Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Juzi siku ya Ijumaa ya tarehe 23/9/2011 usiku katika kipindi cha Kipima Joto cha ITV kilichokuwa kikiongozwa na Reinfred Masako, mmoja wa wachangiaji katika mjadala huo mama Rehema Mwateba kutoka mtandao wa kijinsia wa TGNP alizungumzia jambo ambalo limekuwa likipigiwa kelele na wanawake kila uchao.
Mfumo Dume, ndio kilio kikubwa cha mama huyo, kilichonisisimua ni pale alipotoa mfano wa jinsi mwanamke anavyobebeshwa majukumu ya kutunza familia kule Rungwe huku kina baba wakifuja fedha kwa ulevi.
Akiongea kwa uchungu mama huyo alidai kuwa kuna hata msemo unatumiwa na akina baba kule Rungwe wakiwa kwenye vilabu vya pombe, hujisifu kwa kusema, "Kunywa pombe, watoto wakitembea uchi atajua mama yao" (Neno hili alilitamka kwa lugha inayotumiwa na wakazi wa hapo Rungwe na alilitolea tafsiri)
Hii inadhihirisha ni kiasi gani mwanamke anabebeshwa majukumu kiuonevu, huku wanaume wakitanua na ulevi na pengine nyumba ndogo.
Mfumo Dume, ndio kilio kikubwa cha mama huyo, kilichonisisimua ni pale alipotoa mfano wa jinsi mwanamke anavyobebeshwa majukumu ya kutunza familia kule Rungwe huku kina baba wakifuja fedha kwa ulevi.
Akiongea kwa uchungu mama huyo alidai kuwa kuna hata msemo unatumiwa na akina baba kule Rungwe wakiwa kwenye vilabu vya pombe, hujisifu kwa kusema, "Kunywa pombe, watoto wakitembea uchi atajua mama yao" (Neno hili alilitamka kwa lugha inayotumiwa na wakazi wa hapo Rungwe na alilitolea tafsiri)
Hii inadhihirisha ni kiasi gani mwanamke anabebeshwa majukumu kiuonevu, huku wanaume wakitanua na ulevi na pengine nyumba ndogo.