Kuna Wanawake Mungu Kaumba!

imhotep

JF-Expert Member
Oct 13, 2012
46,678
71,032
Niliingia Ofisi Moja Maeneo ya KAMATA nilikuwa nafuatilia Shughuli zangu,jamaa nilishaongea nae Kwenye Simu akasema Njoo.

Nikidandia BodaBoda ya Dogo Mmoja Mjanja sana halafu huwa anajua kukichezea Chombo Kile na kuwakwepa Maaskari wa jiji na Control ndio usiseme.

Vuuup!...Mpaka Jengoni nikaanza kuulizia Pale Chini ile Kampuni iko Ghorofa ya Ngapi nikaelekezwa bhana nikapanda ngazi haraka haraka

Kufika kule nikaona Bango nikaingia Kilichonipeleka pale GHAFLA! nikakisahau,, Yule Binti Ni Mzuri!! Sijui kama alihisi..Nikamuomba Maji ya Kunywa akasimama eeeh Bwana wee...yaani Sura Nzuri sauti nzuri figa Zuri Mgongo mzuri akaenda kuniletea maji.

Mimi nikasema Moyoni kwanza jali kilichokuleta nikamuuliza Bossi nilieongea nae kama yupo akasema katoka kidogo

"Msubiri hatochelewa"..Tukaanza kuongelea Mambo ya Biashara nikayashinda matamanio Thank you God!

Namba nilichukua ila kila nikijaribu niseme niipige Nguvu Mbili ndani ya Mwili wangu zinapingana

Ila No Swaet Mke wangu pia kaumbika na Mwenzake pia kaumbika lakini Uzuri nao Ukipita Kiasi unaweza kutuletea Heart attack yule Binti kidogo aniletee.
 
usijipunje ndugu jaribu bahati yako mamb mazuri hayo kulaaaaa usiache
Roho ilikuwa inaniambia hapa sichomoki kwa hiyo nina Majukumu nikiliongeza na hili..Hapana aliniambia asili yake ni Mnyasa.
Uongo Mbaya Haya ni Maua ya Dunia.
 
ACHANA NAE HUYO MDADA WE JAMAA, FANYA KUNITUPIA NAMBA NIMCHEKI, NTAKULETEA MREJESHO
 
Back
Top Bottom