukue damu, na ukutwe unayo sasa!
Mimi: (Nikasema huyu dada hana maana, asije akanibambikizia status, sikumjibu kitu, nikajisemea, la asije akafanya makusudi)
Dada: chukua hiki kikaratasi kina namba yako, subiri nje utaitwa
Nikawa nimetoka zangu nje, ila dah, moyo ukawa unaenda sana mbio, kama mnavyojua, angaza huwezi kujiamini.
Baada ya kama dk 7, nikaitwa kwenda kuchukua majibu.
Dada: Karibu (Dada akawa mpole sana, halafu ananiangalia kwa huruma)
Mimi: A- h sa nte (Maneno yananikwama kooni!)
Dada: Umesema hujawahi kufanya ngono?
Mimi: Samahani dada wewe nipe mie majibu niende zangu
Dada: Kwa hiyo ulikuwa unanitania?
Mimi: Utani gani! Sijawahi kufanya ngono, na kama nimefanya sikumbuki ni lini
Dada: Subiri (katoka nje akamwita dada kutoka chumba kingine, nikasema, dah, majibu sio! Anatafuta ushauri namna ya kunipakulia au? Karibu nisepe alivyotoa huo mwanya lakini nikapiga moyo konde na kuamua kusubiria, baada ya kama dakika 2, Dada akarudi). Wewe kaka umeamua kwa moyo mweupe kabisa kuja kupima?
Mimi: (Nikasema, haya maswali kulikoni, kuna nini?) Ndio
Dada: Uko tayari kupokea majibu?
Mimi: Ndio
Dada: Unatambua kukutwa na maambukizi ya ukimwi sio mwisho wa kuishi?
Mimi: Ndio (Nikasema dah, something detected!)
Dada: Umeshawahi kusikia/kupata ushauri nasaha jinsi ya kuishi na virusi vya ukimwi?
Mimi: Nilishawahi kusikia radioni (Karibu nimnyang'anye daftari ambalo lilikuwa na majibu, najiuliza huyu kwa nini hanipi majibu! Nikazidi kuwa mpole)
Dada: Una watu wowote wanaokutegemea?
Mimi: Dada tafadhali naomba majibu kama unanipa
Dada: Sasa wewe unataka kupewa bila kufuata utaratibu!?
Mimi: Bwana mie nimechoka na maswali hayaishi (Nikamjibu swali lake)
Dada: Iwapo umekutwa na maambukizi ya ukimwi utafanyaje?
Mimi: Hakuna kitu kama hicho (Alicheka wakati mie jasho linanitoka!)
Dada: Wewe kaka una vituko! Hakuna si usingekuja sasa?
Mimi: Siwezi kuwa na uhakika kihivyo, ndio maana nimekuja!
Dada: Nakupa majibu kama utahitaji ushauri au elimu yoyote kuhusiana na ukimwi ofisi zetu ziko wazi Jtatu - Jumamosi, kuanzia saa mbili - saa nane mchana. Tafadhali tumia kondomu wakati wa kukutana kimwili.
Mimi: Naomba majibu (Mood yangu hapo imebadilika kabisa)
Dada: Kwa sasa hivi hauna maambukizi yoyote ya ukimwi, rudi tena kupima baada ya miezi mitatu.
Alivyomaliza tu kuongea sikumwaga, nduki nje, hakuna cha kwa heri wala nini! Kumbe nyuma nimesahau simu. Kidogo mtu ananikimbilia wee kaka umesahu simu yako. Dah huku jasho likiwa linanitoka, watu pale walinipiga macho, na wanaweza kuamini tofauti!
Angaza sio sehemu ya kufanyia majaribio, nenda kama umeamua kweli na tegemea chochote!
Dah, pamoja na kwamba jasho lilinitoka, lakini baada ya kuambiwa sina maambukizi nilitoka mwepesi kama air force one, huku moyo mweupe! Nilienda sehemu nikanunua grand malt, nikawa nakunywa huku nikipumzika taratibu!
Dah, kutokujua status yako ni zigo la misumiri, lakini kupima nako inahitaji ujivue ufahamu!
Nenda kapime ujue uwe huru.
Starehe: Ferooz ft Proffesor Jay - Starehe - YouTube
CC: watu8 lara 1 Kongosho Kaunga charminglady mdida The Boss tinna cute Himidini mwe----- Washawasha nanjilinji MadameX madameA Madame B King'asti Dublin musubati Smile Sista sister Mshinga Mashaxizo Mtambuzi MziziMkavu gfsonwin HorsePower AshaDii mimi49 Heaven on Earth Lady doctor KOKUTONA Nyani Ngabu Eiyer Boflo SnowBall snowhite Mapi
na wana MMU wengine wote, hasa hasa moderators, pamoja na kusimamia JF ni vizuri mkajua status zenu.
Nimengia hapo angaza saa 2 asubuhi, nikakuta kundi la watu wa kutosha tu. Basi ndio tumewekewa video kwenye TV wakati tukisubiri vipimo (Video ilikuwa na mikwara mingi sana kuhusiana na mambo ya ukimwi). Baadaye kidogo, akaja dada mmoja, ni mrembo, katupa semina na watu wakauliza na kujibu maswali kadha wa kadha.
Angaza sio mchezo! Nilikuwa mtu wa kati katika mfuatano wa kwenda kupima. Waliotangulia, kuna watu walitoka wanacheka, wengine walitoka na nyuso zimebadilika, wengine wanalia, n.k.!
Muda huo, wakati wengine tukisubiria kwenda kupima, wenye roho nyepesi walitoka na kusepa kimojaa. Ukitoka, ilikuwa ni lazima utoke na macho ya watu wote waliokuwepo hapo! Watu wakisikia purukushani kama za mtu kutaka kutoka, hasa kama alikuwa amekaa viti vya nyuma, walikuwa wakigeuka kimyakimya bila kusema chochote na kukupiga macho paa!
Mie nilitoka kwenda kupokea simu nje, walinikata macho, halafu nikasikia wadada fulani wawili wakisema amejibeep huyo! Dah, watu tulikuwa hatuaminiani kabisa! Niliwajibu, kwa taarifa yenu narudi!
Ikafika zamu yangu kwenda kuchukuliwa damu. Maongezi yangu na Dada mtoa damu yakawa hivi:
Dada: Karibu, kaa kwenye kiti (sikusalimia, maana hapo unasahau mengi), jina lako, taja majina matatu
Mimi: Simplicity. XXXX YYYY
Dada: Umri wako
Mimi: XXX
Dada: Unaishi wapi?
Mimi: Dar, Nimehamia Mbezi Kimara hivi karibuni
Dada: Kiwango chako cha elimu?
Mimi: Nimemaliza chuo, VETA
Dada: Umeoa/una mke?
Mimi: Sijaoa/sina mke
Dada: Unaishi na mwanamke/wanawake?
Mimi: Hapana, naishi mwenyewe
Dada: Namaanisha una mahusiano ya kimapenzi na wanawake?
Mimi: Hapana, nina mahusiano tu ya kawaida
Dada: Una mchumba/girlfriend?
Mimi: Sina mchumba wala girlfriend
Dada: Mara ya mwisho kushiriki ngono ilikuwa lini?
Mimi: Sijawahi kushiriki ngono
Dada: Wewe kaka, acha masihara, umekuja kufanya mzaha eee! Tafadhali umeshiriki ngono lini, mara ya mwisho, na ulitumia condom au haukutumia?
Mimi: Labda zamani, wakati tunacheza michezo ya utotoni, na sidhani hata kama nilimfanya mdada fulani enzi hizo tunacheza michezo ya baba na mama, kondomu sidhani kama zilikwepo enzi hizo. Sikumbuki chochote
Dada: Wewe kaka, naona umekuja kunipotezea muda! Sasa kama hujashiriki ngono unapima nini?
Mimi: Kwani ngoma inaambukizwa kwa kujamiana tu!
Dada: (Kwa hasiri kidogo) Haya leta mkono nichukue damu, na ukutwe unayo sasa!
Mimi: (Nikasema huyu dada hana maana, asije akanibambikizia status, sikumjibu kitu, nikajisemea, la asije akafanya makusudi)
Dada: chukua hiki kikaratasi kina namba yako, subiri nje utaitwa
Nikawa nimetoka zangu nje, ila dah, moyo ukawa unaenda sana mbio, kama mnavyojua, angaza huwezi kujiamini.
Baada ya kama dk 7, nikaitwa kwenda kuchukua majibu.
Dada: Karibu (Dada akawa mpole sana, halafu ananiangalia kwa huruma)
Mimi: A- h sa nte (Maneno yananikwama kooni!)
Dada: Umesema hujawahi kufanya ngono?
Mimi: Samahani dada wewe nipe mie majibu niende zangu
Dada: Kwa hiyo ulikuwa unanitania?
Mimi: Utani gani! Sijawahi kufanya ngono, na kama nimefanya sikumbuki ni lini
Dada: Subiri (katoka nje akamwita dada kutoka chumba kingine, nikasema, dah, majibu sio! Anatafuta ushauri namna ya kunipakulia au? Karibu nisepe alivyotoa huo mwanya lakini nikapiga moyo konde na kuamua kusubiria, baada ya kama dakika 2, Dada akarudi). Wewe kaka umeamua kwa moyo mweupe kabisa kuja kupima?
Mimi: (Nikasema, haya maswali kulikoni, kuna nini?) Ndio
Dada: Uko tayari kupokea majibu?
Mimi: Ndio
Dada: Unatambua kukutwa na maambukizi ya ukimwi sio mwisho wa kuishi?
Mimi: Ndio (Nikasema dah, something detected!)
Dada: Umeshawahi kusikia/kupata ushauri nasaha jinsi ya kuishi na virusi vya ukimwi?
Mimi: Nilishawahi kusikia radioni (Karibu nimnyang'anye daftari ambalo lilikuwa na majibu, najiuliza huyu kwa nini hanipi majibu! Nikazidi kuwa mpole)
Dada: Una watu wowote wanaokutegemea?
Mimi: Dada tafadhali naomba majibu kama unanipa
Dada: Sasa wewe unataka kupewa bila kufuata utaratibu!?
Mimi: Bwana mie nimechoka na maswali hayaishi (Nikamjibu swali lake)
Dada: Iwapo umekutwa na maambukizi ya ukimwi utafanyaje?
Mimi: Hakuna kitu kama hicho (Alicheka wakati mie jasho linanitoka!)
Dada: Wewe kaka una vituko! Hakuna si usingekuja sasa?
Mimi: Siwezi kuwa na uhakika kihivyo, ndio maana nimekuja!
Dada: Nakupa majibu kama utahitaji ushauri au elimu yoyote kuhusiana na ukimwi ofisi zetu ziko wazi Jtatu - Jumamosi, kuanzia saa mbili - saa nane mchana. Tafadhali tumia kondomu wakati wa kukutana kimwili.
Mimi: Naomba majibu (Mood yangu hapo imebadilika kabisa)
Dada: Kwa sasa hivi hauna maambukizi yoyote ya ukimwi, rudi tena kupima baada ya miezi mitatu.
Alivyomaliza tu kuongea sikumwaga, nduki nje, hakuna cha kwa heri wala nini! Kumbe nyuma nimesahau simu. Kidogo mtu ananikimbilia wee kaka umesahu simu yako. Dah huku jasho likiwa linanitoka, watu pale walinipiga macho, na wanaweza kuamini tofauti!
Angaza sio sehemu ya kufanyia majaribio, nenda kama umeamua kweli na tegemea chochote!
Dah, pamoja na kwamba jasho lilinitoka, lakini baada ya kuambiwa sina maambukizi nilitoka mwepesi kama air force one, huku moyo mweupe! Nilienda sehemu nikanunua grand malt, nikawa nakunywa huku nikipumzika taratibu!
Dah, kutokujua status yako ni zigo la misumiri, lakini kupima nako inahitaji ujivue ufahamu!
Nenda kapime ujue uwe huru.
Starehe: Ferooz ft Proffesor Jay - Starehe - YouTube
CC: watu8 lara 1 Kongosho Kaunga charminglady mdida The Boss tinna cute Himidini mwe----- Washawasha nanjilinji MadameX madameA Madame B King'asti Dublin musubati Smile Sista sister Mshinga Mashaxizo Mtambuzi MziziMkavu gfsonwin HorsePower AshaDii mimi49 Heaven on Earth Lady doctor KOKUTONA Nyani Ngabu Eiyer Boflo SnowBall snowhite Mapi
na wana MMU wengine wote, hasa hasa moderators, pamoja na kusimamia JF ni vizuri mkajua status zenu.
Last edited by a moderator: