Kununua magazeti siku hizi ni kupoteza pesa yako

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,848
15,257
Mfumo wa chama kimoja utafanya maisha ya mtanzania kubadilika kabisa, kiuchumi, kijamii nk.

Tukiongelea upande wa magazeti hamna kipya kwa kweli, habari ni zile zile na watu ni wale wale tutakaowasikia. Hiyo ni mbaya maana itapelekea watu kutonunua magazeti na mwisho wake waandishi kwenye kampuni hizo kupunguzwa ili kuenenda na gap.

Zile habari za kiuchunguzi na kukosoa serikali na viongozi hakuna tena, zimebaki zile za kupamba serikali na viongozi wake tu

Watu wengi wanaona ni bora kuingia YouTube na mitandao Mingine ambayo habari hazijaelemea upande mmoja ili kupata wanachohitaji
 
Mfumo wa chama kimoja utafanya maisha ya mtanzania kubadilika kabisa, kiuchumi, kijamii nk.

Tukiongelea upande wa magazeti hamna kipya kwa kweli, habari ni zile zile na watu ni wale wale tutakaowasikia. Hiyo ni mbaya maana itapelekea watu kutonunua magazeti na mwisho wake waandishi kwenye kampuni hizo kupunguzwa ili kuenenda na gap.

Zile habari za kiuchunguzi na kukosoa serikali na viongozi hakuna tena, zimebaki zile za kupamba serikali na viongozi wake tu

Watu wengi wanaona ni bora kuingia YouTube na mitandao Mingine ambayo habari hazijaelemea upande mmoja ili kupata wanachohitaji
Una uhakika wa 100% kuwa Siku hizi hakuna Magazeti ya 'Kuikosoa' Serikali? Tatizo lenu mnalazimisha mnayoyataka na siyo 'Maadili' yanavyotaka.
 
Kwani ili gazeti liuze ni lazima liikosoe serikali ? Tatizo mnapenda umbea tu wa siri za nchi. Nchi ipo kwenye mikono salama, pigeni kazi na someni magazeti yanayotangaza mema ya nchi.
IMG_20201118_102439.jpg

IMG_20201118_102416.jpg
 
Magazeti na Media zote wanaleta habari za mapambio.

Huko tunapoelekea hayo mapambio watasikilizana wenyewe!
 
Tangu kipindi kile magazeti yalivokuwa yanaedit picha za mbele kiuongo ili kuvutis Wateja, afu ukisoma kwa ndani unakuta " inasemekana"


Mfyuuuuuu.
 
Back
Top Bottom