Kupaa kwa bei ya Mafuta ni Janga, Kuyashinda Majanga Huhitaji Uongozi Wenye fikra za ziada

Hamatan

JF-Expert Member
Nov 10, 2020
3,183
7,645
Ukitaka kumtambua kiongozi mzuri, ni wakati wa matatizo. Ukitaka kumtambua dereva mzuri, angalia atafanya nini pale ambapo ajali ni dhahiri.

Kuna.mambo, kama nchi, huna uwezo wa kuyabadilisha bali unahitajika kuonesha weledi na ujuzi wa pekee, namna ya kukabiliana na yale usiyo na uwezo wa kuyabadilisha.

Hakuna asiyejua kuwa bei ya mafuta imepanda kwenye soko la Dunia. Wala wananchi hawahitaji kubiwa hilo, kwa dababu wanafahamu. Wanachotaka kubiwa ni je, Serikali inafanya nini ili kukabiliana ja hali hiyo. Hapo ndipo weledi wa uongozi unapotakiwa kupimwa.

Kipindi hiki ni vha janga, na majanga yanahitaji skills za ziada kukabiliana na hali. Kukitokea janga au changamoto, ukibweteke, unateketea moja kwa moja, uktafuta suluhisho sahihi, unaweza kutoka, tena ukiwa imara zaidi kuzidi hata ulivyokuwa mwanzo. Matatizo huikomaza nchi, hasa yanapotafutiwa suluhisho sahihi.

Kubweteka na kubakia kusema eti mbona Duniani kote bei za mafuta zimepnda, ni dalili ya kuishiwa maarifa na ufahamu wa namna ya kukabiliana na tatizo la upandaji bei ya mafuta.

Kuna kodi zaidi ya 10 kwenye mafuta, zote hizi zinaongeza mzigo wa bei ya mafuta, ambao tayari ni mzito kupindukia kutokana na bei kubwa ya mafuta kwenye soko la Dunia.

Kubakia tunasema eti mbona nanchi nyingina yamepanda, kama vile, kusema vile ndiyo utatuzi wa tatizo ni kukosa uongozi wenye maarifa.

Mazingira ya uchumi ya nchi moja na nyingine, yanatofautiana sana.

Kwa mfano, mataifa yaliyoendelea, mizigo mingi inasafirishwa kwa treni zinazotumia umeme, hivyo ongezeko la bei ya mafuta, haliwezi kuwa na athari kubwa ya moja kwa moja kwenye upanfldaji wa bei za bidhaa zote. Kuna nchi sahizi, zina kiasi kikubwa cha magari yanayotumia umeme/betri badala ya mafuta, lakini pia kuna yale ya hybrid, yanatumia mafuta kidogo, umeme zaidi. Hawa wote, kwao athari ya upandaji bei ya mafuta, japo ipo, lakini siyo ya kiwango kikubwa kama hapa kwetu.

Tanzania, kila kitu kinasafirishwa kwa mafuta. Kupanda kwa bei ya mafuta, ni kupanda kwa bei ya kila kitu.

Nilishangaa sana siku moja kumsikia Waziri Mkuu, akiuliza kwa nini bidhaa zinazozalishwa hapa hapa nchini nazo zipande bei!! Loh, kweli nchi ina ombwe la uongozi. Hivi kweli Majaliwa, hana uwezo wa kutambua kuwa unapopandisha gharama za usafirishaji maana yake umepandisha bei ya kila siku? Hivi mchele kutoka Mbeya kuusafirisha mpaka Dar, unabebwa vichwani au kwenye matumbo ya watu?

Ili kukabiliana na hali mbaya ya bei ya mafuta Duniani, Serikali ifute kodi zote kwenye mafuta. Mapato ya Serikali yatashuka, na baadhi ya miradi itasimama, lakini ni afadhali kutokee hayo kuliko uchumi wa nchi na maisha ya watu yaparanganyike.

NOTE:
Kuna mambo yanatia aibu. Wasaidizi wa Rais wanasema kuwa ile kauli ya Rais kuwa bei ya mafuta Marekani ipo juu sana kuliko Tanzania, ni kwa vile Rais alishindwa kutofautisha kati ya galoni na lita. Vituo vingi vya mafuta US, bei zilizoandikwa ni kwa gallon na siyo kwa lita. Ifahamike kuwa gallon 1 ni sawa na 3.785.
 
Zamani pamoja kuwa nilikuwa mdogo lakini niliamini kuwa wanasiasa ni watu wasio na maarifa na upeo. Nafikiri nirudi tena kulekule ila changamoto imekuja zaidi kwa wenye taaluma kujiunga nao na wao kufungia maarifa yanayoweza kubadilisha nchi kwa ajiri ya mlo wa kila siku na wao kuwa wasaliti kwa wenye taaluma wenzao kwa wakati mwingine kuwa tayari hata kuwasaliti wenzao na pale wanapofanya kile kisicho na maslahi kwao.

Hivyo tumeendelea kukaa na kutawaliwa na watu wasio na maono ya mbali bali wanamaono binafsi. Hivi unafikiri kuna wanasiasa yupo tayari kuona biashara yake ya malori zaidi ya 3000 yanakosa mzigo kizembe kwa ajili ya treni harakaharaka tu. Wapo tayari wao waneemeke wengi waumie.

Nilitegemea selikali ingepunguza kodi kwenye mafuta kwa kuwa zaidi ya silimia 50 ya bei ya mafuta ni kodi. Na pia wao kupunguza gharama za uendeshaji wa serikali kwa kupunguza misafara isiyo ya lazima na kuwekeza zaidi kwenye tekinolojia sio kila sehemu lazima waende kufungua.

Likingine ni wao kuongeza uwezo wa kufanya kazi watumishi wengi wanafanya kwa kiwango kidogo kisichozidi asilimia 30 na hii inabebwa na waalimu pamoja na kada ya afya hili linatokana na maisha duni ya wengi wa watumishi muda mwingi wanafikiria jinsi ya kujikomboa na maisha kuliko kuwajibika sasa tutegemee nini mtu mwenye stress.

Tunahitaji kufikiri zaidi ya leo, kesho na kesho kutwa.
 
zamani pamoja kuwa nilikuwa mdogo lakini niliamini kuwa wanasiasa ni watu wasio na maarifa na upeo. nafikiri nirudi tena kulekule ila changamoto imekuja zaidi kwa wenye taaluma kujiunga nao na wao kufungia maarifa yanayoweza kubadilisha nchi kwa ajiri ya mlo wa kila siku na wao kuwa wasaliti kwa wenye taaluma wenzao kwa wakati mwingine kuwa tayari hata kuwasaliti wenzao na pale wanapofanya kile kisicho na maslahi kwao.
hivyo tumeendelea kukaa na kutawaliwa na watu wasio na maono ya mbali bali wanamaono binafsi. hivi unafikiri kuna wanasiasa yupo tayari kuona biashara yake ya malori zaidi ya 3000 yanakosa mzigo kizembe kwa ajili ya treni harakaharaka tu.
wapo tayari wao waneemeke wengi waumie.
nilitegemea selikali ingepunguza kodi kwenye mafuta kwa kuwa zaidi ya silimia 50 ya bei ya mafuta ni kodi. na pia wao kupunguza gharama za uendeshaji wa serikali kwa kupunguza misafara isiyo ya lazima na kuwekeza zaidi kwenye tekinolojia sio kila sehemu lazima waende kufungua. likingine ni wao kuongeza uwezo wa kufanya kazi watumishi wengi wanafanya kwa kiwango kidogo kisichozidi asilimia 30 na hii inabebwa na waalimu pamoja na kada ya afya hili linatokana na maisha duni ya wengi wa watumishi muda mwingi wanafikiria jinsi ya kujikomboa na maisha kuliko kuwajibika sasa tutegemee nini mtu mwenye stress.
tunahitaji kufikiri zaidi ya leo, kesho na kesho kutwa.
Umenena vema:

1)Tanzania, wengi tunaowaita wasomi, ni watu wenye maarifa kidogo sana, lakini walioishi miaka mingi madarasani kukariri mambo yaliyofanywa na wenye maarifa. Ndiyo maana hakuna kitu hata kimoja cha maana, ambacho wasomi wa Tanzania wamewahi kugundua. Wengine ni madokta wa uchumi na biashara, wakistaafu, wanashinndwa kuendesha hata mradi wa ufugaji kuku. Ni wasomi wasio na maarifa, wala elimu ya viwango walivyoishia kusoma. Maana yake ni kwamba unamkuta dokta aliyefikia kiwango cha PhD lakini ana elimu chini ya ile ya kidato cha nne ya biashara.

Kati ya watu wasio na mchango wowote wa maana ni hao wanaojiita wasomi wa Tanzania. Wengi wao ni wanafiki, waongo, watu wa kujikomba kwa watawala, wamekuwa watumwa wa fikra wa watawala wasio na Elimu, alimradi kama wanawahakikishia kujaa kwa matumbo yao.
 
Ukitaka kumtambua kiongozi mzuri, ni wakati wa matatizo. Ukitaka kumtambua dereva mzuri, angalia atafanya nini pale ambapo ajali ni dhahiri.

Kuna.mambo, kama nchi, huna uwezo wa kuyabadilisha bali unahitajika kuonesha weledi na ujuzi wa pekee, namna ya kukabiliana na yale usiyo na uwezo wa kuyabadilisha.

Hakuna asiyejua kuwa bei ya mafuta imepanda kwenye soko la Dunia. Wala wananchi hawahitaji kubiwa hilo, kwa dababu wanafahamu. Wanachotaka kubiwa ni je, Serikali inafanya nini ili kukabiliana ja hali hiyo. Hapo ndipo weledi wa uongozi unapotakiwa kupimwa.

Kipindi hiki ni vha janga, na majanga yanahitaji skills za ziada kukabiliana na hali. Kukitokea janga au changamoto, ukibweteke, unateketea moja kwa moja, uktafuta suluhisho sahihi, unaweza kutoka, tena ukiwa imara zaidi kuzidi hata ulivyokuwa mwanzo. Matatizo huikomaza nchi, hasa yanapotafutiwa suluhisho sahihi.

Kubweteka na kubakia kusema eti mbona Duniani kote bei za mafuta zimepnda, ni dalili ya kuishiwa maarifa na ufahamu wa namna ya kukabiliana na tatizo la upandaji bei ya mafuta.

Kuna kodi zaidi ya 10 kwenye mafuta, zote hizi zinaongeza mzigo wa bei ya mafuta, ambao tayari ni mzito kupindukia kutokana na bei kubwa ya mafuta kwenye soko la Dunia.

Kubakia tunasema eti mbona nanchi nyingina yamepanda, kama vile, kusema vile ndiyo utatuzi wa tatizo ni kukosa uongozi wenye maarifa.

Mazingira ya uchumi ya nchi moja na nyingine, yanatofautiana sana.

Kwa mfano, mataifa yaliyoendelea, mizigo mingi inasafirishwa kwa treni zinazotumia umeme, hivyo ongezeko la bei ya mafuta, haliwezi kuwa na athari kubwa ya moja kwa moja kwenye upanfldaji wa bei za bidhaa zote. Kuna nchi sahizi, zina kiasi kikubwa cha magari yanayotumia umeme/betri badala ya mafuta, lakini pia kuna yale ya hybrid, yanatumia mafuta kidogo, umeme zaidi. Hawa wote, kwao athari ya upandaji bei ya mafuta, japo ipo, lakini siyo ya kiwango kikubwa kama hapa kwetu.

Tanzania, kila kitu kinasafirishwa kwa mafuta. Kupanda kwa bei ya mafuta, ni kupanda kwa bei ya kila kitu.

Nilishangaa sana siku moja kumsikia Waziri Mkuu, akiuliza kwa nini bidhaa zinazozalishwa hapa hapa nchini nazo zipande bei!! Loh, kweli nchi ina ombwe la uongozi. Hivi kweli Majaliwa, hana uwezo wa kutambua kuwa unapopandisha gharama za usafirishaji maana yake umepandisha bei ya kila siku? Hivi mchele kutoka Mbeya kuusafirisha mpaka Dar, unabebwa vichwani au kwenye matumbo ya watu?

Ili kukabiliana na hali mbaya ya bei ya mafuta Duniani, Serikali ifute kodi zote kwenye mafuta. Mapato ya Serikali yatashuka, na baadhi ya miradi itasimama, lakini ni afadhali kutokee hayo kuliko uchumi wa nchi na maisha ya watu yaparanganyike.
Umenena. Tupo pabaya ndugu
 
IMG-20220505-WA0190.jpg
 
Hizi ndizo nchi zinazoongozwa na watu wenye akili iliyotangulia mbele ya matatizo.

Ukiwa na viongozi ambao hawana uwezo wa kuona athari ya jambo kabla halijatokea, kama Tanzania, ni hasara kwa nchi nzima.

Mtu atakayemfanya Samia, licha ya kuwa na dhamira njema yake, awe very unpopular ni Mwigulu. Uongozi unahitaji kitu cha ziada, zaidi ya dhamira njema.

Watu wote hawa wenye doctorate za kujipachika, kama Mwigulu, wanaishi kwa ujanja ujanja, hawafai kuwa viongozi kwa namna yoyote ile. Ni gabbage.
 
Back
Top Bottom