Kuongoza nchi kunahitaji sana busara na hekima kuliko chochote

Major

JF-Expert Member
Dec 20, 2007
1,865
2,439
Kwanza napenda bila unafiki wowote kumpa sifa kubwa sana Mwenyekiti wa CCM kaka yetu JK. Aliongoza nchi hii kwa umakini mkubwa sana. Anahitaji kila aina ya sifa kutoka kwa yeyote mzalendo wa nchi hii. Alitumia hekima na busara kubwa. Hii ilifanya nchi ikatulia vizuri sana

Inanifanya niamini kuwa, uongozi wa nchi siyo lazima kiongozi awe na elimu kubwa sana. Kama kuna wakati nchi hii iliwahi kupitia ktk changamoto nyingi, basi ni kipindi cha JK.

Kwanza ndiyo wakati demokrasia ilishika kasi mno. Lakini sikuwahi kumsikia kaka yetu akipiga marufuku mkutano wa mtu au chama chochote.na nchi ikaendelea kutulia Kama maji ya mtungi.

Kipindi chake kila mtu alikuwa na furaha akifuhia amani na kila aina ya uhuru. Mungu akujaalie maisha marefu na yenye baraka Mwenyekiti wetu.

Sasa hivi hali ni tofauti kabisa. Kiongozi aliyepo anaaza kuigawa nchi vipande vipande.watu wa itikadi tofauti hawasalimiani, hawazikani. Zanzibar ndiyo mfano halisi. Mfano mwingine ni bunge letu na vyama vyetu vyote vya siasa kwa ujumla. Hali ni mbaya. Mlio karibu naye mwambieni ukweli kuwa hali ni mbaya. Msisifie kila kitu.

Sasa hivi kuna hatari kubwa sana nchi hii ikaingia ktk machafuko makubwa kabisa kuwahi kutokea. Hili kila mtu analiona.na yanaweza kuanzia Dodoma na yakasambaa nchi nchi nzima.

Ushauri wangu, mkuu wa nchi aite mkutano wa vyama vyote wakae pamoja watafute muafaka. Kinga ni bora kuliko tiba.
 
Anasema hana muda..... Tutakumbuka maneno ya Sumaye
Mkuu, Kati ya watu ambao wangeweza kumsaidia sana huyu kiongozi wetu ni JK. Lakini yeye anamdharau. Ni vema akamwuliza yeye alifanyaje mpaka akaweza?. Kwa sasa wananchi tuko gizani na hofu imetanda everywhere.
 
Umemponda J.p.m na kumsifia J.k. ! ! Hata uzi wako wachangiaji watakuwa wachache.
 
Umemponda J.p.m na kumsifia J.k. ! ! Hata uzi wako wachangiaji watakuwa wachache.
Hakuna nilipompanda JP, soma vizuri. Ni ushauri natoa. Ina maana panapoharibika wazi wazi na panaonekana mtu akisema kweli basi inakuwa ameponda? Open your mind
 
Tatizo hakujiandaa kuwa kiongozi mkubwa hivyo.

Amepita baada ya msuguano wa wale wawili wenye nguvu.

Tusimlaumu ila tujue tuna miaka mingine 10 ya hovyo.
 
Niliwahi kumshauri Rais mmoja Ambaye kwangu mimi naweza kudhihirisha pasi na Shaka kuwa ndiye raisi wa hovyo kutokea tangu nimeijua hii dunia, alipuuza ushauri wangu tena akanidhaarau. Matokeo yake baada ya miezi 3 vita ikafumka.

Wamepigana wenyewe kwa wenyenyewe kwa miaka 5' watu waliokufa ni zaidi ya laki 3 pamoja na mateso makubwa kwa akina mama na watoto. Juzi tu mwanzoni mwa 2016 ati ndiyo anafata ushauri wangu. It's too late.

Tena ni wa hapa East African. Kila mtu anamjua. Usidharau kila kitu. Wengine huwa tumejaliwa kuona mambo kabla hayajatokea.
 
Kwanza napenda bila unafiki wowote kumpa sifa kubwa sana Mwenyekiti wa CCM kaka yetu JK. Aliongoza nchi hii kwa umakini mkubwa sana. Anahitaji kila aina ya sifa kutoka kwa yeyote mzalendo wa nchi hii. Alitumia hekima na busara kubwa. Hii ilifanya nchi ikatulia vizuri sana

Inanifanya niamini kuwa, uongozi wa nchi siyo lazima kiongozi awe na elimu kubwa sana. Kama kuna wakati nchi hii iliwahi kupitia ktk changamoto nyingi, basi ni kipindi cha JK.

Kwanza ndiyo wakati demokrasia ilishika kasi mno. Lakini sikuwahi kumsikia kaka yetu akipiga marufuku mkutano wa mtu au chama chochote.na nchi ikaendelea kutulia Kama maji ya mtungi.

Kipindi chake kila mtu alikuwa na furaha akifuhia amani na kila aina ya uhuru. Mungu akujaalie maisha marefu na yenye baraka Mwenyekiti wetu.

Sasa hivi hali ni tofauti kabisa. Kiongozi aliyepo anaaza kuigawa nchi vipande vipande.watu wa itikadi tofauti hawasalimiani, hawazikani. Zanzibar ndiyo mfano halisi. Mfano mwingine ni bunge letu na vyama vyetu vyote vya siasa kwa ujumla. Hali ni mbaya. Mlio karibu naye mwambieni ukweli kuwa hali ni mbaya. Msisifie kila kitu.

Sasa hivi kuna hatari kubwa sana nchi hii ikaingia ktk machafuko makubwa kabisa kuwahi kutokea. Hili kila mtu analiona.na yanaweza kuanzia Dodoma na yakasambaa nchi nchi nzima.

Ushauri wangu, mkuu wa nchi aite mkutano wa vyama vyote wakae pamoja watafute muafaka. Kinga ni bora kuliko tiba.
Naamini ni mkristo safi anaemjua Mungu hivyo basi amkumbuke mfaleme suleiman aliomba nini kwa Mungu binafsi wala hakuombewa.Mtu mwenye hofu ya Mungu binafsi huwa anakua msikivu sana na Mungu anamsaidia na hawi na maamuzi yake binafsi bila kumshirikisha Mungu.Mtu yeyeto anaejijua udhaifu wake na kuomba msaada Mungu huwa anamsikia na si ajikwezae huwa anashushwa na ajishushae anakweza.Hizo ndio kanuni za kumjua Mungu.Hekima kwa kiongozi ni kila kitu.
 
Nani alikuambia mtukifu rais huwa anakosea?? Nadhani wewe umechoka kuishi uraiyani. Alafu unahamu ya kuhojiwa na polisi kwa kuchochea machafuko na kusababisha taharuki kwa bandiko lako. Mwache rais wetu mwema afanye kazu yake atuletee viwanda na wataalam wa IT kutoka Rwanda waje watusaidie tusonge mbele.
 
Nani alikuambia mtukifu rais huwa anakosea?? Nadhani wewe umechoka kuishi uraiyani. Alafu unahamu ya kuhojiwa na polisi kwa kuchochea machafuko na kusababisha taharuki kwa bandiko lako. Mwache rais wetu mwema afanye kazu yake atuletee viwanda na wataalam wa IT kutoka Rwanda waje watusaidie tusonge mbele.
Mkuu, ukweli humuweka mtu huru daima. Na ni lazima ujue. Hii nchi ni mali yetu wote. Tena tuliachiwa urithi na babu zetu.ni lazima tuheshimu utaratibu tuliojiwekea sisi wenyewe ili kuipa afya nchi yetu.
 
Kinga ni bora kuliko tiba, ungekuwa unatoa ushauri wakati wa kuchukua fomu maana mtu anapojieleza unajua huyu sie huyu ndie.
 
Umemponda J.p.m na kumsifia J.k. ! ! Hata uzi wako wachangiaji watakuwa wachache.
yeye amesema ukweli idadi ya wachangiaji inamhusu nini? Hivi hizi akili zenu hazikuagi? au ndio zimedumaa
 
Inategemea na nchi yenyewe ila kwa Tz kuongoza n rahis sana haina haja ya busara
 
Nchi ya South Sudan. Ina jumla ya raia milion 8 tu. Lakini ina utajiri mkubwa sana wa mafuta. Kwa hesabu za 2011 ilionekana kila siku moja serikali ilikuwa inapata pesa ambayo, wakiamua kumgawia kila mwananchi basi kila raia angepata dola 200 kila Siku.

Cha ajabu, kwa kuwa Salva Kiir Hana busara na hekima, akaitumbukiza ile nchi ktk vita ya wenyewe kwa wenyewe tena kwa mikono yake mwenyewe. Sasa hivi pamebakia vumbi ndiyo anajuta. Kichwa ngumu haimfikishi mtu popote.
 
Katika mambo ambayo yalinifanya nimuone Kikwete ni Kiongozi ni haya yafuatayo:

(1) Alivyosolve Mgogoro wa Kuchinja kati ya Waislamu na Wakiristo

(2) Alivyo solve mgogoro wa Walimu, Wafanyakazi na Madaktari kwa Kuyapa Mazungumzo nafasi huku akichanganya Carrot na Stick approach

(3) Jinsi alivyokuwa haogopi kukaa na Viongozi wa Upinzani na Kuzungumza masuala

(4) Jinsi alivyomkata Lowasa, halafu akamuachia uhuru wa kuzunguuka nchi nzima na kufanya kampeni atakavyo


Jk ni born Leader
 
Y
Katika mambo ambayo yalinifanya nimuone Kikwete ni Kiongozi ni haya yafuatayo:

(1) Alivyosolve Mgogoro wa Kuchinja kati ya Waislamu na Wakiristo

(2) Alivyo solve mgogoro wa Walimu, Wafanyakazi na Madaktari kwa Kuyapa Mazungumzo nafasi huku akichanganya Carrot na Stick approach

(3) Jinsi alivyokuwa haogopi kukaa na Viongozi wa Upinzani na Kuzungumza masuala

(4) Jinsi alivyomkata Lowasa, halafu akamuachia uhuru wa kuzunguuka nchi nzima na kufanya kampeni atakavyo


Jk ni born Leader
Umesema kweli tean kweli tupu
 
Back
Top Bottom