Kuna watu wameshangaa Maria Sarungi kupewa Mkuki na Ngao!

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,434
7,055
Watu hawana dogo!

Jana THRDC wametoa tuzo kutambua mchango wa wanaharakati wanaotetea haki za binadamu kupitia platforms mbalimbali.

Miongoni mwa waliopokea tuzo hiyo ni Mwanaharakati Maria Sarungi ambaye alitambuliwa kwa kupaza sauti kupitia mtandao wa Twitter.

Tuzo haina shida. Wapo walioona nembo ya tuzo ambayo ni Mkuki na Ngao haikupendeza kwa mwanamke hasa kwa kuzingatia mila na desturi za kiafrika.

"Hii tuzo iliyotolewa kwa akina Maria ni ya ajabu! Mtu kupewa Mkuki na Ngao ni ishara ya mwanaume wa kiafrica anayeenda vitani. Kwa asili yetu, mwanamke wa kiafrica hapewi mkuki na ngao" ameandika mdau mmoja kwenye mitandao ya kijamii akiambatanisha na picha ya Maria akiwa amesimama na tuzo hiyo kama inavyoonekana kwenye Uzi huu.

Mwingine akaongeza;

"Waandaaji wanatoa tuzo bila kuzingatia Maadili ya Kitanzania. Tafsiri ya Mkuki/Ngao/Panga/Upinde inakinzana na fikra za tuzo kwa mwanamke. Ni bora wangempa hiyo tuzo bila kukabidhiwa Mkuki au Ngao!"

Aidha, yupo aliyehoji kama ikitokea mwanaume kupewa tuzo ya chungu, mwiko na ufagio, itakuwa ni sahihi kupokea?

My take: Naona inafikirisha kweli. Je, kuna haja ya waandaaji wa tuzo kama hizi kuzingatia aina ya nembo kulingana na jinsia, tamaduni, mila na desturi?
D5S1PL2WAAEYSjG.jpeg
 
Kushangaa ni jambo la kawaida kwa mwanadamu, kwani sio kila mtu anakuwa na mawazo sawa na mwenziwe katika kuwaza na kufikiri, kwako anaweza kuwa mbaya ila kwa mwengine kuwa mzuri sana.

Mchango wa Maria ni mkubwa san hasa kwa vijana ambao ni taifa la leo kwani sio kila mtu ambaye anakuwa na uwezo wa kupata na kuchambua habari kwa kina kama afanyavyo Aunt wa Taifa
 
Kushangaa ni jambo la kawaida kwa mwanadamu, kwani sio kila mtu anakuwa na mawazo sawa na mwenziwe katika kuwaza na kufikiri, kwako anaweza kuwa mbaya ila kwa mwengine kuwa mzuri sana.

Mchango wa Maria ni mkubwa san hasa kwa vijana ambao ni taifa la leo kwani sio kila mtu ambaye anakuwa na uwezo wa kupata na kuchambua habari kwa kina kama afanyavyo Aunt wa Taifa
Na nembo?
 
Hiyo tuzo ya Ngao na Mkuki kupewa mwanamke wa kiafrika unaizungumziaje?
kapewa ngao na mkuki kama ishara ya kukubali uwezo wake wa kuchanganua mambo ya kitaifa na kimataifa na sijaona shida kwa mwanamke kupata ngao na mkuki kwa kweli. Thamani ya kazi yake ndo imempa heshima yake
 
kapewa ngao na mkuki kama ishara ya kukubali uwezo wake wa kuchanganua mambo ya kitaifa na kimataifa na sijaona shida kwa mwanamke kupata ngao na mkuki kwa kweli. Thamani ya kazi yake ndo imempa heshima yake
Kwahiyo hukubaliani na wanaodhani kwamba inamchoresha kupewa zawadi ya kiume, siyo?
 
Kwahiyo hukubaliani na wanaodhani kwamba inamchoresha kupewa zawadi ya kiume, siyo?
huo ni mfumo dume kudhani kwamba kupewa mkuki na ngao ni kwa ajili ya wanaume tu, cha kwanza kujiuliza hao wanaume wanaopewa hupewa kwa sababu gani zamsingi? Ni k wamba kuna jambo la kishujaa mbalo wamefanya na thamani ya jambo lenyewe ni mkuki na ngao, na bahati nzuri shangazi naye anafanya na anaendelea kufanya jambo la kishujaa basi lazima apewe thamani inayoendana na ushujaa wake ambao ni mkuki na ngao sasa shida iko wapi? Shida ni kwamba watu bado wanafanya kazi kwa kukariri
 
huo ni mfumo dume kudhani kwamba kupewa mkuki na ngao ni kwa ajili ya wanaume tu, cha kwanza kujiuliza hao wanaume wanaopewa hupewa kwa sababu gani zamsingi? Ni k wamba kuna jambo la kishujaa mbalo wamefanya na thamani ya jambo lenyewe ni mkuki na ngao, na bahati nzuri shangazi naye anafanya na anaendelea kufanya jambo la kishujaa basi lazima apewe thamani inayoendana na ushujaa wake ambao ni mkuki na ngao sasa shida iko wapi? Shida ni kwamba watu bado wanafanya kazi kwa kukariri
Me nadhani it is a bit unfair kumtunuku zawadi ambayo itampa taswira ya mabavu.. Mwanamke kiasili sio mtu wa mabavu.. Ngao na Mkuki ni alama ya mabavu..

Naamini angeweza kupewa award kwa ushujaa wake bila kumpa taswira yenye ukakasi.. Kumpa Ngao na Mkuki inaweza kumuondelea hata ile pride yake as a woman..

Halafu, hivi kumfananisha mwanamke na mwanaume ndio usawa wa kijinsia? Sio kumdhalilisha kweli?
 
But angeweza kupewa tuzo isiyotweza nafasi yake kama mwanamke!
Kwani kule anapigana kama mwanamke au anapigana kama askari? Kuna tofauti yoyote kati ya harakati anazofanya yeye na wanazofanya wanaume? Kwa hiyo unataka kusema siku wakiwapa tuzo ma spika wa bunge Anne Makinda apewe tuzo yake peke yake wakati kazi aliyoifanya ni ile ile?
 
lazima na ni haki kushangaa. dunia nzima kazi ya kulinda ni mwanaume!! ngao, sime , mkuki nui mwanaume. Mpe mwanamke kuchinja kuku uone atakavyotimua mbio! mpe mkuki akamchome adui!!, au kwa vile leo hii wanaandikishwa jeshi basi!!
angepewa mwiko, kinu, ungo, ndiyo tungeelewa. mfano melo angepewa mwiko, kinu, ungo tungeshangaa!! haya mademokrasia na mausawa haya mpaka tunapoteza dira!! HATA MIMI NASHANGAA!!!
 
Back
Top Bottom