TataMadiba
JF-Expert Member
- Feb 7, 2014
- 9,866
- 5,742
Tangu kuingia Madarakani kwa Serikali ya Awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Vyama vya upinzani hususan chama kikuu cha Upinzani cha CHADEMA kimetoa maelekezo kwa vijana wake walioko katika mitandao mbalimbali ya kijamii kuandika taarifa za uongo dhidi ya serikali.
Maelekezo yenye lengo la kudhoofisha kasi ya utendaji kazi wa serikali ya Magufuli yamekuja baada ya Upinzani kukosa hoja za msingi za kuuwezesha kujijenga.
Baadhi ya Uzushi ambao kwa makusudi uliandaliwa na vijana hao kwa maelekezo ya viongozi wao ni pamoja na:
1. Kwamba Makamu wa rais, Samia Suluhu Hassan aliandika barua ya kujiuzulu kwa sababu eti hakuwa na maelewano na rais Magufuli
2. Kwamba Makamu wa Rais aliiagiza mamlaka husika kuzima internet kuanzia asubuhi hadi jioni ili kuwezesha watumishi kufanyakazi
3. Kwamba Rais, Dkt. Magufuli alitengua uteuzi wa RC wa Arusha, Mrisho Gambo
4. Kwamba kiwanda cha Saruji cha DANGOTE kimesitisha uzalishaji kutokana na kupanda kwa gharama za uzalishaji wakati kumbe ni kutokana na tatizo la kiufundi
5. Kwamba Benki ya CRDB itafunga matawi yake yote nchini kuanzia mwezi januari 2017 ili kupunguza gharama za uendeshaji za benki hiyo
6. Kwamba Waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi, Prof. Joyce Ndalichako atangaza kuwa Walimu wote wangeshonewa sare za kuvaa wawapo kazini
7. Kwamba Kifaru cha jeshi kiliuzwa
Huo ni baadhi tu ya uzushi ambao umekuwa ukienezwa na vijana hawa ambao wamekuwa tegemeo la propaganda za wanasiasa baada ya Serikali ya awamu ya tano kuonekana kufanyakazi kwa umakini zaidi na hivyo upinzani kukosa hoja za kupanda nazo kwenye majukwaa ya kisiasa.
Mytake: Ni wakati sasa serikali iubaini mtandao huu wa kutengeneza uzushi na kuuchukulia hatua za kisheria. Aidha Wananchi na sisi tujiepushe na uongo wa aina hii na tumuunge mkono rais bila kujali itikadi za vyama, dini na makabila yetu kwani kazi anayoifanya ni ngumu, ina vikwazo na hujuma nyingi zikiwemo hizi za kutaka kuidhoofisha serikali yake kwa maneno ya uongo.
Maelekezo yenye lengo la kudhoofisha kasi ya utendaji kazi wa serikali ya Magufuli yamekuja baada ya Upinzani kukosa hoja za msingi za kuuwezesha kujijenga.
Baadhi ya Uzushi ambao kwa makusudi uliandaliwa na vijana hao kwa maelekezo ya viongozi wao ni pamoja na:
1. Kwamba Makamu wa rais, Samia Suluhu Hassan aliandika barua ya kujiuzulu kwa sababu eti hakuwa na maelewano na rais Magufuli
2. Kwamba Makamu wa Rais aliiagiza mamlaka husika kuzima internet kuanzia asubuhi hadi jioni ili kuwezesha watumishi kufanyakazi
3. Kwamba Rais, Dkt. Magufuli alitengua uteuzi wa RC wa Arusha, Mrisho Gambo
4. Kwamba kiwanda cha Saruji cha DANGOTE kimesitisha uzalishaji kutokana na kupanda kwa gharama za uzalishaji wakati kumbe ni kutokana na tatizo la kiufundi
5. Kwamba Benki ya CRDB itafunga matawi yake yote nchini kuanzia mwezi januari 2017 ili kupunguza gharama za uendeshaji za benki hiyo
6. Kwamba Waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi, Prof. Joyce Ndalichako atangaza kuwa Walimu wote wangeshonewa sare za kuvaa wawapo kazini
7. Kwamba Kifaru cha jeshi kiliuzwa
Huo ni baadhi tu ya uzushi ambao umekuwa ukienezwa na vijana hawa ambao wamekuwa tegemeo la propaganda za wanasiasa baada ya Serikali ya awamu ya tano kuonekana kufanyakazi kwa umakini zaidi na hivyo upinzani kukosa hoja za kupanda nazo kwenye majukwaa ya kisiasa.
Mytake: Ni wakati sasa serikali iubaini mtandao huu wa kutengeneza uzushi na kuuchukulia hatua za kisheria. Aidha Wananchi na sisi tujiepushe na uongo wa aina hii na tumuunge mkono rais bila kujali itikadi za vyama, dini na makabila yetu kwani kazi anayoifanya ni ngumu, ina vikwazo na hujuma nyingi zikiwemo hizi za kutaka kuidhoofisha serikali yake kwa maneno ya uongo.