Kunani Wizara ya AFYA??

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,592
29,712
Nimesoma ktk Mwananchi la leo kuwa wale wahanga wa kifo cha mama mjamzito na kichanga pale Mwananyamala Hosipitali wamelazimishwa kuhongwa dizel lita 120 za kusafirisha maiti, pia walitishwa kwamba wakikataa kufuta ile taarifa yao ktk vyombo vya habari watazuiwa kuchukua marehemu mpaka afanyiwe uchunguzi.

Pia walilazimishwa kumtaja aliyepeleka taarifa kwa umma kuhusu hiyo default. Behind all this yupo Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Noel Mahyenga. Hii ni aibu kwa serikali na ni KASHFA kwa Wizara ya Afya na Wizara ya Mambo ya Ndani pamoja na ile ya Wanawake na Watoto.

nimejitahidi kutafuta source yake online nimeikosa, kama kuna mtu anaweza kuscan ule ukurasa wa kwanza na wapili aweke hapa wanabodi wauone as source.

Ninafuatilia sana hizi takataka za wanaafya kwani kwa uzembe wao nimepoteza Binti yangu na marafiki zangu wengi wamkumbana na mikasa hii. Je wewe hili tatizo halijawahi kukutokea au hata kwa mtu unayemfahamu??? Tuchangie uzoefu hapa ili tulenge suluhisho.

Naomba kuwasilisha
 
Last edited:
Back
Top Bottom