Jambo Wanajamii. Ninaandika kwa masikitiko makubwa na majonzi, na stori yangu ni ya manyanyasiko makubwa.
Nimekuwa kwenye relationship huu mwaka wa 5 na huu mwaka wa pili nimekaa na huyu mwanamume as wife. Tuna watoto 2. Jamani nimepitia matatizo meeeeeeeeeengi na nimekuwa navumilia tu. Na mimi ndo nimekuwa nahangaika na kibarua changu kusupport familia. Amenipiga mara mbili vibaya tu, na hata mtoto wangu mkubwa akishuhudia.
Mara ya pili akamwita mama yake ambaye alinisimanga na kunitolea maneno machafu na hata kunivua kanga mbele za wadogo zangu,mwanangu na mkwelima wake. Mwisho walinifukuza na watoto usiku. Hata ninapoandika hapa sina sehemu ya kukaa naomba kujiegesha tu kwa ndugu. Baada ya siku moja akanifuata kuomba msamaha, mimi roho bado nzito. Siku 2 hazijapita akanitumia matusi ambayo si heshima kuandika hapa jamvini na hata kunionesha jinsi anavyobadilisha wanawake na kwamba nisipige jungu atamchukua mwanamke mwingine.
Jamani sina amani na nimekuja kuwachukia saaaaaaaaaaaana wanaume. Nimeondoka na wanangu na sitaki hata wamjue baba yao maana kanifanyia unyama. Wadau naombeni ushauri. Mdogo ana miezi 5 na wamenifukuza usiku.
Natanguliza shukrani.
Nimekuwa kwenye relationship huu mwaka wa 5 na huu mwaka wa pili nimekaa na huyu mwanamume as wife. Tuna watoto 2. Jamani nimepitia matatizo meeeeeeeeeengi na nimekuwa navumilia tu. Na mimi ndo nimekuwa nahangaika na kibarua changu kusupport familia. Amenipiga mara mbili vibaya tu, na hata mtoto wangu mkubwa akishuhudia.
Mara ya pili akamwita mama yake ambaye alinisimanga na kunitolea maneno machafu na hata kunivua kanga mbele za wadogo zangu,mwanangu na mkwelima wake. Mwisho walinifukuza na watoto usiku. Hata ninapoandika hapa sina sehemu ya kukaa naomba kujiegesha tu kwa ndugu. Baada ya siku moja akanifuata kuomba msamaha, mimi roho bado nzito. Siku 2 hazijapita akanitumia matusi ambayo si heshima kuandika hapa jamvini na hata kunionesha jinsi anavyobadilisha wanawake na kwamba nisipige jungu atamchukua mwanamke mwingine.
Jamani sina amani na nimekuja kuwachukia saaaaaaaaaaaana wanaume. Nimeondoka na wanangu na sitaki hata wamjue baba yao maana kanifanyia unyama. Wadau naombeni ushauri. Mdogo ana miezi 5 na wamenifukuza usiku.
Natanguliza shukrani.