Kunguru na Mwewe wanashambulia sana vifaranga wangu

Kuna mbinu hii itumie mkuu nunua pumba na asubuhi usiwatoe wape pumba halafu usiwafungulie nje na hao kunguru na mwewe muda wao wa kutafuta chakula kuanzia saa nne asubuhi mpaka saa nane mchana halafu wewe wafungulie kuku wako kila siku saa kumi na mpaka saa kumi na mbili halafu kuwa nao makini kwa muda huu kunguru na mwewe watakuwa wachache au wameshiba.
Ushauri mzuri mkuu naomba kuboresha kidogo. Pumba yenyewe tuu haitoshelezi unaweza kununua chakula cha kuanzishia vifaranga au kuwachanganyia mchanganyiko ambapo watapata lishe ya kutosha. Cheki hapa jf unaweza kupata formula ukachanganya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom