Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,597
- 215,272
Kuna dada msomi mwenye career yake, mume na watoto wawili. Wana nyumba nzuri watoto wanasoma shule nzuri. Maisha yake aliyaona yamekamilika. Mpaka siku alipokua na shida na msichana wa kazi.
Alikuja binti alikabithiwa na Mkatekista kanisani. Binti mlugaluga, amevaa yeboyebo, Amesuka tweede kilioni na nguo ameweka kwenye mfuko wa Rambo. Binti haongei hata Kiswahili vizuri kwenye R anaweka L.
Wamefika nyumbani amemfundisha kazi, alimuacha kwa amani. Asilolijua binti ni mchepuko wa mume wake na alisoma mpaka kidato cha sita ila hana ajira. Ana tiririka Kiingereza na Kifaransa vizuri tu.
Kitu nisichoelewa sijui Mkatekista aliufahamu mchezo mzima!
-----
Ni hivi, hii familia inaishi kwenye nyumba ya vyumba vitatu vya kulala. Master’s bedroom na kila mtoto ana chumba chake. Nje kuna servants quater ambayo kwa makusudi farther house aliitoa kwa mlinzi wao.
Mama alishauri dada anunuliwe kitanda alale na binti yake. Mume aliamua kununua double decker na kumwambia wa kiume alale juu wa kike chini ili dada apate chumba chake.
Maisha yaliendelea. Dada akiulizwa umepika nini leo anasema mahalage. Mama ali under value mdada mpaka kumteta Kizungu na mume we lakini mume hajibu.
Ni baada ya dada kupata mimba. Mama alimchapa kibao katika interrogation ya kumtaja mhudumu. Hii ni baada ya kuishi pamoja kwa miaka miwili na mshahara wa laki mbili kwa mwezi. Dada wa kazi kufungua don’t you dare touch me again! Mama anauliza hiki Kizungu ulijifunza wapi ndipo kuambiwa CV halisi ya dada wa kazi na mhusika wa hii mimba ni mume wako.
Alikuja binti alikabithiwa na Mkatekista kanisani. Binti mlugaluga, amevaa yeboyebo, Amesuka tweede kilioni na nguo ameweka kwenye mfuko wa Rambo. Binti haongei hata Kiswahili vizuri kwenye R anaweka L.
Wamefika nyumbani amemfundisha kazi, alimuacha kwa amani. Asilolijua binti ni mchepuko wa mume wake na alisoma mpaka kidato cha sita ila hana ajira. Ana tiririka Kiingereza na Kifaransa vizuri tu.
Kitu nisichoelewa sijui Mkatekista aliufahamu mchezo mzima!
-----
Ni hivi, hii familia inaishi kwenye nyumba ya vyumba vitatu vya kulala. Master’s bedroom na kila mtoto ana chumba chake. Nje kuna servants quater ambayo kwa makusudi farther house aliitoa kwa mlinzi wao.
Mama alishauri dada anunuliwe kitanda alale na binti yake. Mume aliamua kununua double decker na kumwambia wa kiume alale juu wa kike chini ili dada apate chumba chake.
Maisha yaliendelea. Dada akiulizwa umepika nini leo anasema mahalage. Mama ali under value mdada mpaka kumteta Kizungu na mume we lakini mume hajibu.
Ni baada ya dada kupata mimba. Mama alimchapa kibao katika interrogation ya kumtaja mhudumu. Hii ni baada ya kuishi pamoja kwa miaka miwili na mshahara wa laki mbili kwa mwezi. Dada wa kazi kufungua don’t you dare touch me again! Mama anauliza hiki Kizungu ulijifunza wapi ndipo kuambiwa CV halisi ya dada wa kazi na mhusika wa hii mimba ni mume wako.