Kupata vibali vya ujenzi manispaa ya Kinondoni ni rushwa tupu

mwanza

JF-Expert Member
May 7, 2009
759
486
Jamani, nimejaribu kufuata utaratibu wa kupata kibali cha ujenzi wa nyumba kutoka manispaa ya Kinondoni ila sasa ni mwaka mmoja tangu niombe ila ni usumbufu na rushwa imejaa mpaka sasa sijapata kibali.

Nikifuatilia mwanzoni walikuwa wanasema kikao bado hakijakaa kupitisha vibali na na nilipofuatilia toka mwezi wa tatu wakaniambia madiwani mpaka wakague kiwanja. Yaani sasa imekuwa ni usumbufu kila municipal engineer ananiambia atanisaidia na kuvuta hela akisema ni kwa ajili ya kuwalainisha mabosi lakini wapi mpaka leo naenda ila natoka patupu.
Nimafuatilia mainjinia wote wanataka rushwa na nimejaribu kumwona municipal director bila mafanikio.

Jamani naomba msaada wa mawazo ili nijue hatua za kuchukuwa.
 
Ujenzi holela ndani ya miji mingi ikiwema Mwanza na Arusha na kwingineko unatokana na ukiritimba na rushwa iliyokisiri katika Halmashauri za miji na majiji hapa nchini. Watanzania wa kawaida hawezi kupata pesa ya kujengea halafu ukaahirisha kumuidhinishia kujenga zaidi ya mwaka na bado akaendelea kuwa na hizo fedha zake hivyo apatapo usumbufu kama huo anaona heri ajijengee tuu liwalo na liwe huko mbeleni. Sasa inapofika suala la kubomolewa ndio ujue serikali inapochangia umasikini wa raia wake kwa kuruhusu watendaji watumie ofisi za umma kukwamisha mambo kwa manufaa binafsi.
 
Mkuu, sasa hivi vikao vya kupitia michoro na kutoa vibali hufanyika mara 2 kwa mwezi kwenye municipal zote za jiji la DSM, diwani hahusiki na kikao cha kupitisha kibali cha ujenzi coz hiyo inahusu zaidi watalaam, kama ofisa mipango miji, mhandisi na msanifu majengo, madiwani wao wanakaa vikao vya kuamua matumizi ya ardhi kama sikosei lakini sio kupitisha ramani, huo ni uhuni tu wanakufanyia.
 
There is nothing political in this thread! Mods please do something about this misplacement.
 
Ili upate kibali cha ujenzi unapaswa kuwa na ramani ya jengo unalokusudia kujenga, pia ramani ya jengo lazima iendane na matumizi ya eneo husika. (residential, commercial residential etc) sasa huo ukiritimba wa kusema madiwani pia wanatakiwa wawepo kwenye kikao cha kupata kibali ni uhuni tu huo.
 
Ni kweli kabisa mkuu. Hili suala ni kwa manispaa zote tu, huwezi kupata kibali hata kama una documents zote zinazostahili. Utazungushwa hadi utaamua kukata tamaa. Pole sana mwananchi mwenzangu, lakini wana JF hili ni tatizo kubwa sana linalokabili taifa letu. Nawaomba wana JF kwa sauti ya pamoja tupaze ili tujaribu kuondoa suala kama hili katika manispaa zetu.

SALAMU KWA WAZIRI WA ARDHI (PROF ANNA TIBAIJUKA)
Hapa muheshimiwa una kazi kubwa sana, ila mimi binafsi nina imani sana na huyu mama. Ameonyesha uthubutu katika hili, tumpe muda na pia tumtie moyo huyu mama jasiri. Hapa muheshimiwa kwa kweli unatakiwa uwe na msimamo wa kweli vinginevyo utaadhirika katika hili.
 
mkuu asaivi vikao vya kupitia michoro na kutoa vibali hufanyika mara 2 kwa mwz kwenye municipal zote za jiji la DSM, diwani hahusiki na kikao cha kupitisha kibali cha ujenzi coz hiyo inahusu zaidi watalaam, kama ofisa mipango miji, mhandisi na msanifu majengo, madiwani wao wanakaa vikao vya kuamua matumizi ya ardhi kama sikosei lakini sio kupitisha ramani, huo ni uhuni tu wanakufanyia.
<br />
<br />
Wataalamu akiwemo municipal engineer na municipal architect walishapitia michoro yangu na wakaniambia haina tatizo ila jambo lingine ni kuwa si jukumu la mwananchi wa kawaida kufuatilia ilitakiwa nikisha submit documents zangu wao wazipitishe kwa wahusika kwa muda unaotakiwa na either waniambie hiyo nyumba haifai kujengwa au wanipe kibali si kusubiri zaidi ya mwaka bila majibu
 
There is nothing political in this thread! Mods please do something about this misplacement.
<br />
<br />
Labda ndugu yangu Mbopo haujaelewa pale municipal nimejaribu kuongea na baadhi ya wafanyakazi wanasema tatizo pale lipo kati ya technical staff na wanasiasa ndio maana madiwani ambao ni wana siasa wanaweza kumkataa mkurugenzi nahili la kutoa vibali nalo linawahusu madiwani kwa sababu wanashiriki kwenye vikao.
Tatizo lingine ni rushwa ambayo wenye nafasi kubwa ya kutusaidia sisi wananchi wa kawaida ni wanasiasa tuliowachagua likiwemo hili la kuwajulisha taabu tunayoipata kwenye vibali vya ujenzi
 
Mkuu nakushauri umpigie simu meya wa manispaa Hon Mwenda, mpe malalamiko yako, namba yake ni 0754441335
 
Mkuu nakushauri anza ujenzi fastaaa, cha msingi uwe na risiti uliyotumia kulipia maombi ya kibali cha ujenzi.

Kuna sheria inasema zikipita siku 90 toka ulipoomba kibali cha ujenzi na hujapewa sababu ya kutopewa kibali cha ujenzi unaweza kuanza ujenzi na lawama au matatizo yatayojitokeza yatabebwa na municipal husika, ipo ngoja niingie library nikutafutie.

Watanzania tujifunze kujua haki zetu ndogondogo za msingi kabsaaa.

Nawasilisha hoja.
 
mkuu nakushauri anza ujenzi fastaaa...cha msingi uwe na risiti uliyotumia kulipia maombi ya kibali cha ujenzi. <br />
<b><br />
kuna sheria inasema zikipita siku 90 toka ulipoomba kibali cha ujenzi na hujapewa sababu ya kutopewa kibali cha ujenzi unaweza kuanza ujenzi na lawama au matatizo yatayojitokeza yatabebwa na municipal husika</b>...ipo ngoja niingie library nikutafutie. <br />
<br />
watanzania tujifunze kujua haki zetu ndogondogo za msingi kabsaaa...nawasilisha hoja
<br />
<br />
Nitashukuru sana ukinisaidia hicho kipengele cha sheria na mimi naanza fasta ujenzi
 
Mimi niliweka file langu hapo swala likakaa muda mrefu wakati nafuatilia nikaambiwa mara afisa Mipango yupo ktk kikao mara nikaambiwa yuko Dodoma bungeni sasa hapo ndio niligombana nao hadi nikagundua lile file liko kwa masecretary na ndio waliokwamisha mizunguko yote. Niligombana nao sana baada ya mwezi nikapata kibali. Hiyo ni golofa kama ni nyumba ya chini, anza kujenga tu.

Nilichachamaa shida hakuna pa kushitaki masekretary vigeuvigeu na mayor haonekani vikao daily. Nikagundua pia vikao ndio vinawapatia posho siyo kuwa hapo ofisini.

Nashukuru kwa hiyo namba ila sijui kama atapokea yeye au secretary.
 
Back
Top Bottom