Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,597
- 215,272
Kijana wangu alitafuta ajira kwa miezi sita baada ya kumaliza chuo. Mwisho tuliamua kuingia katika kilimo cha mboga mboga.
Shamba ni la urithi la ekari tatu, tulikodi trekta kung’oa visiki. Tulichimba kisima na kununua simtank la litre 3,000 pamoja na pump yake. Ilibidi kujenga kibanda na kuajiri mtu kwa mshahara wa laki moja na nusu. Huyu alimwagilia bustani na kuchuma mboga alfajiri.
Ilibidi kupata mkopo wa kununua pick up double cabin used. Alfajiri kijana alipeleka sokoni bamia, nyanya, mchicha na hoho. Kwa siku alipata laki 350/400. Hapa kuna gharama za mafuta, na kuweka marejesho ya mkopo wa gari.
Sasa hivi baada ya kupanda kwa gharama za mafuta, mpaka kufikisha mboga sokoni ni karibu laki na nusu kwa mafuta tu. Licha ya hivyo wanunuzi hakuna na mboga zinarudi.
Hasara imekuwa kubwa hata mshahara wa mfanyakazi wa shamba imekuwa vigumu kuupata.
Shamba ni la urithi la ekari tatu, tulikodi trekta kung’oa visiki. Tulichimba kisima na kununua simtank la litre 3,000 pamoja na pump yake. Ilibidi kujenga kibanda na kuajiri mtu kwa mshahara wa laki moja na nusu. Huyu alimwagilia bustani na kuchuma mboga alfajiri.
Ilibidi kupata mkopo wa kununua pick up double cabin used. Alfajiri kijana alipeleka sokoni bamia, nyanya, mchicha na hoho. Kwa siku alipata laki 350/400. Hapa kuna gharama za mafuta, na kuweka marejesho ya mkopo wa gari.
Sasa hivi baada ya kupanda kwa gharama za mafuta, mpaka kufikisha mboga sokoni ni karibu laki na nusu kwa mafuta tu. Licha ya hivyo wanunuzi hakuna na mboga zinarudi.
Hasara imekuwa kubwa hata mshahara wa mfanyakazi wa shamba imekuwa vigumu kuupata.