Kupeleka watoto wa miaka2 hadi miaka10 shule za bweni kwa wazazi tujitafakari sana

mama D

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
19,763
35,201
Kumekua na ongezeko kubwa la wazazi kukupeleka watoto wadogo kuanzia chekechea. Kweli wazazi tumekua na majukumu mengi huku usaidizi katika malezi ukiwa changamoto kubwa sana.

Lakini kwa niliyoyaona na kuyasikia wazazi tujitafakari tena, watoto wengi wanaopelekwa bweni wanateseka mnoo. Wengine wanaishia kupata hadi ulemavu sababu ya kukosa malezi yanayoambatana na upendo toka kwa familia.

Matukio mengi yanayotokea kule yanaumiza ila kuna hili la mtoto ninayemjua kupelekwa bweni akiwa miaka3. Alipofika darasa la tano mtoto aligundulika kuwa na tatizo la kutoa haja kubwa bila kujijua. Kwanza kabisa tulijua mtoto keshaharibiwa, wazazi katika kuhangaika kumpeleka hospitali tofauti na kila wanasaikolojia na madaktari walivyokua wakimchunguza hawakuweza kupata ushahidi kwamba amewahi kufanyiwa kitendo chochote.

Baadae wakaambiwa wamepeleke muhimbili kwa matibabu zaidi na pale ndipo madaktari walipogundua kwamba mtoto katika umri wake mdogo alikua akiogopa kujisaidia either sababu ya kukaripiwa au kuona aibu kitu ambacho kilisababisha mfumo wa ufahamu ya utoaji haja kupoteza mawasliano na mtoto kupoteza uwezo wa kuhisi haja kabisa.

Kama sisi wazazi tunaona ni kazi kubwa sana kuwalea hawa malaika tuliowazaa kwa uchungu tunaonaje hili la kumpelekea matron mmoja watoto 10, 20, 30 na kuamini kwamba anawapa malezi bora kuliko sisi?

Watoto vinateseka jamani na kibaya kama mzazi unavyoamini kwamba shuleni ni bora kuliko nyumbani na matron na walimu ni bora kuliko wewe na mtoto anaamini hivyo, hadi uje ujue anachopitia mtoto anakua kashaumia sana
 
Hili ni tatizo kubwa sana. Unawezaje kwanza kukaa mbali na mwanao kizembe zembe kisa shule ukiangalia mtoto mwenyewe mdogo.

Hii mitindo imechangia pakubwa sana kuwepo na mashoga,wasagaji,vijana kutokuwa na utu, tabia mbaya, uhuni na uchafu mwingine.
 
Kingine wamama hata kama mmesoma secular kiasi gani, kaeni majumbani,kwani huko ndiko kuna salama kwenu na kwa watoto wenu.

Siku hizi wamama hamlei watoto, watoto wenu wanalelewa na wadada wa kazi na na matroni (Mtaniweka sawa hapa kama nimekosea kuandika) huko mashuleni. Hakuna mtu mwenye mapenzi na mwanao na kumjali kukuzidi wewe uliye mzaa hao, hao wengine wapo kwa ajili ya ujira tu

Sisi waswahili huwa tunanena hivi "Kila abiria achunge mzigo wake"

Ahsante.
 
Hili ni tatizo kubwa sana. Unawezaje kwanza kukaa mbali na mwanao kizembe zembe kisa shule ukiangalia mtoto mwenyewe mdogo.

Hii mitindo imechangia pakubwa sana kuwepo na mashoga,wasagaji,vijana kutokuwa na utu, tabia mbaya, uhuni na uchafu mwingine.
Mie nshasema marufuku kupeleka wanangu bweni, nwisho wa siku wanakuwa kama Amsterdam wa Lissu! Kufa bila marinda dhambi kubwa!
 
Ni Hatari asee, Kuna shule flani mkoa flani mtoto wa darasa la nne alikamatwa anaweka sumu kwenye chakula Cha wanafunzi wa darasa la tatu, alibanwa Sana akasema kila kitu...kiukweli tuwe makini Sana.
 
Watanzania tumekurupukia mambo ya ajabu sana.

1. Unapelekaje mtoto wa chini ya miaka 10 kwenda kukaa boarding school.

2. Unatafuta hela wewe na mumeo ila baada ya miaka 7 mnakaa kuangalia tena afya ya mtoto wenu kwa machungu makubwa.

3. Niliwahi kwenda shule moja ya boarding kwa watoto wa miaka 4 yaani mpaka unaona huruma. Watoto hawana furaha kabisa yaani wamekaa kaa tu.

Tuache kutesa watoto.
 
Asilimia kubwa ya wazazi wa aina hii ni wale mama na baba usipitwe kila sherehe wanataka wawemo,kila warsha,kongamano,safari za kikazi etc wao wanajiweka mbele mbele. Mtoto akilalamika anaambiwa ni kwa faida yake
 
Wenyewe wanajiona wajanja na wazazi bora kwa kuweza kumlipa mtu awalelee watoto kupunguza usumbufu.
Kuna Wazazi wengine kila wakizidi kupata pesa ya kuchezea na Ujinga wao unaongezeka! Kibaya zaidi hawaruhusiwi hata kupaona sehemu wanapolala Watoto wao!!
 
Asilimia kubwa ya wazazi wa aina hii ni wale mama na baba usipitwe kila sherehe wanataka wawemo,kila warsha,kongamano,safari za kikazi etc wao wanajiweka mbele mbele. Mtoto akilalamika anaambiwa ni kwa faida yake
Watoto wanateseka sana. Kama huna muda wa kulea heri usizae
 
Kuna Wazazi wengine kila wakizidi kupata pesa ya kuchezea na Ujinga wao unaongezeka! Kibaya zaidi hawaruhusiwi hata kupaona sehemu wanapolala Watoto wao!!
Haya mateso wanayowapa watoto baada ya Mungu kuwabariki na pesa kama kiama kipo kweli sijui wanaenda kujibu nini
 
Ni Hatari asee, Kuna shule flani mkoa flani mtoto wa darasa la nne alikamatwa anaweka sumu kwenye chakula Cha wanafunzi wa darasa la tatu, alibanwa Sana akasema kila kitu...kiukweli tuwe makini Sana.
hebu funguka zaidi. alisema nini?
 
Back
Top Bottom