Habari zenu wana jf, ninaomba msaada wenzangu, mke wangu anaendelea kupata damu ya uzazi huu ni mwezi wa pili toka ajifungue, ingawa inatoka kidogodogo. Je hii ni hali ya kawaida au atakuwa na tatizo?
===
===
Kuna kitu inaitwa lochia, ambayo ni maji maji yatokayo kupitia uke baada ya kujifungua. Hii huchukua kuanzia wiki tatu mpaka sita na stage zake. Siku ya kwanza mpaka sita huwa mekundu(reddish) siku ya sita mpaka kumi huwa pink in color na baada ya hapo huwa whitish or yellowish-white. Yanatakiwa yasiwe na harufu mbaya kwani ni dalili ya uambukizo. Sasa wa kwako mwezi wa pili bado ni reddish! Kuna tatizo jingine, nenda hospitali.