Kupandisha majini/mashetani na kunena kwa lugha ngeni

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Sep 10, 2017
10,561
19,056
Kumekua na kawaida kwa watu wanopandisha majini au mashetani au maruhani au mizimu kudai au kudaiwa kua na uwezo wa kuzungumza lugha ngeni isiyofahamika na yule mtu ambae jini linapanda kichwani mwake na kumposes kwa muda flani wenyewe wakimwita kiti. Kwamba utakuta mtu hajawahi kujifunza labda kimasai au hata kiingereza lakini akipandisha huyo jini au mzimu wenye asili ya kizungu au kimasai utakuta eti na yeye anaongea lugha hizo.

Kwa utafiti nilioufanya jambo hilo sio kweli. Katika hili kuna mambo mawili tu. Ama huyo kiti anafahamu hiyo lugha ambayo jini anaitumia, au kama kiti hajui kabisa lugha husika basi ataongea makorokocho kwa lafudhi ya lugha hiyo na watasema hiyo ndio lugha yenyewe, hasa kama katika wasikilizaji hakuna mtu anayeijua. Kwa mfano kama kiti anafahamu kuongea kiingereza broken basi huyo jini ataongea pia kiingereza broken

Hapa sipingi taarifa wanazozitoa kama ni sahihi au sio sahihi (maana kwa utafiti wangu wengine hutoa taarifa sahihi ya mambo yaliyotokea bila ya kua wameelezwa au kuyajua kabda). Ninachokisema na kutoa changamoto ni kwamba lugha watakayoitumia ni ile ambayo kiti anaijua kwa ufasaha na kama anijua kwa kubabaisha na jini ataongea kwa kubabaisha. Natoa changamoto kama kuna mtu anaweza kutoa ushuhuda tofauti na aka prove laki moja ya krismass kutoka kwangu inamsubiri
 
ushuhuda upi unataka,

mie nimeona kiti akiwa kapandisha na haongei lugha yoyote mpya bali anakuwa ana andika chini maneno ya kiarabu na baada ya kuondoka (ruhani) anakuomba umwambie alisemaje (mengine anakuwa anayajua) na anaisoma ile karatasi

Pia nimeona kiti (anakuwa na ruhani na majadi) inatokea siku anakuja mtu wa jadi ambaye gata kiti hamfahamu na anatibu.

mkuu umewahi tibiwa kwa maji na mawe tu bilq kupewa kitu chochote.

unataka ushuhuda upi hasa
 
nimekumbana na hizi vitu toka utotoni mwangu i mean nimekuwa nikiwaona hawa watu wa aina hii tangu utotoni na wakati mwingine kutokea kupendwa na hawa makitu wananipa zawadi mbalimbali hahahaha lolz itakuwa nina nyota ya mapepo asee
 
Nimewahi shuhudia kiti ana tibu watu wa mataifa tofauti tena kwa lugha fasaha alikuwepo mkomoro, mkongo na sie wabongo

hawajui kiswahili ila alipo pandisha akawa ana bonga nao kilugha chao, pale walipo takiwa fanya kitu ndo kiswahili kilikuwa kinatumika

umekutana na matapeli sio waganga mkuu
 
Ukisikia mtu kapandisha majini au ananena kwa lugha jua ni moja kati ya mambo mawili
Either
1. Anajifanya au
2. Ni kichaa apelekwe hospitalini
 
ushuhuda upi unataka,

mie nimeona kiti akiwa kapandisha na haongei lugha yoyote mpya bali anakuwa ana andika chini maneno ya kiarabu na baada ya kuondoka (ruhani) anakuomba umwambie alisemaje (mengine anakuwa anayajua) na anaisoma ile karatasi

Pia nimeona kiti (anakuwa na ruhani na majadi) inatokea siku anakuja mtu wa jadi ambaye gata kiti hamfahamu na anatibu.

mkuu umewahi tibiwa kwa maji na mawe tu bilq kupewa kitu chochote.

unataka ushuhuda upi hasa
Sipingi uwezo wa maruhani au mizimu au jadi kutibu, hua wanatibu na wanajua taarifa na habari nyingi sana. Ninachosema hakuna jini au jadi atakae ongea au hata kuandika lugha ambayo kiti haijui. Huyo alieandika kiarabu kama kweli kiti hajui kiarabu basi nakupa changamoto kua kilichoandikwa sio kiarabu. Yaweza kua ni lugha ambayo huyo jini au kiti wake au mtu anayetafsiri anaijua. Watu wengi wakiona maandishi ya ajabu ajabu wanadanganyika hicho ni kiarabu
 
Hujui tofauti ya kupandisha majini yakaanza kuongea kiarabu au lugha za ajabu ajabu za masheni na kunena kwa lugha.kunena kwa lugha ni kujazwa Roho mtakatifu kunakojidhihirisha kwa kuongea lugha kwa kuongozwa na Roho mtakatifu.

Utafiti wako uliufanya kwa watu wenye majini/mapepo/masheti.
 
Mkuu na jirani yangu hapa anahayo makitu.. Mdada na mfaham vyema kaishia la saba tu ila akipanda uyo sijui ndio kiti anamwaga ung'eng'e atari
 
Sipingi uwezo wa maruhani au mizimu au jadi kutibu, hua wanatibu na wanajua taarifa na habari nyingi sana. Ninachosema hakuna jini au jadi atakae ongea au hata kuandika lugha ambayo kiti haijui. Huyo alieandika kiarabu kama kweli kiti hajui kiarabu basi nakupa changamoto kua kilichoandikwa sio kiarabu. Yaweza kua ni lugha ambayo huyo jini au kiti wake au mtu anayetafsiri anaijua. Watu wengi wakiona maandishi ya ajabu ajabu wanadanganyika hicho ni kiarabu
si kweli nisha ona kiti kapandisha anaongea ki kongo na hakifahamu hata kidogo ila walio kuwa wana tibiwa walikuwa wanaelewa lugha iyo.
 
Nimewahi shuhudia kiti ana tibu watu wa mataifa tofauti tena kwa lugha fasaha alikuwepo mkomoro, mkongo na sie wabongo

hawajui kiswahili ila alipo pandisha akawa ana bonga nao kilugha chao, pale walipo takiwa fanya kitu ndo kiswahili kilikuwa kinatumika

umekutana na matapeli sio waganga mkuu
Mimi natoa changamoto mkuuhuyo atkua anajua hizo lugha , kikomoro na Kikongo(kama sio lingala yenyewe) ni viswahili tu vya kubadilisha lafudhi
 
Mimi natoa changamoto mkuuhuyo atkua anajua hizo lugha , kikomoro na Kikongo(kama sio lingala yenyewe) ni viswahili tu vya kubadilisha lafudhi
wewe naona unataka ligi sasa mtu huyu namfahamu mimi hta kongo hajawah fika, huko komoro ndo kabisaaa
 
Wewe mtoa mada na nyie wengine mnaosema mtu aliyepagawa na pepo hawezi kusema lugha asioifahamu hamjui kitu mnachosema. Kwanza kwa Kiingereza kupagawa kunaitwa "being possessed" Yaani huyo pepo anayenena huwa AMEMMILIKI KABISA huyo mtu. Pili, mtu aliyepandisha mapepo anapokuja kuulizwa baadaye hajui alisema nini (maana sio yule binadamu anayesema bali pepo aliye ndani yake). Kama unamfahamu mtu yeyote ambaye anahudhuria maombi ambapo mapepo yanatolewa muulize atakwambia ni kweli. Ni jambo la kawaida kabisa. Hata waganga wanaotibu kwa kutumia majini na vitabu, wao wenyewe wakipandisha mashetani yao wanakuja kuuliza baadaye kwamba jini alisemaje. Na wateja wao wenye majini pia hawatambui hayo majini yalikuwa yanasema nini wakati wanaaguliwa.
 
Hujui tofauti ya kupandisha majini yakaanza kuongea kiarabu au lugha za ajabu ajabu za masheni na kunena kwa lugha.kunena kwa lugha ni kujazwa Roho mtakatifu kunakojidhihirisha kwa kuongea lugha kwa kuongozwa na Roho mtakatifu.

Utafiti wako uliufanya kwa watu wenye majini/mapepo/masheti.


Nyie wafia dini mna matatizo sana.

Eti kunena kwa lugha ni kujazwa roho mtakatifu.

Mada zingine mkiona zina mashetani zipitieni mbali huku mkiziombea zishindweee.
 
Wewe mtoa mada na nyie wengine mnaosema mtu aliyepagawa na pepo hawezi kusema lugha asioifahamu hamjui kitu mnachosema. Kwanza kwa Kiingereza kupagawa kunaitwa "being possessed" Yaani huyo pepo anayenena huwa AMEMMILIKI KABISA huyo mtu. Pili, mtu aliyepandisha mapepo anapokuja kuulizwa baadaye hajui alisema nini (maana sio yule binadamu anayesema bali pepo aliye ndani yake). Kama unamfahamu mtu yeyote ambaye anahudhuria maombi ambapo mapepo yanatolewa muulize atakwambia ni kweli. Ni jambo la kawaida kabisa. Hata waganga wanaotibu kwa kutumia majini na vitabu, wao wenyewe wakipandisha mashetani yao wanakuja kuuliza baadaye kwamba jini alisemaje. Na wateja wao wenye majini pia hawatambui hayo majini yalikuwa yanasema nini wakati wanaaguliwa.

Iko wazi Mkuu.

Vinginevyo watuambie huwa wanafanya viini macho.
 
daah, ishawahi nitokea hiyo nlipandsha Mara ya kwnz kabisa nkawa naongea na kuandika cjui ni quran ama kiarabu kile huku natafsir kiswahl
 
Kumekua na kawaida kwa watu wanopandisha majini au mashetani au maruhani au mizimu kudai au kudaiwa kua na uwezo wa kuzungumza lugha ngeni isiyofahamika na yule mtu ambae jini linapanda kichwani mwake na kumposes kwa muda flani wenyewe wakimwita kiti. Kwamba utakuta mtu hajawahi kujifunza labda kimasai au hata kiingereza lakini akipandisha huyo jini au mzimu wenye asili ya kizungu au kimasai utakuta eti na yeye anaongea lugha hizo.

Kwa utafiti nilioufanya jambo hilo sio kweli. Katika hili kuna mambo mawili tu. Ama huyo kiti anafahamu hiyo lugha ambayo jini anaitumia, au kama kiti hajui kabisa lugha husika basi ataongea makorokocho kwa lafudhi ya lugha hiyo na watasema hiyo ndio lugha yenyewe, hasa kama katika wasikilizaji hakuna mtu anayeijua. Kwa mfano kama kiti anafahamu kuongea kiingereza broken basi huyo jini ataongea pia kiingereza broken

Hapa sipingi taarifa wanazozitoa kama ni sahihi au sio sahihi (maana kwa utafiti wangu wengine hutoa taarifa sahihi ya mambo yaliyotokea bila ya kua wameelezwa au kuyajua kabda). Ninachokisema na kutoa changamoto ni kwamba lugha watakayoitumia ni ile ambayo kiti anaijua kwa ufasaha na kama anijua kwa kubabaisha na jini ataongea kwa kubabaisha. Natoa changamoto kama kuna mtu anaweza kutoa ushuhuda tofauti na aka prove laki moja ya krismass kutoka kwangu inamsubiri
Aah,haya ni mawazo yako bwana,una haki ya kuyatoa.Hata hivyo ukweli ni huu,jini au pepo ana "supernatural powers,"kwa hiyo ana uwezo mkubwa sana, achilia mbali wa kuongea lugha yeyote anayoitaka through a person.Jini ana uwezo wa ku-manipulate your body the way he wishes,at any time,including speaking in any tongue through a person.

Njia pekee mtu anayoweza kumzuia jini au pepo asiweze ku-manipulate mwili wa mwanadamu in anyway ni kukiri wokovu/kumpokea Yesu au kuzaliwa mara ya pili.Ukishafanya hivyo unampokea Roho Mtakatifu.Roho Mtakatifu is a righteous being tofauti na majini na mapepo, ambayo ni very evil beings.Huyu anapoingia katika mwili wa mtu kama vile jini anavyofanya,anamuongoza mtu into all truth about God,worshipping him and righteousness. He might at times use a person to bring Gods messages to true believers(the church) and hence speak through him by using the so called "tongues." Through the Holy Spirit while speaking in tongues,a person may also pray to God for personal edification.Kwa hiyo njia pekee ya kupendeza Mungu ni kupokea Roho Mtakatifu,without the Holy Spirit you are as evil as you can possibly be.
 
Back
Top Bottom