Kupenda kumbe ni kazi! .. kunakuja na machozi!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,462
39,929
Moyo ukija kupenda, wenda ukidundadunda,
Mtu aanza kukonda, anapomkosa nyonda,
Alalama kama konda, mwenzenu kumbe kapenda,
Mtu akiisha kupenda, huogopa kuvurunda
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Ukishampenda mtu, moyo usipate kutu
Roho yako iwe kwatu, usilie mimi ‘mbwitu’
Usilete katukatu, kwa kusikia ya watu
Mwisho wajikuta fyatu, na penzi likawa butu,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Nilimpenda fulani, yule binti wa jirani,
Kaniingia moyoni, penzi hadi mifupani,
Leo kanuna jamani, amepata kisirani
Kosa langu miye nini, najiuliza watani,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi

Kusema nami hataki, akija kwangu habaki,
Kwenye miadi hafiki, nikichekesha hacheki,
Nisimuite rafiki, hata mpenzi hataki,
Hata kudeka hadeki, vya kuvila haviliki
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Nikimgusa aruka, kumbusu anan’gaka,
Nyonda mbona washtuka, wanitatiza hakika,
Lipi limevurugika, nambie wangu wa shoka,
Ni vipi umekwazika, nitonye nikatonyeka,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Siku zikapitiliza, maswali najiuliza,
Kuliza ameniliza, na majonzi kanijaza,
Najikunyata nawaza, hadi nimepitiliza,
Ni dogo amelikuza, au nikubwa sijaliwaza
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi

Nabaki nasubiria, nyonda kunihurumia,
Na aje kuniambia, ni wapi nimechapia,
Mwenzako ninaumia, ninavyokufikiria
Fanya hima kunijia, kosa sitalirudia,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi.

Nilichokuandikia, ni kweli nakuambia,
Tafadhali fikiria, jibu nalisubiria
Mikono nimeachia, niweze kukumbatia
Ni mbali tumeanzia, si tayari kuachia
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi.

Nafunga ninafungana, ya leo siyo ya jana,
Na wewe nafungamana, ee nyonda wangu mwanana,
Zikongine zafanana, penzi tulilopeana,
Fanya hima kuonana, nina hamu kukuona,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
 
Pole sana kwa kutoa chozi, pengine kapenda mwingine au umemkosea muulize polepole, kama vipi mpotezee.
 
Kusema nami hataki, akija kwangu habaki,
Kwenye miadi hafiki, nikichekesha hacheki,
Nisimuite rafiki, hata mpenzi hataki,
Hata kudeka hadeki, vya kuvila haviliki
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Labda amestukia wewe ni mlaji ukishiba waeza tafuta mti mwengineo wenye matunda kesho yake.

Ushauri: Jaribu
kutangaza nia.
 
moyo ukija kupenda, wenda ukidundadunda,
mtu aanza kukonda, anapomkosa nyonda,
alalama kama konda, mwenzenu kumbe kapenda,
mtu akiisha kupenda, huogopa kuvurunda
kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Ukishampenda mtu, moyo usipate kutu
roho yako iwe kwatu, usilie mimi ‘mbwitu’
usilete katukatu, kwa kusikia ya watu
mwisho wajikuta fyatu, na penzi likawa butu,
kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Nilimpenda fulani, yule binti wa jirani,
kaniingia moyoni, penzi hadi mifupani,
leo kanuna jamani, amepata kisirani
kosa langu miye nini, najiuliza watani,
kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi

kusema nami hataki, akija kwangu habaki,
kwenye miadi hafiki, nikichekesha hacheki,
nisimuite rafiki, hata mpenzi hataki,
hata kudeka hadeki, vya kuvila haviliki
kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Nikimgusa aruka, kumbusu anan’gaka,
nyonda mbona washtuka, wanitatiza hakika,
lipi limevurugika, nambie wangu wa shoka,
ni vipi umekwazika, nitonye nikatonyeka,
kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Siku zikapitiliza, maswali najiuliza,
kuliza ameniliza, na majonzi kanijaza,
najikunyata nawaza, hadi nimepitiliza,
ni dogo amelikuza, au nikubwa sijaliwaza
kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi

nabaki nasubiria, nyonda kunihurumia,
na aje kuniambia, ni wapi nimechapia,
mwenzako ninaumia, ninavyokufikiria
fanya hima kunijia, kosa sitalirudia,
kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi.

Nilichokuandikia, ni kweli nakuambia,
tafadhali fikiria, jibu nalisubiria
mikono nimeachia, niweze kukumbatia
ni mbali tumeanzia, si tayari kuachia
kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi.

Nafunga ninafungana, ya leo siyo ya jana,
na wewe nafungamana, ee nyonda wangu mwanana,
zikongine zafanana, penzi tulilopeana,
fanya hima kuonana, nina hamu kukuona,
kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Na. M. M. Mwanakijiji (sauti ya kijiji)
1.haya ni mapenzi original
2.mapenzi kama haya ni adimu kuyapata.
3.usanii kwenye mapenzi hivi sasa ndio unatawala kwa kiasi kikubwa.
 
Moyo ukija kupenda, wenda ukidundadunda,
Mtu aanza kukonda, anapomkosa nyonda,
Alalama kama konda, mwenzenu kumbe kapenda,
Mtu akiisha kupenda, huogopa kuvurunda
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Ukishampenda mtu, moyo usipate kutu
Roho yako iwe kwatu, usilie mimi ‘mbwitu'
Usilete katukatu, kwa kusikia ya watu
Mwisho wajikuta fyatu, na penzi likawa butu,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Nilimpenda fulani, yule binti wa jirani,
Kaniingia moyoni, penzi hadi mifupani,
Leo kanuna jamani, amepata kisirani
Kosa langu miye nini, najiuliza watani,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi

Kusema nami hataki, akija kwangu habaki,
Kwenye miadi hafiki, nikichekesha hacheki,
Nisimuite rafiki, hata mpenzi hataki,
Hata kudeka hadeki, vya kuvila haviliki
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Nikimgusa aruka, kumbusu anan'gaka,
Nyonda mbona washtuka, wanitatiza hakika,
Lipi limevurugika, nambie wangu wa shoka,
Ni vipi umekwazika, nitonye nikatonyeka,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Siku zikapitiliza, maswali najiuliza,
Kuliza ameniliza, na majonzi kanijaza,
Najikunyata nawaza, hadi nimepitiliza,
Ni dogo amelikuza, au nikubwa sijaliwaza
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi

Nabaki nasubiria, nyonda kunihurumia,
Na aje kuniambia, ni wapi nimechapia,
Mwenzako ninaumia, ninavyokufikiria
Fanya hima kunijia, kosa sitalirudia,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi.

Nilichokuandikia, ni kweli nakuambia,
Tafadhali fikiria, jibu nalisubiria
Mikono nimeachia, niweze kukumbatia
Ni mbali tumeanzia, si tayari kuachia
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi.

Nafunga ninafungana, ya leo siyo ya jana,
Na wewe nafungamana, ee nyonda wangu mwanana,
Zikongine zafanana, penzi tulilopeana,
Fanya hima kuonana, nina hamu kukuona,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)

Hii inaelekea kufanana na kisa fulani hivi, kweli kupenda ni kazi especially unapokuja kutoa machozi kwa mtu unayempenda halafu yeye haoni hilo ndio maana watu wengi wakiumizwa na mtu fulani kwenye mapenzi na yeye anaamua kuumiza wengi pia ambayo kwangu mimi huwa siaafiki kabisa lakini hayo ndio mapenzi na kupenda ni kazi tegemea lolote kukutokea.
 
Pole mzeee MM wajua kupenda ni kazi ..wewe waweza penda binti fulani kumbe yeye kapenda kwingine .:confused2:
 
Usipokuwa makini, unaweza kuwa chizi
Ukipenda kwa undani, utatokwa na machozi
Unasumbukia nini, si uwaambie wazazi
Mapenzi yanayo nguvu, tena yashinda mauti,
 
Hapa tupo ukurasa mmoja mkuu inawezekana kabisa hii....:confused2:
 
Moyo ukija kupenda, wenda ukidundadunda,
Mtu aanza kukonda, anapomkosa nyonda,
Alalama kama konda, mwenzenu kumbe kapenda,
Mtu akiisha kupenda, huogopa kuvurunda
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Ukishampenda mtu, moyo usipate kutu
Roho yako iwe kwatu, usilie mimi ‘mbwitu'
Usilete katukatu, kwa kusikia ya watu
Mwisho wajikuta fyatu, na penzi likawa butu,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Nilimpenda fulani, yule binti wa jirani,
Kaniingia moyoni, penzi hadi mifupani,
Leo kanuna jamani, amepata kisirani
Kosa langu miye nini, najiuliza watani,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi

Kusema nami hataki, akija kwangu habaki,
Kwenye miadi hafiki, nikichekesha hacheki,
Nisimuite rafiki, hata mpenzi hataki,
Hata kudeka hadeki, vya kuvila haviliki
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Nikimgusa aruka, kumbusu anan'gaka,
Nyonda mbona washtuka, wanitatiza hakika,
Lipi limevurugika, nambie wangu wa shoka,
Ni vipi umekwazika, nitonye nikatonyeka,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Siku zikapitiliza, maswali najiuliza,
Kuliza ameniliza, na majonzi kanijaza,
Najikunyata nawaza, hadi nimepitiliza,
Ni dogo amelikuza, au nikubwa sijaliwaza
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi

Nabaki nasubiria, nyonda kunihurumia,
Na aje kuniambia, ni wapi nimechapia,
Mwenzako ninaumia, ninavyokufikiria
Fanya hima kunijia, kosa sitalirudia,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi.

Nilichokuandikia, ni kweli nakuambia,
Tafadhali fikiria, jibu nalisubiria
Mikono nimeachia, niweze kukumbatia
Ni mbali tumeanzia, si tayari kuachia
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi.

Nafunga ninafungana, ya leo siyo ya jana,
Na wewe nafungamana, ee nyonda wangu mwanana,
Zikongine zafanana, penzi tulilopeana,
Fanya hima kuonana, nina hamu kukuona,
Kupenda kweli ni kazi, huko kwaja na machozi!

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Kweli kupenda ni kazi,huwa najiuliza kwanini Mungu aliweka upendo wa mapenzi i wish usingekuwepo!! MM hapo penye red ni pagumu sana maana watu wengi ni selfish,full usanii utadhani wote wamepita bagamoyo!
 
wenzio walipokubwa na maswahiba kama yako walisema hivi

si kitu kunipuuza, kwako tamaa sikati
fikira sitogeuza, moyo wangu madhubuti
ni lani utavyoweza, naapa sikubanduki


anaependa kikweli, hachoki kuvumilia
habadilishi kauli, japo ukimchukua



wajua ninakupenda, ndo mana waniringia
unanifanyia inda, mapenzi kuyasusia
baada ya hiki kidonda, na moto unanitia

anaependa kikweli, hachoki kuvumilia
habadilishi kauli, japo ukimchukua


nikimbie japo mwaka, nipo ninakungojea
ukirudi nakutaka, wala sitoona haya
........................,........................


anaependa kikweli, hachoki kuvumilia
habadilishi kauli, japo ukimchukua


Source: nyimbo moja ya zamani sana
 
Uwe na busara kama Wiselady
Au na upendo kama FirstLady,
Na ma "passion kama queenKammy
Mapenzi bado yanatesa, 'kiyapatia unatesa!

Na Ukipendwa kama Nyani Ngabu
Watu hawakosi sababu!
Ili mradi mapenzi tabu, na
Mapenzi bado yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Mfikiriea Zion daughter,
Kila kitu amepata,
Naye JS amedata, kisa
Mapenzi bado yanatesa, 'kiyapatia unatesa!

Uwe mkarimu kama bacha
Au Fidel80 wa kukacha,
Na The Finest wa kuacha..bado
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Ukiwa mtulivu kama Asprin
Au Mlokole kama Gaijin
Bado utaikuta Acid! kisa?
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa!

Nilidhani katulia Teamo,
Kumbe madhila yangalimo!
Nikamuliza Masanilo! kanambia:
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Ni kwako Cheusimangala,
Je waweza kugangamala?
Manake hayana muamala,
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Alipata kusema Nyamayao,
'kitusimulia ya kwao
Kumbe ndio hayo hayo,
Mapenzi yanatesa 'kiyapatia unatesa....
 
kaizer sikujua kama na wewe ni mmalenga ...............:smile-big:
 
Uwe na busara kama Wiselady
Au na upendo kama FirstLady,
Na ma "passion kama queenKammy
Mapenzi bado yanatesa, 'kiyapatia unatesa!

Na Ukipendwa kama Nyani Ngabu
Watu hawakosi sababu!
Ili mradi mapenzi tabu, na
Mapenzi bado yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Mfikiriea Zion daughter,
Kila kitu amepata,
Naye JS amedata, kisa
Mapenzi bado yanatesa, 'kiyapatia unatesa!

Uwe mkarimu kama bacha
Au Fidel80 wa kukacha,
Na The Finest wa kuacha..bado
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Ukiwa mtulivu kama Asprin
Au Mlokole kama Gaijin
Bado utaikuta Acid! kisa?
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa!

Nilidhani katulia Teamo,
Kumbe madhila yangalimo!
Nikamuliza Masanilo! kanambia:
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Ni kwako Cheusimangala,
Je waweza kugangamala?
Manake hayana muamala,
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Alipata kusema Nyamayao,
'kitusimulia ya kwao
Kumbe ndio hayo hayo,
Mapenzi yanatesa 'kiyapatia unatesa....

Dah nimeipenda hii.....
Very creative.....
 
Uwe na busara kama Wiselady
Au na upendo kama FirstLady,
Na ma "passion kama queenKammy
Mapenzi bado yanatesa, 'kiyapatia unatesa!

Na Ukipendwa kama Nyani Ngabu
Watu hawakosi sababu!
Ili mradi mapenzi tabu, na
Mapenzi bado yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Mfikiriea Zion daughter,
Kila kitu amepata,
Naye JS amedata, kisa
Mapenzi bado yanatesa, 'kiyapatia unatesa!

Uwe mkarimu kama bacha
Au Fidel80 wa kukacha,
Na The Finest wa kuacha..bado
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Ukiwa mtulivu kama Asprin
Au Mlokole kama Gaijin
Bado utaikuta Acid! kisa?
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa!

Nilidhani katulia Teamo,
Kumbe madhila yangalimo!
Nikamuliza Masanilo! kanambia:
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Ni kwako Cheusimangala,
Je waweza kugangamala?
Manake hayana muamala,
Mapenzi yanatesa, 'kiyapatia unatesa

Alipata kusema Nyamayao,
'kitusimulia ya kwao
Kumbe ndio hayo hayo,
Mapenzi yanatesa 'kiyapatia unatesa....
mwanafasihi mzuri sana wewe Kaizer, vipaji mnavyo mnavikalia, au mnataka watu tuwahamasishe kwa campaign za shuka kwa shuka ili mvitoe vipaji vyenu hadharani?
 
Dah nimeipenda hii.....
Very creative.....
Kaizer nitakupeleka kurecord hiyo single, baada ya hapo utafanya featuring na Mwanakijiji so itakuwa full mautamu.Love it, hasa hapo kwa Fidel kukacha nikilinganisha na avatar yake mh,,:becky::eyebrows:
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom