jingalao
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 35,053
- 28,245
mwezi wa pili au wa tatu mwaka huu tulimsikia waziri mkuu ndugu Pinda akitangaza ongezeko la posho ya kuitwa kazini baada ya muda wa kazi (call allowance) kwa wahudumu wa afya.
Ni hivi majuzi tulisikia kutoka bungeni kupitia kwa waziri wa afya ndg mwinyi na pengine waziri mkuu ndg Pinda kuwa posho ya uchunguzi wa maiti(postmortem allowance) imeongezwa kutoka 10000 hadi 100000.ongezeko la postmortem allowance limewashangaza madaktari kwani kwa mujibu wa viongozi wao,hawakuwahi kuomba ongezeko la posho hiyo na pia hawakuwahi kulipwa posho ya mamna hiyo.
Kwa upande wangu nimeshtushwa na aliyeweka huu mpangilio wa hizi posho mbili alidhamiria nini haswa.
Yaani daktari akiitwa kufanya upasuaji wenye kuokoa maisha mfano(c-section) analipwa 25000.halafu daktari huyo huyo akiitwa kufanya upasuaji wa kuchunguza maiti anapewa 100000,hivi hapa unategemea madaktari watapendelea kuokoa maisha au kusubiri vifo vitokee wavichunguze?
Hawa watunga sera hufanya kazi zao gizani wakiwa wamelala au wamelewa.
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
Ni hivi majuzi tulisikia kutoka bungeni kupitia kwa waziri wa afya ndg mwinyi na pengine waziri mkuu ndg Pinda kuwa posho ya uchunguzi wa maiti(postmortem allowance) imeongezwa kutoka 10000 hadi 100000.ongezeko la postmortem allowance limewashangaza madaktari kwani kwa mujibu wa viongozi wao,hawakuwahi kuomba ongezeko la posho hiyo na pia hawakuwahi kulipwa posho ya mamna hiyo.
Kwa upande wangu nimeshtushwa na aliyeweka huu mpangilio wa hizi posho mbili alidhamiria nini haswa.
Yaani daktari akiitwa kufanya upasuaji wenye kuokoa maisha mfano(c-section) analipwa 25000.halafu daktari huyo huyo akiitwa kufanya upasuaji wa kuchunguza maiti anapewa 100000,hivi hapa unategemea madaktari watapendelea kuokoa maisha au kusubiri vifo vitokee wavichunguze?
Hawa watunga sera hufanya kazi zao gizani wakiwa wamelala au wamelewa.
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA