Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,770
- 59,095
. . .What are you Great at?!!
Nini ukipika watu wengine wanaomba kuongeza chakula kama hawana akili nzuri? Au hawaachi kuomba uwaambie ulichoweka? Au hawaachi kutania kwamba lazima umeweka dawa au 'umepika bila nguo' lolz. . .ama wengine unashangaa wanaishia kupenda chakula ambacho hawakuwahi kukipenda mwanzo.
Mimi . . .
1. Maharage/makande, ya nazi au bila nazi. Nimefanya watu wasiopenda wananiuliza kila siku ntapika lini tena.
2. Ndizi na viazi, za nazi, mchemsho, samaki n.k. . ."lini tena nije kula" na "ntapata cha kuondokea ehhhhh?!" hua nyingi.
3. Cabbage ya nyama, na kachumbari za aina mbili hua hazikosi kuuliziwa.
4. Chapati. . . hehehe hizi hua zinanipa mtu wa kunisaidia kazi zangu kabisa. Nasema tu nnatamani kupika chapati ila sina nafasi mtu anajitoa mzima mzima.
5. Wali. . kwanzia pilau tulozoea, pilau ya mautundu binafsi, wali mweupe wa namna tofauti tofauti.
6. Kuku haswa wa kuoka. . hua nakua kichaa na spices and it always pay off.
7. Kitoweo (mchuzi) cha nyama au samaki. Wakati naanza kupika back in the days nilikua napata malalamiko sana wakati wa kula. . mchuzi ni mdogo. Kuna watoto tulikua tunaishi nao wenyewe walikua wanapenda wakidumbukiza tonge la ugali kwenye mchuzi ile kupeleka mdomoni mchuzi utiririke mkononi (I HATE THAT). . na kwenye wali waone punje zinaelea, but they eventually got over it.
8. Lasagne & pizza japo mimi silagi.
9. Samaki na nyama ya kuoka. . .lazima watu walambe vidole na kuuliza kama kuna iliyobaki.
10. Pork chops. . . nilimfundisha mtu miaka mitatu iliyopita mpaka leo haachi kunifagilia yeye akifagiliwa.
11. Chips . . . sikua najua ni nzuri kiviiiiile mpaka nilipoanza kuulizwa huwa nazifanyaje.
12. Na ya mwisho nnayokumbuka (samahanini msiopenda) KITIFAYA. . . yani hapo ndipo moto unapozimika.
Nini ukipika watu wengine wanaomba kuongeza chakula kama hawana akili nzuri? Au hawaachi kuomba uwaambie ulichoweka? Au hawaachi kutania kwamba lazima umeweka dawa au 'umepika bila nguo' lolz. . .ama wengine unashangaa wanaishia kupenda chakula ambacho hawakuwahi kukipenda mwanzo.
Mimi . . .
1. Maharage/makande, ya nazi au bila nazi. Nimefanya watu wasiopenda wananiuliza kila siku ntapika lini tena.
2. Ndizi na viazi, za nazi, mchemsho, samaki n.k. . ."lini tena nije kula" na "ntapata cha kuondokea ehhhhh?!" hua nyingi.
3. Cabbage ya nyama, na kachumbari za aina mbili hua hazikosi kuuliziwa.
4. Chapati. . . hehehe hizi hua zinanipa mtu wa kunisaidia kazi zangu kabisa. Nasema tu nnatamani kupika chapati ila sina nafasi mtu anajitoa mzima mzima.
5. Wali. . kwanzia pilau tulozoea, pilau ya mautundu binafsi, wali mweupe wa namna tofauti tofauti.
6. Kuku haswa wa kuoka. . hua nakua kichaa na spices and it always pay off.
7. Kitoweo (mchuzi) cha nyama au samaki. Wakati naanza kupika back in the days nilikua napata malalamiko sana wakati wa kula. . mchuzi ni mdogo. Kuna watoto tulikua tunaishi nao wenyewe walikua wanapenda wakidumbukiza tonge la ugali kwenye mchuzi ile kupeleka mdomoni mchuzi utiririke mkononi (I HATE THAT). . na kwenye wali waone punje zinaelea, but they eventually got over it.
8. Lasagne & pizza japo mimi silagi.
9. Samaki na nyama ya kuoka. . .lazima watu walambe vidole na kuuliza kama kuna iliyobaki.
10. Pork chops. . . nilimfundisha mtu miaka mitatu iliyopita mpaka leo haachi kunifagilia yeye akifagiliwa.
11. Chips . . . sikua najua ni nzuri kiviiiiile mpaka nilipoanza kuulizwa huwa nazifanyaje.
12. Na ya mwisho nnayokumbuka (samahanini msiopenda) KITIFAYA. . . yani hapo ndipo moto unapozimika.