Kupanda kwa ghafla kwa bei za bidhaa mbali mbali baada ya uchaguzi

Jatropha

JF-Expert Member
Apr 9, 2009
1,151
199
Ndugu WaJF taarifa kutoka mtaani zinaonyesha kuwa bei za bidhaa mbali mbali zimepanda maradufu mara tu baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010; Kama tutakavyokumbuka suala hili la mfumko wa bei ilikuwa ni moja ya ajenda kuu za CHADEMA katika uchuguzi huu.

Habari zinaonyesha kuwa saruji imepanda kutoka Shs 12,500/ kufikia 15,000/= hapa mjini, ndoo ndogo ya mafyta ya kula imepanda kutoka Shs 16,000/= hadi Shs 24,000/= n.k

Wakati natoa wito kwa wabunge wa CHADEMA kuanza kuisurubu Serikali kwa hali hii, naomba wanaJF wenye taaluma ya kiuchumi watusaidie nini chanzo cha hali hii kutokea tena kwa kiwango kikubwa kiasi hiki?
 
acha tu bei ipande kwani nini..si ndo mijitu ilikuwa inataka mambo yawe hivo acha na yawe hivoo hivoo
 
kuna siku (kabla ya uchaguzi)nilikuwa navuka naelekea Kigamboni,
Wakati nakata tiketi nikamwuliza makataji tiket mbona gharama ya kuvuka kwa gari ni kubwa.
Akasema na bado kwani baada ya uchaguzi gharama itapanda zaidi.
Nikashangaa kwanini ipande baada ya uchaguzi, nami sikupata jibu.
 
Wakuu, hili ni tishio na inasikitisha sana, kila kitu kimepanda bei na ukiuliza kwa nini muuzaji anakuambia hii bei ni baada ya kuchakachua.
Naomba wadau mnaohusika mliangalie hili kwa jicho la tatu.
 
Kwani mlitegemea nini zaidi ya hayo kutoka kwa Mkwere? Humu ndani tulikuwa tukilalamika kuhusu CCM watu wanatuona wehu. Juzi naongea na watu wa bush kwangu wanalalamika kwamba wanashindwa kuuza mahindi kwa kuwa bei ipo chini mno. Sasa bei za mazao ya wakulima zimeshuka halafu bei za bidhaa nyingine ambazo wakulima wanazihitaji zimepanda. Hapo mkulima ana chake kweli? Lakini ni hao hao wakulima ndiyo walioongoza kwa kuipa kura CCM. Tuna lipi tena la kushauri. Acha zipande tu hata zaidi ya hapo. Na marufuku mtu kulalamika. Kwani hizo bei sizilifidiwa na Khanga na tshirt?
 
Ndugu WaJF taarifa kutoka mtaani zinaonyesha kuwa bei za bidhaa mbali mbali zimepanda maradufu mara tu baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010; Kama tutakavyokumbuka suala hili la mfumko wa bei ilikuwa ni moja ya ajenda kuu za CHADEMA katika uchuguzi huu.

Habari zinaonyesha kuwa saruji imepanda kutoka Shs 12,500/ kufikia 15,000/= hapa mjini, ndoo ndogo ya mafyta ya kula imepanda kutoka Shs 16,000/= hadi Shs 24,000/= n.k

Wakati natoa wito kwa wabunge wa CHADEMA kuanza kuisurubu Serikali kwa hali hii, naomba wanaJF wenye taaluma ya kiuchumi watusaidie nini chanzo cha hali hii kutokea tena kwa kiwango kikubwa kiasi hiki?

Kura mnawapa CCM, utatuzi wa matatizo ni CHADEMA. Hamwoni kuwa mnawatesa? Dr. Slaa aliwaambia bei ya Saruji haitazidi shs.5,000 watu wakaona haiwezekani sasa ikipanda si ndo kitu wanachotaka watu?
 
Unategemea nini mkuu wakati Tanzania kila kitu tunaagiza

bei imepanda na shilingi imeshuka maana tunaagiza/nunua zaidi ya tunavyozalisha (unfavourable balance of paymment)
hatuna cha maana tunachozalisha na kuuza nje zaidi ya madini na ambayo hatulipwi ipasavyo (ufisadi)
 
Kura mnawapa CCM, utatuzi wa matatizo ni CHADEMA. Hamwoni kuwa mnawatesa? Dr. Slaa aliwaambia bei ya Saruji haitazidi shs.5,000 watu wakaona haiwezekani sasa ikipanda si ndo kitu wanachotaka watu?
Umesema sahihi mkuu, asiyesikia la mkuu huvunjika guu. Watanzania wajiandae na maumivu makubwa sana katika miaka hii mitano ijayo. Pamoja na wizi wa kura, kama wengi wangetaka mabadiliko wizi wao usingefua dafu na sasa tungejipanga vingine katika mkakati wa kuinua kipato cha Mtz na kuzibiti mfumko wa bei. Ndugu zangu wa Singida,Lindi,Pwani Tanga na kwingineko mliko ng'ang'ania kuwa CCM ni nambari wani mtaendelea kuishi kwenye Tembe kwa miaka mingine mitano.
 

Attachments

  • MAISHA BORA.jpg
    MAISHA BORA.jpg
    24.4 KB · Views: 57
  • kasi mpya 3.jpg
    kasi mpya 3.jpg
    8.8 KB · Views: 50
  • kasi mpya 4.jpg
    kasi mpya 4.jpg
    12.3 KB · Views: 51
Hawa watu wa vijijini hawaoni athali kubwa ya maisha, kwani nyumba zao ni za miti na udingo, na nyasi, vyote ni bure, wanahitaji tu chunvi , mafuta ya taa na viberiti, ambavyo havina athali kubwa ukilinganisha na watu wa mijini kila kitu ni cha kununua. Sasa cha msingi ni Kuwaconvisi ndungu zetu wa vijijini wasiipende ccm. kila mwanaharakati wa mjini afanye juhudi hizo.
 
Ndio Bwn Jatropha huo ndio ukweli tumeliwa, wajinga ndio waliwao. Mpaka tumalize hiyo miaka mitano hakuna rangi tutaacha kuona. Ujumbe wa inflation utafika hadi vijijini watakapo nunua chumvi 1Kg Shs 1000/=. Bado tuu uchakachuaji kwenye uchumi unaendelea, na hiyo hakuna mtu wa kukwepa uwe CCM, CHADEMA wala CUF, we are sailing in same boat. Msg ya Dr Slaa itafika tuu!! Watu wataelewa.
 
Iko siku tutachapata hatuwezi endelea kuumia kwa sababu ya watu wachache, Niliingia mtaani kwenda kufanya kiutafiti kidogo haya ndiyo matokeo:
Karanga Kg1 2000 baada uchaguzi 3000
Mchelek g1 1300 baada uchaguzi 1500
Nyama kg1 4000 baada ya uchaguzi 4600
Soya kg1 3000 baada ya uchaguzi 3600
Mahindi ya makande kg1 600 baada ya uchaguzi 800
Choroko kg1 3000 baada ya uchaguzi 4000
Viazi sado1 1800 baada ya uchaguzi 2500
Nyanya sado 2000 baada ya uchaguzi 5000
 
Ndugu WaJF taarifa kutoka mtaani zinaonyesha kuwa bei za bidhaa mbali mbali zimepanda maradufu mara tu baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010; Kama tutakavyokumbuka suala hili la mfumko wa bei ilikuwa ni moja ya ajenda kuu za CHADEMA katika uchuguzi huu.

Habari zinaonyesha kuwa saruji imepanda kutoka Shs 12,500/ kufikia 15,000/= hapa mjini, ndoo ndogo ya mafyta ya kula imepanda kutoka Shs 16,000/= hadi Shs 24,000/= n.k

Wakati natoa wito kwa wabunge wa CHADEMA kuanza kuisurubu Serikali kwa hali hii, naomba wanaJF wenye taaluma ya kiuchumi watusaidie nini chanzo cha hali hii kutokea tena kwa kiwango kikubwa kiasi hiki?




Na bado!
 
Ndugu WaJF taarifa kutoka mtaani zinaonyesha kuwa bei za bidhaa mbali mbali zimepanda maradufu mara tu baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010; Kama tutakavyokumbuka suala hili la mfumko wa bei ilikuwa ni moja ya ajenda kuu za CHADEMA katika uchuguzi huu.

Habari zinaonyesha kuwa saruji imepanda kutoka Shs 12,500/ kufikia 15,000/= hapa mjini, ndoo ndogo ya mafyta ya kula imepanda kutoka Shs 16,000/= hadi Shs 24,000/= n.k

Wakati natoa wito kwa wabunge wa CHADEMA kuanza kuisurubu Serikali kwa hali hii, naomba wanaJF wenye taaluma ya kiuchumi watusaidie nini chanzo cha hali hii kutokea tena kwa kiwango kikubwa kiasi hiki?


Nakumbuka kuna mtu mmoja alitoa wito kwa wapiga kura hapa jamvini. Alisema, Ni vyema watanzania wasilale siku ya uchaguzi (kwa maana ya kupiga kura na kuzilinda) ili wapate serikali isiyolala au walale siku ya uchaguzi ili wapate serikali itakayolala miaka mitano ijayo wakati wao wakikesha kuikimbiza shilingi. Pia Mrema alisha sema kuwa kuichagua CCM ni kukata tiketi ya miaka 5 ya mateso.

Mfumuko wa bei unaoonekana sasa hivi ni kionjo tu bado mfumuko wenyewe kina mkulo wakisharudi kusimamia uchumi. Tulipewa kunyoa au kusuka tukachagua kusuka sasa nywele zinawasha tunalalamika wakati tulijua kabisa mba wataingia na nyele zinawasha. Kunyoa baada ya kusuka ni gharama mara millioni kuliko kabla. Hatuwezi kubadili serikali ndani ya miaka 5 bila kumwaga damu hivyo tuendelee kuvumilia maumivu.

Pia jamaa (Waagizaji) lazma wapandishe bei ili kurudisha hela walochangia CCM. Tunasingizia mfumuko wa bei ya dola lakini hii dola imekuwa 1500 toka mwezi wa sita na sasa fluctuation yake ni ndogo. Mbona bei haikupanda toka wakati huo?
 
that is fucking style of ccm mwashanga nini mmelilia wembe mmepewa mwatarajia nini makato kwa kwenda mbele!
 
Hawa watu wa vijijini hawaoni athali kubwa ya maisha, kwani nyumba zao ni za miti na udingo, na nyasi, vyote ni bure, wanahitaji tu chunvi , mafuta ya taa na viberiti, ambavyo havina athali kubwa ukilinganisha na watu wa mijini kila kitu ni cha kununua. Sasa cha msingi ni Kuwaconvisi ndungu zetu wa vijijini wasiipende ccm. kila mwanaharakati wa mjini afanye juhudi hizo.

:israel:Kijiji changu ninachotoka tulifutilia mbali ccm toka mwaka 1999 mwenzi september wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaaa, ktk serikali ya kjiji changu chenye watu14 yaani m/kiti na katibu + timu ya watu 12 wanaounda serikali ya kijiji (Halmashauri ya kijiji) tuna mtu moja wa ccm naye yupo pale kwa sababu tu ni mpenda maendeleo.
 
Iko siku tutachapata hatuwezi endelea kuumia kwa sababu ya watu wachache, Niliingia mtaani kwenda kufanya kiutafiti kidogo haya ndiyo matokeo:
Karanga Kg1 2000 baada uchaguzi 3000
Mchelek g1 1300 baada uchaguzi 1500
Nyama kg1 4000 baada ya uchaguzi 4600
Soya kg1 3000 baada ya uchaguzi 3600
Mahindi ya makande kg1 600 baada ya uchaguzi 800
Choroko kg1 3000 baada ya uchaguzi 4000
Viazi sado1 1800 baada ya uchaguzi 2500
Nyanya sado 2000 baada ya uchaguzi 5000

Mkuu Crashwise thanks for the facts. Sijui utafiti wako ulilenga zaidi maeneo yapi vile?. I really appreciate.
 
hamjaingia kwenye maduka ya madawa, pharmacies na medical stores, halafu mwananchi wa kawaida anatoa kila kitu toka mfukoni ( kama haujatoboka). Hana bima ya afya wala serikali haimsaidii hata kidogo.
 
Iko siku tutachapata hatuwezi endelea kuumia kwa sababu ya watu wachache, Niliingia mtaani kwenda kufanya kiutafiti kidogo haya ndiyo matokeo:
Karanga Kg1 2000 baada uchaguzi 3000
Mchelek g1 1300 baada uchaguzi 1500
Nyama kg1 4000 baada ya uchaguzi 4600
Soya kg1 3000 baada ya uchaguzi 3600
Mahindi ya makande kg1 600 baada ya uchaguzi 800
Choroko kg1 3000 baada ya uchaguzi 4000
Viazi sado1 1800 baada ya uchaguzi 2500
Nyanya sado 2000 baada ya uchaguzi 5000

Naongezea kidogo (maeneo ya - sinza)

Chumvi gm 250 toka 150 baada ya uchaguzi 300
Always za kina dada 1300 baada ya uchaguzi 2000
Petrol 1500 baada ya uchaguzi 1800
Samaki fresh 4500 kgbaada ya uchaguzi 5500

 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom