Kuoga aoge Rostam, Mengi, halafu watakate waandishi!haki???

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,927
22,075
Kuoga aoge Rostam, Mengi, halafu watakate waandishi!
Imeandikwa na Neophitius Kyaruzi; Tarehe: 5th May 2009




http://habarileo.co.tz/michezo/?n=244
Hakuna ubishi kwamba hivi sasa nchini, habari zinazotamba katika vyombo vya habari ni zile zinazozungumzia suala la ufisadi nchini. Kutokana na ukweli huo, kwa miezi kadhaa sasa, vyombo vingi vya habari vimekuwa vikifuatilia habari hizo kwa karibu na kuzichapisha au kuzitangaza kwa lengo la kuongeza mauzo au kujipatia umaarufu kwa njia moja au nyingine. Pia kuisaidia jamii.

Lakini jambo baya zaidi ni kwamba sasa inaonekana wazi kuwa vyombo vingi vya habari vimeanza kupoteza mwelekeo, kwani katika siku za hivi karibuni, suala la maslahi ya taifa limewekwa pembeni hivyo kinachoangaliwa zaidi ni maslahi ya kibiashara tu. Kibaya zaidi ni kwamba baadhi ya vyombo vya habari vimejiingiza katika mijadala hiyo bila kujua kwamba ina athari gani kwa taifa letu.

Katika hoja yangu, napenda nizungumzie mvutano uliopo sasa kati ya wafanyabiashara maarufu nchini, Rostam Aziz na Reginald Mengi ambao kwa sasa umeshika kasi kubwa kiasi kwamba kwa siku kadhaa kumekuwapo na majibizano kati yao kupitia vyombo vya habari. Ingawa Waingereza wanasema “big names make news” (majina makubwa hutengeneza habari), wakati umefika sasa kwa vyombo vya habari nchini kuwa makini katika ufuatiliaji na uchapishaji wa habari za watu hawa wenye majina makubwa.

Sitoi hoja hii kwa lengo la kutaka suala hilo lisijadiliwe, bali ninachotahadharisha ni kwamba kwa jinsi mjadala unavyokwenda umehama kutoka katika maslahi ya taifa, na sasa yameibuka malumbano ambayo kwa kiasi kikubwa yanachochewa na vyombo vya habari. Kuna faida gani kwa waandishi? Yanatusaidia kweli? Hebu tutazame jamani, tusije tukafananishwa na paka wa hoteli, ambao hukaa meza yenye chakula na kama mahali hakuna chakula hawakai. Ni ukweli usiopingika kwamba kila mfanyabiashara kati ya hawa wawili ana wafuasi wake na jinsi mjadala unavyozidi kupanuka, wafuasi wao wanazidi kuongezeka.

Hii inatokana na uhusiano ulipo kati ya mtu mmoja mmoja au kundi la watu na mfanyabiashara mmojawapo au jinsi mmoja kati yao anavyoweza kuchanga karata zake mbele ya vyombo vya habari hivyo kufanikiwa kuushawishi umma ili uamini maelezo yake dhidi ya mwingine. Hii ni hatari kubwa! Kinachojitokeza ni kwamba hivi sasa vyombo vyetu vya habari vimeacha kuibua mijadala ya masuala yanayohusu maslahi ya taifa kama vile hali ya uchumi wa taifa letu na jinsi ya kujikwamua katika uchumi wa dunia ulioporomoka, badala yake nguvu zote zimeelekezwa kwa watu hawa wawili.

Kila kukicha vyombo vya habari vinafuatilia nani atajibu nini juu ya tuhuma zinazomkabili. Vyombo vyetu vya habari vimegeuka waendesha mashitaka ambao huwauliza maswali wahutumiwa ili kujenga hoja mbele ya hakimu au jaji. Vyombo hivi vimesahau kabisa kwamba malumbano yanayoendelea sasa yanapaswa kusikilizwa mahakamani badala ya vyombo vya habari kuyatangaza hivyo kuongeza uchonganishi kati ya watu hawa wawili matajiri, kwa maisha ya Kitanzania.

Kama itakumbukwa kutokana na nguvu ya malumbano hayo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliulizwa bungeni kuhusu mwenendo wa mjadala huo, naye alisema ni wajibu wa aliyetuhumiwa kwenda mahakamani kulalamika na kuonya kwamba si vyema masuala yalioko mahakamani kuzungumzwa na mtu yeyote. Ingawa alijibu kwa ufupi, kauli yake ilikuwa na maana kubwa kwani hakuna atakayetupatia ufumbuzi zaidi ya mahakama. Kwa kuwa kila mtu anasema kwamba anao ushahidi dhidi ya matendo ya kifisadi ya mwenzake, aende akatoe taarifa kwenye vyombo vya dola ili sheria ichukue mkondo wake badala ya kuuondoa umma katika ajenda muhimu za kijamii na kujadili mambo yao ambayo yanahitaji ufumbuzi wa kisheria.

Hatuna haja ya kujadili tuhuma zinazomkabili mmoja kati ya hao, kwani wananchi ni wasikilizaji tu na hawana la kufanya juu ya tuhuma hizo. Tunahitaji tuhuma hizo zifikishwe mahakamani na ushahidi wa kutosha ili fisadi wa kweli atumikie adhabu kutokana na ukubwa wa makosa yake. Vyombo vya habari bado vina kazi kubwa ya kuibua changamoto zinazowakabili Watanzania badala ya kung’ang’ania mivutano hiyo ambayo mwisho wake haujulikani. Vyombo vya habari havina budi kubadilika, Tanzania si ya watu wawili tu walio katika neema, ina watu wengi masikini ambao sauti zao hazisikiki popote, ambao wanahitaji kusikika kupitia vyombo hivi.

Ni vyema sasa waandishi tukawa makini katika mjadala huu, kwangu mimi nasema Mengi na Rostam wameoga, sasa waandishi iweje tutakate sisi? Ikumbukwe kwamba mwisho wa siku tutageukana sisi kwa sisi, na jambo hilo limeshaanza kujitokeza kwani baadhi yetu wameshaanza kujibizana kwenye magazeti tena kwa kukashfiana. 'Any way', tumeyataka wenyewe! Tusipeleke dhahabu kwa mhunzi badala ya sonara, tutakuwa tunakosea. Mhunzi kazi yake ni kufua vyuma, jambo la msingi ni kuwaambia waungwana hawa wapeleke mambo yao mahakamani. Lakini jambo la msingi kwa Mengi na Rostam hakuna haja ya kulaani giza, bali wawashe mshumaa. Maana yangu ni kuwa kama nilivyoeleza wasitupiane maneno makali, waende mahakamani, kwisha. Naomba kutoa hoja, nikiamini msema yote husifiwa na wachache. Ukweli ndio huo!
 
Jamani sasa huu mvutano unataka kutugawa watanzania.Watu wanaanza kujadili ukabila>Ooh eti mengi ni mchaga ana upendeleo nk.Hebu nyie weusi wa TZ mjiulize nani mkabila kati ya Mengi na Wahindi.Wala tusifike mbali kimaslahi,hakuna muhindi anayependa kuolewa au na MTZ na akikutwa na MTZ anatengwa kwao.Wahindi hawa ndo wanawachezea dada zetu kutokana na fweza zao ila hawataki hata kusikia sie tunaongea na dada zao.Je! huu si ukabila?WatZ wakifanya kazi kwa wahindi mishahara ni tofauti na Wahindi.MTZ akilipwa 100,000.00 muhindi of the same level anapata 1,000,000.00.Leo WaTZ mnakaa kuwatetea hawa Manguruwe.

Mbaya zaidi wanaochangia humu ndani waafrika wengi ndo wanabainisha ukabila just kwa sababu alotoa malalamiko ni Mchaga.E bwana e,mi si mchaga ila usiombe ukakujua uchagani.This chagas are fighters of life.they are very much behind other Tanzanians.Watetapakaa every periferry of this country and across the border.Kwa upande wa elimu wapo,biashara they are TZ one.Na wana uwezo wa kufocus thas why mengi amefocus na kuamua kuweka wazi.Their are jelous.Nani Mtz anaweza kuwatikisa hawa wanaoitwa mafisadi papa!!!Unajua hata Mungu alisema mwenye nacho huongezewa na asokuwa nacho hunyanganywa hata alichonacho.Hii niwazi hata kwa hili.Mwenye nacho anawatetea msokuwa nacho ili mgawane sawa kile walichotuibia mafisadi,ajabu ni kuwa mnamtetea yule alokuwa nacho(alichotuibia) ili aendelee kuwa nacho!!!!!!!!!!!!

Hapa tunataka watanzania wote tufanane na wachaga na wahindi.watu mnaendelea kula mlo mmoja kwa siku na kusihi kwenye mbavu za mbwa ila bado hamtaki kutoka huko mnang'ang'ania mafisadi.

Wachaga wametupiga bao uongo si kazi na tuache wivu.Ukienda sahemu yoyote TZ hii huwezi kupata huduma nzuri kama hamna mchaga.Nani anapinga hilo?

Wachaga wakihamisha biashara na nyumba zao Dar panabaki kama mkuranga.Nani anabisha hilo?This people are civilised.

Hapa tuchangie hoja ya magabacholi ku-expatriet our resources.That is the issue
 
Mvutano huu wa RM na RA ni wa maana sana katika ukombozi mpya wa nchi yetu maana kuna anayesema ukweli na msema ukweli.Pia Mengi amesaidia kufungua mdomo wa RA ulikuwa umeziba,sasa tunasubiri atuambia anafanya biashara zipi na kampuni zake ni zipi na ziko wapi.Biashara za RM zinafahamika,ayataje kabla ya kumfuata Ditopile na Kolimba.
 
Da...
Waandishi kweli mnayo.
Sisi tulikuwa tunawaangalia tu jinsi mlivyo hodari wa kujipendekeza kwa mafisadi mamba na kenge.
Lakini tusimame sisi kama sisi, tuupige vita ufisadi kwani kila fisadi anashiriki kikamilifu kudororesha hali zet.
 
Mjadala ni heathy kwa taifa. Mengi ana ajenda yake ambayo anaipush kwa umma, amini usiamini, kwa wenye busara na kujiuliza mara mbilimbili 'what is the motive behind' unapata jibu issue sio mafisadi papa bali mlezi wa mafisadi papa mzee anauma huku akipulizia na kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa.
Mengi ni fisadi na Rostam ni fisadi. Siungi mkono Mengi kuwataja mafisadi, bali pia Rostam kujibu vile vile, wote ni wajinga hawa. Hatari ya Mengi iko kwa Jeeth Patel, kesi yake ya EPA itaisha, atashinda kesi, hatatoa majibu kwa tuhuma za Mengi, hatafanya press conference wala hata kwenda mahakamani, tusubiri kitakacho tokea.
Nadhani Jeethu Patel ni mmoja wa 5 powerful men in Tanzania who are filthy rich and cool silent. wengine wa aina hii ni Fida Hussein na mtu anayeitwa Yokhes Manik.
Waandishi wetu, hiki ni kipindi cha mavuno mpaka uchaguzi mkuu upite.
 
Mjadala ni heathy kwa taifa. Mengi ana ajenda yake ambayo anaipush kwa umma, amini usiamini, kwa wenye busara na kujiuliza mara mbilimbili 'what is the motive behind' unapata jibu issue sio mafisadi papa bali mlezi wa mafisadi papa mzee anauma huku akipulizia na kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa.
Mengi ni fisadi na Rostam ni fisadi. Siungi mkono Mengi kuwataja mafisadi, bali pia Rostam kujibu vile vile, wote ni wajinga hawa. Hatari ya Mengi iko kwa Jeeth Patel, kesi yake ya EPA itaisha, atashinda kesi, hatatoa majibu kwa tuhuma za Mengi, hatafanya press conference wala hata kwenda mahakamani, tusubiri kitakacho tokea.
Nadhani Jeethu Patel ni mmoja wa 5 powerful men in Tanzania who are filthy rich and cool silent. wengine wa aina hii ni Fida Hussein na mtu anayeitwa Yokhes Manik.
Waandishi wetu, hiki ni kipindi cha mavuno mpaka uchaguzi mkuu upite.
yogesh manek....huyu anamiliki mac group of companies which includes;
exim bank, chemi and cotex, heritage insurance, strategies insurance,....

vipi kwani naye ni papa au nyangumi????
 
Binafsi Naunga mkono kuwataja mafisadi (Name and shaming) kama kuna ushahidi wa wazi...

Isitoshe mengi si mtu wa kwanza kuwataja akina RA... Alichofanya ni ku-paraphrase tu yaliyokwisha sema huko nyuma na akina Dr Slaa...

RA na wengine wanatakiwa wam-sue Mengi kwa defamation kama wana hakika aliyoyasema ni uzushi ...

Hata kama wakimshitaki hawatashinda maana mengi atasema alichokisema yaani tuhuma alizozisema si yeye bali ni hearsay ambayo mahakamani is not admissible... Kesi kwisha na mengi kupiga matalumbeta...

Labda ndo maana akina RA wamekimbilia Takukuru ambako wanajua sio competent kiasi hicho...

Nilisikia pia Ra akihoji moral authority ya mengi kumsema.. Hivi Mtu anapataje moral authority ? Yaani inabidi ukae kimya na mawazo yako bonafsi kama hukuchaguliwa na wananchi kama RA? Moral authority inapatikana pia kutokana na standing ya mtu katika jamii hivyo RA sidhani kama yeye ana hiyo moral authority ya kumkemea mengi ili hali akijua kwamba anatuhumiwa ameiba fedha za umma katika utapeli...

Kama mengi alichukua mikopo, ni juu ya tasisi hizo zilizomkopesha kumdai na kumlimbikizia Riba na sio vinginevyo kwa mtu kama RA kutoa mambo ambayo hayahusiani...

Mwisho... details a mengi RA kazitoa wapi? maana navyofahamu ni kwamba unapoomba mkopo ni kakubaliano kati yako na bank au mkopeshaji na itakuwa breach of confidentiality or privacy kwa mkoposhaji kutoa au kuanika hadharani makubaliano yenu bila idhaa za wahusika wote... Je mengi aliridhia madeni hayo yawe public knowledge? kama ni ndio je wakopeshaji walimuarifu mengi kwamba wata-share datas na RA?

Kama jibu ni hapana basi RA katumia umafia kuzipata data hizo za mengi ambapo wanazishikilia data hizo inabidi waulizwe iweje RA kuwa na data za Mengi bila idhini yake...

Huu waweza kuwa pia ni ufisadi mwingine ambapo RA anaweza kuwa ameufanya maana inaoneka amehangaika sana kutafuta kumu-expose mengi...

Fahari wawili wakigombana, ziumiazo ni nyasi... Walaji nyasi ni sisi watanzania maskini kama alivyosema Basil Pesambili mramba... Hivyo wao waendelee kurumbana na hatimaye watuambie wanahusikaje kuidhulumu TZ yetu na wakubali pia kukiri makosa yao kama moral authority inavyowasukuma na wakubali kuzirudisha pesa zetu...

Asanteni..
 
Back
Top Bottom