Jinsi ya Kuondoa weusi katikati ya mapaja na kwapa

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,480
9,236

KUONDOA WEUSI KATIKATI YA MAPAJA NA KWAPA

Leo wapendwa nataka kuongelea jambo ambalo linasumbua sana wanawake sio kwamba wanaume wao hawana bali hawalichukulii kiundani sana kama sisi wanawake linavyotusumbua, weusi katikati ya mapaja najuwa wanawake hapa wenye tatizo hili wamesema kweli kabisa..

Weusi huo wanawake tunao sana kwasababu ya jasho katikati ya mapaja maana kutwa yanagusana kwa kuvaa sana skirts na vitu vingine vingi vinavyofanya mapaja kuwa meusi labda hata mimi sivijui utafanyaje kama na wewe mapaja yako yapo hivyo..utatumia mafuta ya nazi

Ndio mafuta ya nazi ndio dawa ya kusafisha huo weusi ukishaoga asubuhi, mchana na jioni unayapaka kwenye mapaja ndani ya mwezi bila kuacha hata siku moja utaona huo weusi wote unapotea kabisa.
Kama hukulijuwa lako hilo beba na baba mpe na mkeo pia ukirudi nyumbani

NJIA 3 ZA ASILI ZA KUONDOA WEUSI KATIKA MAPAJA NA MAKWAPA.
Inner thighs/mapaja ya ndani na makwapa hutokea weusi kutokana na msuguano wa ngozi kwasababu ya mapaja kugusana, hata ngozi iliyokauka pia inaleta weusi katika ngozi.
Hivyo nimekuletea njia natural ya kuondoa weusi huo bila kutumia madawa makali.

1. TUMIA MAFUTA YA NAZI NA NDIMU.
Mafuta ya nazi yanatumikakulainisha ngozi lakini unaweza kutumia pia katika kuondoa weusi ukichanyanya na ndimu..fata step hizi::
Chukua vijiko 3 vya mafuta ya nazi changanya na ndimu nusu
Paka sehemu yenye weusi katika mapaja huku ukisugua kama unafanya massage kwa dakika 15.
Kisha osha na maji ya uvuguvugu na kausha kwa kitambaa kilaini na kisafi.

2. TUMIA MCHANGANYIKO WA SUKARI ASALI NA NDIMU.
Mchanganyiko huu pia unaweza ukaondoa weusi katika mapaja na makwapa, fuata step hizi::
Changanya kijiko kimoja cha asali, ndimu nusu na kijiko kimoja cha sukari.
Paka sehemu yenye weusi na sugua kawaida hadi sukari ipotee.
Acha ikae kama dakika 10 kisha osha na maji ya uvuguvugu.

3. GANDA LA CHUNGWA NA ASALI
Kama mnavyojua machungwa yana vitamin C, na hivyo ukichukua ganda la chungwa pamoja na asali, mchanganyiko wake pia unaondoa weusi. Fuata step hizi::

Chukua ganda la chungwa na kijiko kimoja cha asali.
Kamua hilo ganda maji yake yangie kwenye asali.
Kausha nakusaga hilo ganda kisha poda yake ichanganye na asali
Paka mchanganyiko huo katika sehemu yenye weusi, kaa kwa muda wa dakika 15
Osha na maji ya kawaida hadi kugandaganda kupotee.
 
Nadhani ni Limao sio ndimu....

Lakini pia mtu anaweza kuchukua BAKING SODA na LIMAO akasugulia sehemu husika kama makwapani, mapajani, kwenyw vidole vya mikono na miguu.
baada ya kunawa akapaka Mafuta ya nazi.

Kiazi mviringo pia kinaondoa weusi akikate tu kipande na kuanza kusugua hata wale wenye madoa ya chunusi inawahusu hii.

Acha kutumia yale ma deodorant (sijui kama nimepatia spelling. lol) na pafyum kali zenye alcohol huleta sanaaaaa weusi.

Good Luck.
 
Aiseee hii haihusu yale mauweusi kwenye mashavu ya ndevu aiseee????
 
ila ujue kuna wengine ngozi zao ni ngumu hata uloweke kwenye mafuta ya nazi au malimao, shida iko palepale.....
 
Apake vaseline au mafuta ya nazi au asugue na ndimu kisha mafuta ya nazi
 
Kuna wengine weusi umezidi kiasi kwamba ukiona tu mshedede unanywea nywiiiiii halafu unaonekana huna nguvu za kiume shubaaaaaamit.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom