Kuongea na kuwafanyia "nasty" things wahudumu wa kike sio jambo zuri

Good evening brothers and sisters.

Kuna jambo nimekuwa nalishuhudia mara kwa mara na limekuwa likinipa maswali kadhaa. Ni kuhusu wanaume kuongea maneno "nasty" kwa wahudumu hasa wa migahawani na sehemu nyingine na wengine hadi wanawachezea miili yao.

Leo niliingia sehemu kupata mtori asubuhi sasa pembeni nilikuwa nimekaa na bro mmoja mtu mzima kabisa na watu wengine pembeni, huyu bro akamwita muhudumu ambaye ni wa kike, yule muhudumu alikuja na kuanza kumsikiliza jamaa, jamaa likaropoka"unanitolea macho hivo unataka nini kutoka kwangu, au dudu?" huku akijichekesha chekesha. Aisee nilimshangaa sana jamaa, kulikuwa na ulazima gani wa kuongea vile tena sehemu yenye watu wengi?

Wengine wanaendaga mbali na kuanza kuwashika miili yao. Naona hili sio jambo zuri, watu waheshimu kazi za watu.

Au hii ni package iliyopo kwenye kuhudumiwa? Maana linakuwa kama ni jambo la kawaida kwa hawa wahudumu wa kike.
Unakuwa kama unaishi matogoro bana....
kumbe upo hapa hapa town
 
Ndicho KE wanachopenda, maofisini hata mashuleni ukitaka uelewane nao lazima uwe na akili hizo. Hata humu jf ni hivyohivyo
 
Na kupitia hii situation nilimwambiaga wife kitu kinachoitwa kukufungulia mgahawa sahau jpo kila siku anatamani,mkeo akiwa mama ntilie atanyanyasika sana watamshka makalio,watamchezea wanaume tubadilikeni na tuwe na roho za huruma kwa wenzetu,bora wew ulkasrika tu mm nlishawahi kumlamba mtu kofi kwa ujinga huo
In short wanawake huwa hatupendi hyo tabia ya kuzalilishwa maana mtu Yuko kazini
 
Good evening brothers and sisters.

Kuna jambo nimekuwa nalishuhudia mara kwa mara na limekuwa likinipa maswali kadhaa. Ni kuhusu wanaume kuongea maneno "nasty" kwa wahudumu hasa wa migahawani na sehemu nyingine na wengine hadi wanawachezea miili yao.

Leo niliingia sehemu kupata mtori asubuhi sasa pembeni nilikuwa nimekaa na bro mmoja mtu mzima kabisa na watu wengine pembeni, huyu bro akamwita muhudumu ambaye ni wa kike, yule muhudumu alikuja na kuanza kumsikiliza jamaa, jamaa likaropoka"unanitolea macho hivo unataka nini kutoka kwangu, au dudu?" huku akijichekesha chekesha. Aisee nilimshangaa sana jamaa, kulikuwa na ulazima gani wa kuongea vile tena sehemu yenye watu wengi?

Wengine wanaendaga mbali na kuanza kuwashika miili yao. Naona hili sio jambo zuri, watu waheshimu kazi za watu.

Au hii ni package iliyopo kwenye kuhudumiwa? Maana linakuwa kama ni jambo la kawaida kwa hawa wahudumu wa kike.
Mkeo kasafiri nini mkuu?

Mbona ile ni sehemu ya package ya siri. We nenda pale jifanye uko serious Mara mbili tatu utakuta hata huduma inachelewa kukufikia.
 
Hivi yule mzee baba hizi si ndiyo zake za kudhalilishaga dada zetu majukwaani?

Bila kupepesa macho tabia kama hizi ni za kukemewa na bila kuangalia makunyanzi ya mtu.

Ni tabia tabia za kishamba tu.
Roger that,tuwaheshimu wanawake.
 
Hiyo sekta ya huduma Imeajiri wasichana wengi na vijana wengi sana. Inabidi isimamiwe mabinti wale waheshimiwe na Na walindwe.Ndio maana Inabaki kuwa ajira ya wasichana wa aina Fulani tu. Nchi zilizoendelea Nikawaida kwa mwanachuo kufanya hizi kazi za Huduma kama part time ili kuweza kumudu gharama za maisha Chuoni.
Iwekewe mazingira rafiki, iheshimike.
 
Darmian wengine mademu zetu usishangae tukiwabambia wewe kunywa mtori wako tu
Mkuu sasa ni lazima kuyapuka?..tulikuwa maeneo ya hospital na huo mgahawa upo maeneo hayo,na tulikuwa tumekaa watu wa rika tofauti kila mtu yupo kimya..from now where tu jamaa likaropoka..aisee lazima usome mazingira
 
Mfano kwa hii case niliyoisema sio bar..ni mgahawa ambao hata vilevi hamna na penyewe zina-apply zile za kibar bar?
Sijui, ila na mie nilikuwa na haka katabia kaku watania wadada na sio kwenye migahawa midogo, ni hotel kubwa, au migahawa mikubwa huwa naona wana furahi zamani kidogo wengine hadi nilikuwa nawala ki masihara.. Ila siku hizi sifanyi hivyo tena.. wapo unao watania wanajua kweli wamajimilikisja siku ukifika unasikia shemeji shemeji sasa kama upo na mtu wa heshima ndio utakoma.. hapo lazima ubebe msala
 
Mkuu sasa ni lazima kuyapuka?..tulikuwa maeneo ya hospital na huo mgahawa upo maeneo hayo,na tulikuwa tumekaa watu wa rika tofauti kila mtu yupo kimya..from now where tu jamaa likaropoka..aisee lazima usome mazingira
Ha ha ha aibu ukaona wewe
 
Hujawakuta wao wenyewe wakiwa wanaongea mambo yao. Utaziba masikio. Na wao jinsi wanavyojibeba ndio watu wanavyowachukulia. Au sio mazee. Ukipeana utawezana?
 
Good evening brothers and sisters.

Kuna jambo nimekuwa nalishuhudia mara kwa mara na limekuwa likinipa maswali kadhaa. Ni kuhusu wanaume kuongea maneno "nasty" kwa wahudumu hasa wa migahawani na sehemu nyingine na wengine hadi wanawachezea miili yao.

Leo niliingia sehemu kupata mtori asubuhi sasa pembeni nilikuwa nimekaa na bro mmoja mtu mzima kabisa na watu wengine pembeni, huyu bro akamwita muhudumu ambaye ni wa kike, yule muhudumu alikuja na kuanza kumsikiliza jamaa, jamaa likaropoka"unanitolea macho hivo unataka nini kutoka kwangu, au dudu?" huku akijichekesha chekesha. Aisee nilimshangaa sana jamaa, kulikuwa na ulazima gani wa kuongea vile tena sehemu yenye watu wengi?

Wengine wanaendaga mbali na kuanza kuwashika miili yao. Naona hili sio jambo zuri, watu waheshimu kazi za watu.

Au hii ni package iliyopo kwenye kuhudumiwa? Maana linakuwa kama ni jambo la kawaida kwa hawa wahudumu wa kike.

Haina tofauti na hii:

Laughter as Magufuli's 'Unataka Kupanuliwa' Statement to a Woman is Given a Second Meaning -VIDEO - Opera News Official

Watu wa namna hii ni wakukemea hadharani.
 
Back
Top Bottom